Shadida Salum
Journalist at JamiiForums
- Sep 11, 2020
- 69
- 104
Mashindano ya CHAN awali ilikuwa yafanyike kuanzia tarehe 4 hadi 25 mwezi Aprili 2020 nchini Cameroon lakini CAF ilitangaza kuahirisha mashindano hayo hadi Januari 16, 2021 kutokana na janga la COVID-19.
Awali Ethiopia ilipewa nafasi ya kuwa mwenyeji wa mashindano hayo lakini Shirikisho la soka nchini humo, EFF lilikiri kwamba haikuwa tayari kuandaa mashindano hayo na nafasi yake kupewa Cameroon kuwa mwenyeji wa michuano hiyo.
CHAN, tofauti na Kombe la Mataifa ya Afrika, timu za kitaifa zinazoshindana lazima ziwe na wachezaji wanaocheza ligi yao ya nyumbani pekee.