TAIFA STARS: Tatizo kocha au wachezaji?

TAIFA STARS: Tatizo kocha au wachezaji?

Ulimakafu

JF-Expert Member
Joined
Mar 18, 2011
Posts
31,701
Reaction score
13,672
Hii timu baada ya kuchukuliwa na babu Jan Poulsen imekuwa kama homa ya kipindi, tunashindwa hata na Chad nyumbani?

Tatizo mi silielewi kama ni kocha, mfumo au wachezaji wanaounda kikosi hicho.
 
Mi naona tatizo ni wachezaji, tutabadilisha makocha mpaka basi ila tusipobadili system nzima ya mpira wetu hatutafika popote!

Huwezi kua na wachezaji ambao wanafanya mazoezi kwenye viwanja vibovu kabisa, hawana diet ya kimichezo ila ni kula chips mitaani, hawana ari ya ushindi kwasababu wanajua hata wakishinda hawana maslahi ya kueleweka na vingine vingi!!
 
kocha mgonjwa huyu bwana...hawezi kazi
 
kocha mgonjwa huyu bwana...hawezi kazi

Kaka embu tuambiane hapa kocha gani tulishawahi kusema ameweza kazi? Nakumbuka paulsen alovyoshinda challenge tulisema kocha mzuri ila leo hafai
 
Kaka embu tuambiane hapa kocha gani tulishawahi kusema ameweza kazi? Nakumbuka paulsen alovyoshinda challenge tulisema kocha mzuri ila leo hafai
Alibahatisha....
 
hii timu baada ya kuchukuliwa na babu jan poulsen imekuwa kama homa ya kipindi,tunashindwa hata na chad nyumbani?tatizo mi silielewi kama ni kocha,mfumo au wachezaji wanaounda kikosi hicho.

ushawahi kumtongozea mtu alafu aakaenda guest house na jimama likamshinda
tatizo linakuwa kwa nani msaada pls??
 
Kwa kweli taifa stars mimi siipendi kabisa, jana kuna shabiki mmoja wakati wa mapumziko radio free afrika alicomment akiitakia ushindi chad kwani aliona ni jinsi gani timu inavyocheza kwa kubahatisha, fukuzeni huyo babu poulsen, hana faida kwa timu yetu, tunategemea nini tukijapambana ivory coast au morocco kwa timu mavi kama hii?
 
Tatizo wote wawili...Kocha na Wachezaji
1.kocha....hana mbinu mbadala....mfumo wake haueleweki...
2.wachezaji...baadhi hawana sifa tena za kucheza stars...Mfano...Machupa..kafunga goli ngapi ligi ya huko swedeni?...na yuko Kikosi cha kwanza katika timu yake?
..Jiulize kuhusu vietnam ligi yao...Timu ya babi na Mrwanda ..inashuka daraja...je wanaisaidiaje timu zao?

Ukweli ni kwamba hatuna wachezaji wenye ushindani

CECAFA...wadau wa mpira tunajua ...nini kilifanyika kuchukua kombe lile..na sasa watu wamipango wana malumbano na TFF..tegemea Vichapo CECAFA...nitarudi baadae
 
Timu gani ambayo haichezi mechi za kimataifa? Inaingia kambini wiki moja kabla ya mechi? Piga chini Tenga, kisha tuitishe uchaguzi mpyaa
 
Makocha huwa wanazeekea Kwenye Timu sasa huyo Poulsen ndo kwanza anafundisha timu kubwa bora aende kwao tatizo ni Makocha wa Bei Rahisi.
 
Kabla ya kumponda kocha tujiulize tulishafanya nini kimataifa?CECAFA mara 2,CAF mara 1.Simba na Yanga wamefanya nini kimataifa?

Je kuna mchezaji hata mmoja wa Kitanzania aliyewahi kung'aa kwenye ligi ngumu? Hatuna mfumo wa soka, hatuna viongozi makini. Vimashindano vya vijana ni utani mtupu.

Ok,tunasema kocha wa bei rahisi,kocha gani wa kiwango cha juu atakuja kuharibu Cv yake hapa,Maximo ametoka hapa amekosa timu kabisa kwa sababu hakufanya lolote.

Hao wazawa wanaolilia kupewa timu wamefanya nini? Kama hawawezi hata kuvuka mipaka na kufundisha klabu za CECAFA Watawezaje Taifa stars?Kwanza wakasome, wengi wao hata leseni A za CAF hawana.
 
Pale TFF hakuna Mipango...Si Tenga wala Kayuni ambaye ndiye Mkurungenzi wa Ufundi..wamekaa kusuburi Posho na makato ya mechi...
Mipango duni...timu inakosa Tiketi ya kwenda sudani kucheza Friend match...unategemea nn...

Wanashindwa kulea watoto wale wa TSA......Vipi serengeti boys.wapi Ngorongoro Heroes...

Nina Hasira sana....Mbaya zaidi tukiwaambia wanasema majungu...
 
Mfumo nzima ni mbovu kabisa.kocha na wachezaji wabebeshwe lawama. Yaani ile mechi ya jana tumeshindwa kushinda.

Babu Poulsen hana uwezo wa kufundisha national team. TFF kina Tenga hawajali national team wanaangalia vitambi vyao tuu.

Kinachotakiwa sasa ni kufungisha virago Poulsen, Team apewe kocha anayejua soka ya Afrika mwenye mafanikio. Team apewe Patrick Phiri
Ambae anwajua wachezaji wa bongo and has a lot of experience with African foootball.

Kocha aje immedietly, aandae program mapema, achukue wachezaji wenye vipaji na achane na akina machupa,and wachezaji wazee.

Tujenge team mapema around kina Shomari kapombe, nyooso, and other proffesional players. Serengeti wanamwaga pesa kila mtu anataka kufaidika.hiyo kundi tuliyopangwa
Tunaenda kama wasindikizaji..ahh
 
ki Ukweli sisi hatuna Kiu ya soka....Kipindi fulani nilikua na Tinoco pale TFF...kwa maoni yake..anasema Uongozi haulewei na ndio maana akamua kuondoka...lkn akamwambia Kayuni..hakikisha hawa watoto wa COpa Cocacola ambao nimeenda nao Brazili..na wakashinda...na Pia South Africa...

Wachomekeni kwenye Timu za wakubwa ..pia wapewe nafasi..yaani iwe kama Sheria ndogo vile kwamba kila timu isajiri Under 18..wawe nao..na wawe wanapangwa..kuwapa Uzoefu..mpk sasa tungewa na Timu nzuri..matokeoa yake Ndio...haya sasa AIBUU

Si Yanga wala Simba..ambao wana KIU ya mafanikio...angalia usajiri wao...tazama Maandalizi yao....
Azam nao wameingia kwenye Mkumbo huo wa kutaka ubingwa wa haraka haraka...wamesajiri wachezaji wakigeni wote Maboya Tu....
.....Nitarudi Tena
 
Back
Top Bottom