Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,798
- 71,218
Yaliyoipata Taifa Stars ilipofuzu AFCON 2019 hatutaki kuyaona tena yakijirudia.
Safari hii Stars imejishindia safari ya fainali hizo huko Cameroon kwa juhudi zao na hao wanasiasa wakiwa wamesha ikatia tamaa baada ya kuwa imefungwa mechi ya nyumbani.
Kauli za watu kama Makonda kuwa Stars inatekeleza ilani ya CCM ilifanya Wa Tanzania wasio na mapenzi na chama hicho kuona timu imebinafsishwa hivyo hamasa kupotea na kwa kauli hiyo ilifanya Taifa Stars ichukiwe na kundi kubwa la Watanzania hadi kuitolea kejeli mbaya za kuwa nyong'onyeza wachezaji.
Hiyo kamati mnaita ya hamasa ivunjwe na kuundwa mpya ya watu makini wanaoheshimika na jamii ya makundi tofauti na wenye historia na mpira na sio watu wengine ambao hawajui hata wachezaji wako wangapi dimbani.
Siasa iwe mwiko kabisa, mbona nchi zingine hazina siasa michezoni iweje hapa?
Karia kama hawezi kujitoa kwenye makucha ya wanasiasa kama Makonda basi sisi wenye timu (watanzania) tutamtoa yeye.
Safari hii Stars imejishindia safari ya fainali hizo huko Cameroon kwa juhudi zao na hao wanasiasa wakiwa wamesha ikatia tamaa baada ya kuwa imefungwa mechi ya nyumbani.
Kauli za watu kama Makonda kuwa Stars inatekeleza ilani ya CCM ilifanya Wa Tanzania wasio na mapenzi na chama hicho kuona timu imebinafsishwa hivyo hamasa kupotea na kwa kauli hiyo ilifanya Taifa Stars ichukiwe na kundi kubwa la Watanzania hadi kuitolea kejeli mbaya za kuwa nyong'onyeza wachezaji.
Hiyo kamati mnaita ya hamasa ivunjwe na kuundwa mpya ya watu makini wanaoheshimika na jamii ya makundi tofauti na wenye historia na mpira na sio watu wengine ambao hawajui hata wachezaji wako wangapi dimbani.
Siasa iwe mwiko kabisa, mbona nchi zingine hazina siasa michezoni iweje hapa?
Karia kama hawezi kujitoa kwenye makucha ya wanasiasa kama Makonda basi sisi wenye timu (watanzania) tutamtoa yeye.