Taifa stars inaweza chukua AFCON 2019

Tabutupu

JF-Expert Member
Nov 26, 2010
13,107
18,323
Naomba msinipige mawe kabla sijaeleza.

1. Nimeangalia timu zote sijaona timu ambayo ina mastars wengi kama miaka ya nyuma au timu ambayo haifungiki. Timu nyingi zina wachezaji toka timu za kawaida sana labda na star mmoja.

Mfano Nigeria ina Iwobi pekee yake ambaye yupo kwenye timu bora. Wengine ni timu ambazo naweza sema za kawaida.


2. Wakibadili mindset na kuona wao wana haki ya kuchukua kombe na wakakomaa inawezekana.. ninapo sema kukomaa yaani ile mkifungwa mnatoa hadi machozi kama brazil ilivyo fungwa na germany . Sasa utakuta timu imefungwa michezaji inacheka au inapongezana .

3. Wakicheza kama timu na kuacha show off .. watapiga senegal na kenya mabao mengi sana. Ila wasipo cheza kama timu taifa star ni mboga ya kila mtu.

4. Wakiacha ushamba na uzembe watafanya vizuri.

5. Waache kulaumiana.

Ni zamu yetu kubeba kombe.
 
Hugo nikujifariji tu more hata matumaini Haywood kama ndo akina Ulimwengu hakuna kitu pale.
 
Hugo nikujifariji tu more hata matumaini Haywood kama ndo akina Ulimwengu hakuna kitu pale.
Boss.. timu upo vizuri.. ukiona tumefungwa ujue ni ushamba wa vijana wetu tuu.. ila wakijiamini wanatoboa.
 
Me Naona ungetazama kwa mchezaji mmoja mmoja hapo ndo ungegundua ni zamu yetu kufungwa au zamu yetu kufunga
 
Naomba msinipige mawe kabla sijaeleza.

1. Nimeangalia timu zote sijaona timu ambayo ina mastars wengi kama miaka ya nyuma. Timu nyingi zina wachezaji toka timu za kawaida sana labda na star mmoja.

Mfano Nigeria ina Iwobi pekee yake ambaye yupo kwenye timu bora. Wengine ni timu ambazo naweza sema za kawaida.


2. Wakibadili mindset na kuona wao wana haki ya kuchukua kombe na wakakomaa inawezekana.. ninapo sema kukomaa yaani ile mkifungwa mnatoa hadi machozi kama brazil ilivyo fungwa na germany . Sasa utakuta timu imefungwa michezaji inacheka au inapongezana .

3. Wakicheza kama timu na kuacha show off .. watapiga senegal na kenya mabao mengi sana. Ila wasipo cheza kama timu taifa star ni mboga ya kila mtu.

4. Wakiacha ushamba na uzembe watafanya vizuri.

5. Waache kulaumiana.

Ni zamu yetu kubeba kombe.
Si bure umetumwa na Kanji wewe
 
Mbona Rahis sana..

Kenya tunawafunga point 3

Algeria tunawafunga point 3 jumla 6.

Senegal tuna drow au kufungwa.
Taifa stars ikichukua afcon,


Tundu lissu anakuwa raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania
 
Algeria hawa waliotupiga wiki.
Mimi sipingi kuchukua lakini staki kufa na pressure nimejipanga kukabiriana na matokeo yoyote.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom