Taifa limegawanyika kuhusu UKUTA

Taifa limegawanyika kuhusu UKUTA

Mkuu;
Tatizo ni kwamba risasi au bomu la machozi halina macho. Humpasukia mlengwa na asiye mlengwa. Hukumbuki yalotokea wakati Lipumba anatiwa nguvuni?? Mpaka watoto wachanga walilia. Hiyo tu ni laana
Labada kama wenzetu mtahama nchi, lakini ka mpo ,achozi hata weye yatakutoka tu.
Mkumbushe na ile risasi iliyomuua muuza magazeti Moro
 
Hili bandiko hasa maneno ya Viongoz kuelimisha wananchi yametulia sana! Good good good!! UKUTA NDIO HABARI YA MJINI
 
nilichoshangaa ni pale polisi wanafanya mazoezi hadharani kama wehu....nilitegemea watumie mbinu yoyote kutatua mgogoro....
sasa wanachofanya nimeani kuna ulazima sana wa kukagua vyeti kwa hawa wenzetu
Mimi magufuli nilimpuuza pale kwa mara ya kwanza alipokuwa akiongea na makamanda wa polisi Dodoma pamoja na siku ya kuwapandisha vyeo makamishina wa polisi. Hapo ndo nilipojua hana ethics za uongozi. maneno aliyotamka, siyo ya staha kwa kiongozi mkubwa akama yeye. kwa hiyo Magufuli mwenyewe tu ni tatizo.
 
Watangaze September 1 ni siku ya mapumziko ili tujumuike kwa wingi.

Mi naamini mapumziko yatakuwepo automatically.
Kama siyo baba Jesca kukurupuka na kutangaza hali ya hatari basi raia wenyewe watajiongoza kutulia majumbani wasifie mikononi mwa WAPUMBAVU.
 
Limegawanyika kwa watetezi wa mafisadi upande mwigine mtetezi wa wanyonge
 
Serikali imekuza mambo. Wangewapuuza chadema yasingefika huku yalipo.
Kikwete aliweza ila kwa John hapana.
Si Kikwete alikuwa "dhaifu?"
Sasa "dhaifu" amekuwa adimu.....
Na watu walipinga "udhaifu" ila bado wanataka kuishi kwa style ya "dhaifu".
Mantiki hii haiingii akilini hata kidogo.
 
Tumegawanyika. Wenye kujua democrasia na wasiojua maana ya democrasia pamoja na mashabiki wa ccm ambao wako pale kwa kulinda tumbo bila kufikiria taifa. Kuishi bila democrasia inafaidisha wachache wanaotawala. Lakini democrasia inafaidisha taifa zima. Hii ni Kwa sababu democrasia inaheshimu mawazo ya kila moja.
 
Tatizo JPM siyo born politician.....

Naamini hata wanaccm wenyewe hivi sasa watakuwa wanaregret sana chama Chao kuwa na Rais ambaye ameanza kuvurunda mapema mno Kabla hata hajafikisha angalau mwaka mmoja wa uongozi wake.

Magu atakuwa amegamble vibaya......

Aliamini kwa yeye pekee kufanya siasa nchi nzima na kuwatia 'kifungoni' vyama vya upinzani hadi mwaka 2020 atakuwa amejihakikishia popularity ya kukiwezesha chama chake kupata ushindi kilaini sana mwaka 2020.

Lakini kwa JPM kuitegemea 'mbeleko' ya Policcm kuwabeba imempunguzia popularity kwa kiwango kikubwa sana.

Naamini kama hivi leo itapigwa kura ya maoni kueleza ni wangapi wanaridhika na utawala wa JPM, inawezekana kabisa hivi sasa akakuta less than 40%wakawa ndiyo wanaomuunga mkono nchi nzima.

Kama kweli JPM hatataka umaarufu wake uendelee kutelemka kwa kasi ya kutisha inabidi abadilishe staili ya utawala wake, na zaidi sana aachane na speech za majukwaani za kutoa kichwani mwake, badala yake asome speech zinazoandaliwa na waandaaji wazoefu wa speech hapo Ikulu.

JPM anawapa shida sana anaofanya nao kazi.
Wanatakiwa kumuambia ukweli ila wanamuogopa.
Kama hawezi siasa akae chini atulie tu. Akubali kuelekezwa.
 
Haswaa kama J.P.M angekuwa mjanja angamaliza haya mambo mapema kwa mazungumzo.. sasa angalia now tension ilivokubwa kila mahali

Chadema wana mprovoke na yeye anajaa mazima.
Siamini kama kutakuwa na maandamano, ila serikali ipo kwenye tension ya kitu wasichokifahamu.
 
Katika Tanzania milioni 8 waliopigia UKAWA wanajua haki yao ya msingi. Lakini 6m waliopigia ccm hawajui haki zao kwani siyo wasomi na hawajui kama kweli ni wanachama.
 
1471894572354.jpg
 
Nilikuwa mapumzikoni kidogo kwa wiki moja, baada ya kazi nzito ya kusukuma gurudumu la maendeleo la Taifa hili la Tanzania.

Katika mapumziko yangu nimetumia muda kujaribu kufuatilia vuguvugu la UKUTA kwenye mitandao ya kijamii na mitaani pia, mwanzoni nilijua UKUTA haina wanachama na ilikuwa ni mbinu ya CHADEMA kuitisha serikali ili wafikie maridhiano, lakini cha kushangaza ni kuwa kuna watu wengi mno, hasa vijana wamehamasika, na kudai kuwa wanasubiria Sept 1 kwa hamu kubwa.

Nimeona jinsi mikakati mingi ya UKUTA ikiendelea kwa upande mmoja na upande mwingine polisi wakifanya mazoezi, ambayo mimi nimeyatafsri kuwa ni njia ya kutoa vitisho kwa wale wanaotaka kuandamana.

Nimeona jinsi kulivyo na tension kubwa katika mitandao ya kijamii kati ya makundi mawili, wanaounga mkono UKUTA na wasiounga, ambao wengi wao wameegemea upande wa serikali na chama tawala.

Nina wasiwasi Sept 1 inaweza kuwa ni siku ya madhara makubwa nchini kuwahi kutokea iwapo pande zote mbili hazitakaa na kufikia mwafaka. Nimepata hofu kuwa nchi inaweza kuingia kwenye vurumai, watu wakafa, tukawekewa vikwazo na kujikuta tunabeba hela kwenye kapu kwenda kununua mkate sokoni kama ilivyokuwa Zimbabwe. Kingine ni wahusika wa sakata kujikuta The Hague.

Habari za UKUTA na maandalizi ya polisi zinazidi kupaa katika anga za kimataifa.

Tensions rise ahead of Ukuta protests

Police ban on political rallies, demonstration lawful

Kwa wasiojua, vita kwenye nchi yoyote ile hasa za kiafrika, ina masilahi makubwa kwa mataifa makubwa hasa USA na Europe.


Mwenye masikio na asikie, naenda zangu.


Kutoka FACEBOOK Page ya Edward Ngoyai Lowassa:

"Leo nimezunguka katika majimbo ya Mbeya Vijijini ,Vwawa na Tunduma nikiwaeleza kuhusu Operation UKUTA,

UKUTA si fujo , UKUTA si machafuko na hatuna haja ya kufanya fujo , tunapiga kelele dhidi ya uvunjwaji wa haki ya kidemokrasia na katiba ya nchi unaofanywa na utawala huu wa awamu ya tano .

CHADEMA ni nani wakapambane na polisi ,polisi ambao ni watoto wetu ,ndugu zetu na hata wake na waume zetu ila tuwahakikishie hatutorudi nyuma pale katiba na haki ya kidemokrasia ikichezewa au kuwa chini ya mtu fulani . Najua polisi watapiga watu ,wataumiza watu na hata kuua ila niwahakikishie wao na walio na mamlaka wataishia katika mahakama ya Kimataifa .

Siasi ni mazungumzo ,lazima tuzungumze milango yetu iko wazi kufanya mazungumzo ila kwa kuwa hawahitaji na sisi hatutorudi nyuma September Mosi ,tumejiandaa vya kutosha na sasa tuko ngazi ya kaya na wajumbe wetu wanakamilisha kazi katika kaya ili tarehe mosi sauti ya kutosha ipazwe kwa maandamano na mikutano kama tulivyokubaliana katika kata zetu na majimbo nchi nzima . Haiwezekani hata kidogo mtu mmoja azuie kila kitu ,nchi hii ni mali yetu sote na inaongozwa na Katiba na sheria.

Kamati kuu ilipo amua katika suala la UKUTA haikukurupuka , kamati kuu yetu inaundwa na mchanganyiko wa wasomi wa kada mbalimbali ,wazee wenye busara na vijana machachari kamwe hawawezi kukukurupuka na UKUTA ni haki ya watanzania wote.

Pili naomba niwape siri ya ushindi 2020 ndugu zangu na wanachama wenzangu , tutashinda uchaguzi Mkuu 2020 kama tutafanya yafuatayo na kuyasimamia
Kwanza; Umoja ndani ya Chama na wanachama ,tuheshimiane ,tusameheane na tuimarishe chama chetu
"Chama ndani ya Chama , chama nje ya chama na chama ndani ya Umma ""

UKUTA mnaikuza tu kwenye MTANDAO wala haipo kiivo huku kwetu mambo wa sijawahiliskia hilo neno UKUTA zaidi ya huku , kwenye jf
 
Cuf wanajielewa hawataki kuburuzwa kama wanavyoburuzwa majizi Chadema na mbadilisha gia za angani mfalme Mbowe
 
Mkuu;
Tatizo ni kwamba risasi au bomu la machozi halina macho. Humpasukia mlengwa na asiye mlengwa. Hukumbuki yalotokea wakati Lipumba anatiwa nguvuni?? Mpaka watoto wachanga walilia. Hiyo tu ni laana
Labada kama wenzetu mtahama nchi, lakini ka mpo ,achozi hata weye yatakutoka tu.
Damu yako imejaa mabarafu! Kwa woga huo huponi utumwa
 
Back
Top Bottom