Tahrir Square ya Tanzania

Tahrir Square ya Tanzania

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
97,088
Reaction score
136,602
Kuna minong’ono nong’ono ishaanza kusikika toka kwa baadhi ya watu juu ya maandamano ya kupinga yaliyotokea kipindi cha chaguzi maalumu zilizomalizika wiki jana.

Niwajuavyo Watanzania, sidhani kama kutakuwepo na hayo maandamano. Wataishia kusema sema tu mitandaoni, basi. Mwishowe watasahau na wayalalamikiayo yatapita tu kama upepo.

Ila, tuseme na sisi tunakuwa na maandamano kama yale ya ‘Arab spring’, ni sehemu ipi hapa Dar ambapo panafaa kukusanyikia?

Mnazi Mmoja? Viwanja vya Leader’s? Kawe kule Tanganyika packers?
 
Hoja sio kuandamana, hoja ya msingi ni kwa nini waandamane. Je, sababu za maandamano ni tatizo linalogusa Watanzania wengi au ni frustration tu za baadhi ya watu wanaodhani malengo yao binafsi ya kisiasa na kijamii yamezibwa.

Naona yule dada yao wa Marekani bado anaendelea kuwashikia akiri makamanda.

Alianzisha zoezi la kuchoma kadi za CCM, sijui liliishia wapi?

Kwa sasa anakuja na utumbo wa kuandamana eti ili kuiondoa serikali madarakani! Huyu anadhani kuondoa serikali madarakani ni kama kuvunja ndoa wakati wowote au kutafuta penzi kwenye mitandao!

Unajua kuna baadhi ya watu wadanganywa sana na vikoment au vi-like vya kwenye mitandao mpaka wanadhani Tanzania ni mitandao ya Kijamii.

Wanadhani hata Ikungulyabashashi kwa kina Nyani Ngabu wanaishi kwenye mitandao ya Kijamii!

Hizi kelele baada ya siku tatu zitaisha halafu wataibuka na suala jingine.

Tanzania kuna vituko!
 
Back
Top Bottom