Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,923
- 6,538
Rais wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO), Geofrey Kiliba, amewakosoa vikali baadhi ya Watanzania wanaoikosoa na kuidharau elimu ya Tanzania, akisisitiza kuwa taifa lina kila sababu ya kujivunia maendeleo yaliyopatikana katika sekta hiyo, hasa chini ya serikali ya awamu ya sita.
Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 15 Mei 2025 jijini Dar es Salaam, Kiliba amepongeza serikali kwa hatua thabiti ilizochukua kuboresha elimu, ikiwa ni pamoja na kuimarisha miundombinu, kuongeza bajeti ya elimu, na kuwekeza katika maendeleo ya walimu na wanafunzi.
Ametoa kauli hiyo wakati akichambua bajeti ya Wizara ya Elimu kwa mwaka wa fedha 2025/2026 , akieleza kuwa bajeti hiyo inaonyesha mwelekeo chanya wa mageuzi katika sekta hiyo muhimu kwa maendeleo ya taifa.
Kiliba pia amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali, sekta binafsi, na wadau wengine wa elimu katika kuhakikisha ubora na usawa wa elimu kwa Watanzania wote.
Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 15 Mei 2025 jijini Dar es Salaam, Kiliba amepongeza serikali kwa hatua thabiti ilizochukua kuboresha elimu, ikiwa ni pamoja na kuimarisha miundombinu, kuongeza bajeti ya elimu, na kuwekeza katika maendeleo ya walimu na wanafunzi.
Ametoa kauli hiyo wakati akichambua bajeti ya Wizara ya Elimu kwa mwaka wa fedha 2025/2026 , akieleza kuwa bajeti hiyo inaonyesha mwelekeo chanya wa mageuzi katika sekta hiyo muhimu kwa maendeleo ya taifa.
Kiliba pia amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali, sekta binafsi, na wadau wengine wa elimu katika kuhakikisha ubora na usawa wa elimu kwa Watanzania wote.