Tahadharini LG Tv Workshop usithubutu

Tahadharini LG Tv Workshop usithubutu

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
23,251
Reaction score
28,406
Nimepeleka LG Tv yangu kwenye karakana ya duka la vifaa vya LG iliyopo mtaa wa Nkurumah Dar es Salaam, ili ipokelewe nimelipa Sh. 30,000/=. Baada ya muda wakanipigia simu gharama za matengenezo Sh 250,000/= na zile 30,000/= inakuwa shs 280,000/= nusu ya bei ya Tv yenyewe Sh. 600,000/=.

Nimeamua kuichukua na wao wanachukua Sh.30,000/= bila jasho na mtu mwingine akienda watambamiza na bei kubwa ashindwe wapate 30,000/= za bure na huenda hawana spea au wameshindwa lakini pesa inaingia bila jasho.

Nimemkumbuka aliyewahi kuulizia karakana hii ya LG.
 
Wakala wa LG tz ni METL ila sioni akifanya la Maana sana sana Vifaa vyote vya LG vina nembo ya KEBS
 
Kuna wakati picha inapotea inabaki ikionekana kwambali lakini sauti inatoka, ikifurahi picha inarudi.
Tatizo lake kubwa ni main card/card inayobeba video chips ina overheat, na kwa tv za flat zikianza hivyo basi ni kubadilisha tu hiyo card, kama uwezo wako ni mdogo basi unafunga zile za universal tu.
Universal tv card unapata kwa 45 - 80 inategemea na model yake then fundi wa kukufungia mnapatana tu malipo ya kazi.
 
Tuliwahi kudiscuss humu jukwaani kwamba karakana ya LG ipo Nairobi tu kwa East Africa?

Una uhakika hao jamaa ni official? Na sio wajanja tu wa mjini wanaojiita LG?
Niwajanja tu, unawapa 30,000/= wanakupa bei mkubwa unashindwa unaichukua wao wanabaki na 30,000/= bila jasho na huenda hata hawakuifungua, ni ujanja wa mjini kama uwajuavyo wahindi.
 
Back
Top Bottom