Tahadhari za matumizi ya jiko la mkaa

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Jan 29, 2021
573
2,553
Haushauriwi kujifungia chumbani ukiwa unalala au wakati wa kupika chakula wakati unatumia jiko la mkaa.

BDB45EAA-32CF-4752-A9A9-E21B52448123.jpeg

Aina hii ya jiko huzalisha gesi yenye sumu inayoitwa Carbon monoxide (CO) ambayo huufanya mwili usipate kiasi cha kutosha cha hewa safi ya Oxygen inayohitajika kwenye upumuaji.

Ikiwa changamoto hii itatokea, mhusika anaweza kupatwa na maumivu makali ya kichwa, kizunguzungu, uchovu mkubwa, kuongezeka kwa mapigo ya moyo, kukata kwa pumzi na hatimaye kupoteza fahamu.

Sumu ya carbon monoxide (CO) inaweza pia kusababisha uharibifu wa kudumu kwenye seli muhimu za ubongo pamoja na kusababisha kifo ikiwa msaada wa haraka hautatolewa.

Kwa watu wanaotumia aina hii ya jiko kwenye kupika chakula wanapaswa kufungua madirisha ya nyumba pamoja na kuruhusu upatikanaji wa hewa ya kutosha. Aidha, kwa wale wanaolala na jiko la mkaa wakati wa baridi kali wanashauriwa kuacha tabia hii inayoweza kugharimu maisha yao.

Chanzo: Mayo Clinic
 
Haushauriwi kujifungia chumbani ukiwa unalala au wakati wa kupika chakula wakati unatumia jiko la mkaa.


Aina hii ya jiko huzalisha gesi yenye sumu inayoitwa Carbon monoxide (CO) ambayo huufanya mwili usipate kiasi cha kutosha cha hewa safi ya Oxygen inayohitajika kwenye upumuaji.

Ikiwa changamoto hii itatokea, mhusika anaweza kupatwa na maumivu makali ya kichwa, kizunguzungu, uchovu mkubwa, kuongezeka kwa mapigo ya moyo, kukata kwa pumzi na hatimaye kupoteza fahamu.

Sumu ya carbon monoxide (CO) inaweza pia kusababisha uharibifu wa kudumu kwenye seli muhimu za ubongo pamoja na kusababisha kifo ikiwa msaada wa haraka hautatolewa.

Kwa watu wanaotumia aina hii ya jiko kwenye kupika chakula wanapaswa kufungua madirisha ya nyumba pamoja na kuruhusu upatikanaji wa hewa ya kutosha. Aidha, kwa wale wanaolala na jiko la mkaa wakati wa baridi kali wanashauriwa kuacha tabia hii inayoweza kugharimu maisha yao.

Chanzo: Mayo Clinic
REWO NDO UMEYAJUA!!! KWANI HAYO MAJIKO/kuni YAMETULEA/KUZA MIAKA NA MIAKA VIZAZI NA VIZAZI LEO YAMEKUWA HAYOOOO! mtatwambia sasa na ugali pia una sumu tule mchele wa China!

Mmmeona Gas haipendwi sasa mmekuja na haya! mistumiwe saaana na wazungu/waarabu km majuha!
 
Km mkaa unatoa gas ya carbon dioxide basi ni Mali nzuri sana make tunagema hiyo tuiweke kwenye mitungi tuka uze ulaya tupate hela!! hamtaki!
 
Back
Top Bottom