Watoto wawili wafariki kwa kulala na jiko la mkaa linalowaka

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,194
4,115
Watoto wawili ambao wanafahamika kwa majina Evance Kapinga (3) na Tabia Ngombele (17) wamefariki dunia baada ya kuacha jiko la mkaa likiwa linawaka ndani wakiwa wamelala nyakati za usiku.

Mwenyekiti wa mtaa wa Frelimo Bw. Jalala Mwinyimbegu amerhibitisha kutokea kwa tukio hilo akisema watoto hao waliachwa peke yao na mzazi waliyekuwa wanaishi naye ambaye alikuwa safarini na aliporejea usiku na kugonga hodi bila mafanikio akawaita majirani waliovunja mlango na kukuta watoto tayari wamefariki.

EATV imezungumza na jirani wa familia hiyo Ibrahim Kitang’ala, ambaye anaiashi katika nyumba waliyokuwa wakiishi watoto hao na mzazi wao na amesema baada ya kuvunja mlango walikuta watoto hao wamefariki huku mtoto mmoja aliyefahamika kwa jina Moline Mligo (7) akiwa amenusurika.

“Tulipovunja mlango tulimkuta mama mdogo wa watoto hao akiwa jirani na mlango kwahiyo tunadhani wakati anasonga ugali alipoona hali inakuwa mbaya alitaka kufungua mlango na yeye akaishiwa nguvu” amesema Ibrahim Kitang’ala, jirani.
 
Ubaya wa hili janga linachukuliwa kwa uwepesi. Natamani hata wasanifu majengo wangebuni njia nyepesi na affordable ya kuongeza joto kwenye majumba hasa kwa sehemu zenye baridi kama iringa na njombe, ambapo vifo hivi vipo common.
 
☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️☹️

R.i.p
 
Watoto wawili ambao wanafahamika kwa majina Evance Kapinga (3) na Tabia Ngombele (17) wamefariki dunia baada ya kuacha jiko la mkaa likiwa linawaka ndani wakiwa wamelala nyakati za usiku.

Mwenyekiti wa mtaa wa Frelimo Bw. Jalala Mwinyimbegu amerhibitisha kutokea kwa tukio hilo akisema watoto hao waliachwa peke yao na mzazi waliyekuwa wanaishi naye ambaye alikuwa safarini na aliporejea usiku na kugonga hodi bila mafanikio akawaita majirani waliovunja mlango na kukuta watoto tayari wamefariki.

EATV imezungumza na jirani wa familia hiyo Ibrahim Kitang’ala, ambaye anaiashi katika nyumba waliyokuwa wakiishi watoto hao na mzazi wao na amesema baada ya kuvunja mlango walikuta watoto hao wamefariki huku mtoto mmoja aliyefahamika kwa jina Moline Mligo (7) akiwa amenusurika.

“Tulipovunja mlango tulimkuta mama mdogo wa watoto hao akiwa jirani na mlango kwahiyo tunadhani wakati anasonga ugali alipoona hali inakuwa mbaya alitaka kufungua mlango na yeye akaishiwa nguvu” amesema Ibrahim Kitang’ala, jirani.
Ooh sad

Hii ajali imetokea wapi? Au nchi jirani ya Kenya?
 
Natamani kujua kama una bei rafiki kutokana na hali za watu wa maeneo hayo.

Sifanyi hiyo kazi, lakini nimeona Mafinga nyumba ina hiyo heating system...

Pia hata nikiwa China, nyumba nyingi zina namna hiyo ya heating system...
 
Back
Top Bottom