Tahadhari; Madalali wengi wanatumia uchawi

Tahadhari; Madalali wengi wanatumia uchawi

kzba

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2014
Posts
1,355
Reaction score
790
Wanajf wenzangu,

Kuweni makini sana pale mnapotaka kufanya maamuzi ya kutaka kupanga au kununua kitu.Wengi wa madalali hasa hapa bongo wanatumia nguvu za giza kuwalaghai watu katika kufanikisha azma yao ya either kupangisha au kumuuzia mtu kitu.

Mfano labda unataka kununua nyumba au kiwanja,dalali atakupeleka kwenye nyumba au viwanja mbalimbali labda wewe hujaridhika navyo yeye anachokifanya anakupumbaza unajikuta unanunua bila hata kujitambua ili mradi yeye chake cha udalali akipate.

Nina ushuhuda wa hili yamemkuta rafiki yangu kauziwa nyumba hata yeye mwenyewe binafsi anashangaa ilikuwaje akakubali kununua sehemu hatarishi kama hiyo.

Nilipokuja kuhoji baadhi ya madalali wakakiri kabisa kuwa uchawi ndio mtindo wao wa maisha ili kufanikisha mipango yao hasa kwa wateja wao wasumbufu.

Think twice before hujafanya maamuzi ya kufanya biashara na madalali.

Nawasilisha
 
si kweli, hayo ni mawazo tu yakishirikina yaliyotawala kwenye akili yako. hakuna uchawi, kweli mtu kukushawishi ndo ametumia uchawi?
 
Hujui tofauti ya kulogwa na kudanganywa wewe.sifa ya mdalali ni kudanganya hayo ya kulogwa ni yako na akili yako nyepesi
 
Dalali amekuzidi maarifa mkuu pole si uchawi wala nini!
 
Hujui tofauti ya kulogwa na kudanganywa wewe.sifa ya mdalali ni kudanganya hayo ya kulogwa ni yako na akili yako nyepesi

mbona mnamshambulia sana mtoa mada!wakati hiyo yeye ameyashuhudia"!kubwa hapa kuamini,kama unaamini uchawi upo hilo linawezekana
 
madalali bila ubishi hutumia njia ya maneno mengi na kukunganizia jambo kimazingara! but sio wote ni baadhi tu!
 
sasa nyie mnabisha nini wakati madalali wenyewe ndo wamesema! mijitu mingine bana!
 
Ishu ya uchawi ni kweli kabisa yamenikuta hata mimi kuna kipande cha ardhi nilikuwa nakiuza kilikuwa ni kizuri tu lakini wanunuzi walikuwa hamna nikamtafuta dalali mmoja maarufu sana maeneo ya Segerea kuja kukiona tu kiwanja chenyewe akaniambia hapo pana kitu kimewekwa ili kisiuzike maana majirani walikuwa wameweka kamba zao za kuanikia nguo na wengine wamelima mbogamboga akafanya mambo yake anayoyajua mwenyewe kesho yake ananipigia simu kuwa mteja kashapatikana nije na hati tuandikishane nichukue changu
 
Kama ni kweli umejiridhisha na upembuzi juu ya hao madalali ni vyema,Ila kumbuka kuwa nao ndo Maisha yao kwa hiyo kutowatumia kuna ugumu kidogo hususani pale unapokuwa ni mgeni na yale mazingira.Cha msingi ni kuwa makini kuwa soma wao kabla hawajakusoma na shida yako
 
Wana jf wenzangu..,kuweni makini sana pale mnapotaka kufanya maamuzi ya kutaka kupanga au kununua kitu
Wengi wa madalali hasa hapa bongo wanatumia nguvu za giza kuwalaghai watu katika kufanikisha azma yao ya either kupangisha au kumuuzia mtu kitu, mfano labda unataka kununua nyumba au kiwanja...,dalali atakupeleka kwenye nyumba au viwanja mbalimbali labda wewe hujaridhika navyo yeye anachokifanya anakupumbaza unajikuta unanunua bila hata kujitambua ili mradi yeye chake cha udalali akipate,
Nina ushuhuda wa hili yamemkuta rafiki yangu kauziwa nyumba hata yeye mwenyewe binafsi anashangaa ilikuwaje akakubali kununua sehem hatarishi kama hyo
Nilipokuja kuhoji baadhi ya madalali wakakiri kabisa kuwa uchawi ndo mtindo wao wa maisha ili kufanikisha mipango yao hasa kwa wateja wao wasumbufu

Think twice before hujafanya maamuzi ya kufanya biashara na madalali

Nawasilisha

akili ndogp hizi!!
 
Ishu ya uchawi ni kweli kabisa yamenikuta hata mimi kuna kipande cha ardhi nilikuwa nakiuza kilikuwa ni kizuri tu lakini wanunuzi walikuwa hamna nikamtafuta dalali mmoja maarufu sana maeneo ya Segerea kuja kukiona tu kiwanja chenyewe akaniambia hapo pana kitu kimewekwa ili kisiuzike maana majirani walikuwa wameweka kamba zao za kuanikia nguo na wengine wamelima mbogamboga akafanya mambo yake anayoyajua mwenyewe kesho yake ananipigia simu kuwa mteja kashapatikana nije na hati tuandikishane nichukue changu
bojo! nini?
 
Hiyo Ni Lugha Ya Biashara ;Sio Uchawi
Angekuwa Mchawi Angekupumbaza Akuuzie Ufukwa Wa Bahar Kabisa
Jigo
 
Hakuna kitu kama hicho,mara nyingi watu ambao hawajazoea kushika hela wakipata uwa na mawenge hivi.
 
Hawa jamaa (madalali) kunakitu wanaita hypnotize attack ukiingia kwenye 18zao umeisha!
 
Kutojiamini ni ugonjwa wa watanzania wengi..yaani dalali akuloge ununue kitu usichokitaka? Siamini hayo mambo
 
Naweza kuamini! kuna madalali wanauza kiwanja kimoja hata kwa watu 10, huwa najiuliza inakuaje rahisi hivo!
Afu kuna yale maeneo dalali anauza mpk mnunuzi mwenyewe haamini alinunuaje!
 
Ni kweli mimi nina rafiki yangu dadali arienda mbaka sumbawanga kwa mganga ili kazi yake iwe safi
 
Hizo ni mbinu za biashara tu hata maduka mengine ukiingia unauliza shati akikupa bei kama hujaridhika unaondoka na muuzaji hakusemeshi, lakini unaingia duka lingine anahakikisha hutoki bila kununua maana atakupiga lugha hiyo mpaka unanunua, hizo ni lugha za biashara wala sio uchawi. Kama napata watu wa hivyo huwa siwaachi nawapa kazi fasta na mshahara mnono
 
Back
Top Bottom