The Assassin
JF-Expert Member
- Oct 30, 2018
- 5,082
- 20,798
Mi hatari sana aisee. Usifanye masihalaYeah ukiwa ndani kule lazima utahamaki na kama hujazoea yaani ndio utahisi unakufa kule.
Mi hatari sana aisee. Usifanye masihalaYeah ukiwa ndani kule lazima utahamaki na kama hujazoea yaani ndio utahisi unakufa kule.
Saa kama tatu hivi zilizopita nilikua Kariakoo kwenye jengo moja la ghorofa saba ambalo hutumika kama makazi ya watu na ofisi pia. Ofisi niliyokua naenda ipo ghorofa hiyo ya saba ambapo ilinilazimu nipande lift
Nilipobonyeza kitufe cha namba ya floor ninayoenda akawa amekuja dada ambaye kwa mavazi yake nikahisi alikua ametoka au anakwenda kwenye mazoezi (nadhani kwenye jengo lile ipo gym) hivyo ikanilazimu nibonyeze kitufe cha kumsubiria akapanda tukaondoka
Sekunde chache tu baada ya kuondoka tukiwa tunapita floor ya tatu taa zikazimika ndani ya ile lift, ikatoa mlio kama imegonga kitu halafu ikawa kama inarudi chini kisha ikasimama kabisaa! Yule dada akapiga yowe la ku panik. Nilipomwambia asiwe na wasiwasi tutatoka akanisogelea na kunikumbatia huku anaendelea kupiga kelele
Changamoto kubwa ni ile milango ya lift yenyewe ilivyokua mizito mpaka unahisi kabisa hata hizo kelele hazifiki popote. Nilinyoosha mkono na kubonyeza kitufe cha emergency bila kuondoa mkono(continuously) lakini hatukuweza kupata msaada kwa haraka
Hali ilikua ya taharuki kubwa maana kile kichumba cha lift ni kdogo, milango ni minene sana na joto lilikua linaongezeka. Tulikaa mle kama dakika saba au nane ambazo zilikua kama mwaka ndipo zikasikika sauti za watu kwa nje wakiwa wanashughulika kutufungulia mlango na muda walipofanikiwa kutufungulia yule dada niliyekua nae alikua amelala chini kwenye sakafu ya lift na akawa kama anaeelekea kupoteza fahamu!!!
Namshukuru Mungu tulitoka salama ingawa yule dada ilibidi apelekwe hospitali kwa hali aliyokua nayo maana hata mambo yake mengine ya kiuanamke (tafsida imezingatiwa) yalimuharibikia na ukizingatia mavazi aliyokua amevaa hakutarajia pengine mambo yamtokee wakati huo!
Wito wangu kwa watengeneza elevators, watengeneze lifts za milango transparent ili mtu aweze kuona nje angalau pressure inapungua kuliko hizi lift zenye milango utadhani gereza au kaburi aisee! Mtu unapokua unawaona watu nje unajua muda wowote unatoka. Amakweli kifo kwa binadamu ni sekunde tu!
Mimi pia ni mhanga, jengo la Mega complex Arusha, floor ya tano Kenyatta University.Ilinitokea jengo la Treasurer Dodoma. Tulikaa kama Dakika tatu, umeme ukarudi. Ndani ya lift tulikuwa wawili tu, Mimi na Mdada mmoja ndugu yangu, sikujua cha kufanya ikabidi niwe namtuliza tu kuwa asiwe na waswas watafungua soon maana shida wanaijua.
From that day, lift huwa nazikwepa sana.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hata pale Shoppers Plaza ya Mikocheni ipo ya vioo japo vigorofa vyao ni viwili. Nyingine ipo jengo la NSSF WaterfrontHata bongo zipo za vioo ni nzuri sana kwajili ya usalama
Asante nimeshapoa kiongozi
Naunga mkono hoja.Saa kama tatu hivi zilizopita nilikua Kariakoo kwenye jengo moja la ghorofa saba ambalo hutumika kama makazi ya watu na ofisi pia. Ofisi niliyokua naenda ipo ghorofa hiyo ya saba ambapo ilinilazimu nipande lift
Nilipobonyeza kitufe cha namba ya floor ninayoenda akawa amekuja dada ambaye kwa mavazi yake nikahisi alikua ametoka au anakwenda kwenye mazoezi (nadhani kwenye jengo lile ipo gym) hivyo ikanilazimu nibonyeze kitufe cha kumsubiria akapanda tukaondoka
Sekunde chache tu baada ya kuondoka tukiwa tunapita floor ya tatu taa zikazimika ndani ya ile lift, ikatoa mlio kama imegonga kitu halafu ikawa kama inarudi chini kisha ikasimama kabisaa! Yule dada akapiga yowe la ku panik. Nilipomwambia asiwe na wasiwasi tutatoka akanisogelea na kunikumbatia huku anaendelea kupiga kelele
Changamoto kubwa ni ile milango ya lift yenyewe ilivyokua mizito mpaka unahisi kabisa hata hizo kelele hazifiki popote. Nilinyoosha mkono na kubonyeza kitufe cha emergency bila kuondoa mkono(continuously) lakini hatukuweza kupata msaada kwa haraka
Hali ilikua ya taharuki kubwa maana kile kichumba cha lift ni kdogo, milango ni minene sana na joto lilikua linaongezeka. Tulikaa mle kama dakika saba au nane ambazo zilikua kama mwaka ndipo zikasikika sauti za watu kwa nje wakiwa wanashughulika kutufungulia mlango na muda walipofanikiwa kutufungulia yule dada niliyekua nae alikua amelala chini kwenye sakafu ya lift na akawa kama anaeelekea kupoteza fahamu!!!
Namshukuru Mungu tulitoka salama ingawa yule dada ilibidi apelekwe hospitali kwa hali aliyokua nayo maana hata mambo yake mengine ya kiuanamke (tafsida imezingatiwa) yalimuharibikia na ukizingatia mavazi aliyokua amevaa hakutarajia pengine mambo yamtokee wakati huo!
Wito wangu kwa watengeneza elevators, watengeneze lifts za milango transparent ili mtu aweze kuona nje angalau pressure inapungua kuliko hizi lift zenye milango utadhani gereza au kaburi aisee! Mtu unapokua unawaona watu nje unajua muda wowote unatoka. Amakweli kifo kwa binadamu ni sekunde tu!
Ndio hapo unajua roho ya binadamu kutoka ni kitu cha sekunde tu mkuuNi ombea mtu tu akusimulie.
Ukiingia kwenye lift za huko lazima uombe sala ya mwishoMimi pia ni mhanga, jengo la Mega complex Arusha, floor ya tano Kenyatta University.
Tulikuwa watatu vidume wote, jamaa yangu akaanza kulipiga ngumi, mlango mgumu balaa, Dakika kama Tano, Jenereta likawashwa hapo tushaanza onja joto ya jiwe kijasho.
Ni ombea mtu tu akusimulie.
Sent using Jamii Forums mobile app
Unapanda na ngazi hata kama ni ghorofa kumi mkuu!? Au utaanza kutumia lift watakapo badilisha technology?Dah unakufa huku unaona an pole mkuu sema mm na lift wala nshazoea zangu kupanda ngaz na miguu yangu
Sent using Jamii Forums mobile app
Halafu sehemu nyingine lift zinajaa balaa! Kama lile jengo la RITA pale karibu na Bilicanas. Unaomba Mungu lisitokee jambo baya maana inabidi hiyo rescue action isichelewe hata kwa dakika moja amasivyo itakua balaa kwa watu wanavyojazanaLift za vioo labda majengo mapya na kwenye malls.
Kuna siku nimeenda ubungo plaza kuingia kwenye lift nikawa nasali isizime maana hapo tu lift haina hata ac unawaza ikizima si ndo mnakufa humo humo
Sisi mwanzo tulipanic sana ila tukasema tupige zile namba za dharura, zote hata haziiti hata, tukaanza kutaniana tunakufa wote taratibu kwa kukosa hewa, tunacheka lakini ukipima mapigo ya moyo kila mmoja ana wasiwasi balaa.Ndio hapo unajua roho ya binadamu kutoka ni kitu cha sekunde tu mkuu
Vijiwe vya mjini huviwezi kwa kuchomekea.SUMATRA WANAHUSIKAJE NA ELEVATORS MKUU?
Yani hapo wenyewe tulikua kibao. Hewa hamna na lift haina ac. Nilivyokua nashuka nikapanda za upande mwingine ndio ziko automated kidogoHalafu sehemu nyingine lift zinajaa balaa! Kama lile jengo la RITA pale karibu na Bilicanas. Unaomba Mungu lisitokee jambo baya maana inabidi hiyo rescue action isichelewe hata kwa dakika moja amasivyo itakua balaa kwa watu wanavyojazana
kajamaa kadogo wakati maisha yako yapo hatarini hakuna kingine kitakachoingia akilini mwako na kwenye hisia zako zaidi ya kuomba uokolewe/uokoke na janga hilo tu. Tena utaweka ahadi za kila aina kwa Mungu wako kua ukitoka salama utaacha dhambi zote 😀😀😀penda sana kuwaza nje ya "box"
Mimi nina wasiwasi kama Anaomba ushauri Angemuomba PAPUCHI "she"
Nawaza kwa sauti tu
Huo wasiwasi ulonao siku Mimi imenipata kama ungekuwepo nadhani ungetabasamu tu kwa kuwa tulianza kutaniana japo hewa hamna.Lift za vioo labda majengo mapya na kwenye malls.
Kuna siku nimeenda ubungo plaza kuingia kwenye lift nikawa nasali isizime maana hapo tu lift haina hata ac unawaza ikizima si ndo mnakufa humo humo