Tahadhari kwa walaji wa Pweza

Tahadhari kwa walaji wa Pweza

Jamani mada mbona imehama? Hivi mnajua wanakoandaliwa hawa samaki hadi wakufikie hapo njiani? Tunalishwa maradhi wandugu
 
Nna asili na kiumbe huyu....najua "kumchokoa",kumtayarisha na kumla.....sijawahi kusikia kuwa pweza akiwekwa kwenye friza anakuwa laini.Ninachojua wavuvi huwa baharini siku 4 hadi 5 kwa wiki,sasa huyo atavuliwa atapigwa kwenye chombo na kusafishwa na kuwekwa kwenye barafu,wewe ukiona wanarudi na kumuuza unajua hajapigwa...no...waulize watu wa pwani watakwambia.Huyubila kumpiga utatafuna Big G mpaka ukome....hanogi ng'o!

Huwa sinunui pweza wa Barafu nanunua fresh na najua yupi fresh na yupi sio fresh na nafahamu hata aina ya pweza na mwambao aliovuliwa!!..pale feri huwa wanakuja wa leo leo na nawajua vizuri na ndio maana huwa sihangaiki sana kuwapiga nabeba naenda kuwaosha vizuri nawaweka kwenye friza then baada ya siku mbili unakata tuu vipande. Kumbuka mimi sio mwenyeji tu wa maeneo yenye pweza wengi ila pia mimi ni mvuvi mstaafu wa pweza!..inaonekana wewe una idea kubwa na pweza ila hapa kwangu unaweza jifunza kitu kuhusu pweza usinibeze fanya hivyo nilivyokuambia lazima unikubali!
 
Huwa sinunui pweza wa Barafu nanunua fresh na najua yupi fresh na yupi sio fresh na nafahamu hata aina ya pweza na mwambao aliovuliwa!!..pale feri huwa wanakuja wa leo leo na nawajua vizuri na ndio maana huwa sihangaiki sana kuwapiga nabeba naenda kuwaosha vizuri nawaweka kwenye friza then baada ya siku mbili unakata tuu vipande. Kumbuka mimi sio mwenyeji tu wa maeneo yenye pweza wengi ila pia mimi ni mvuvi mstaafu wa pweza!..inaonekana wewe una idea kubwa na pweza ila hapa kwangu unaweza jifunza kitu kuhusu pweza usinibeze fanya hivyo nilivyokuambia lazima unikubali!

Ha ha ha.....ntafanyia kazi hili.....hapana mimi si tu kuwa nna idea....ni mvuvi pia...lkn km wasemavyo bahari pana kuna la huku halijulikani kule,thanks!
 
Kula vzr fanya mapenz kwa afya(mara mbili kwa wiki),fanya mazoez ya kutosha uone kama utapungukiwa nguvu ....kula pweza kwa hamu na kwa afya otherwise hvyo vpande vya mitaan na supu za mitaan ni maradh tu nothing else
 
mnyama mzuri hasa ukiandaa mwenyewe nyumbani.

Asante kwa kumaliza ugomvi.

CLOSED.png
 
mfafanulie vizuri kuhusu aliyepigwa, sio kupikwa
Mkuu moja ya matayarisho ya pweza ni kumchezesha judo,kumpa kichapo kikali akiwa amekufa la sivyo haliki atagangamaa na akipikwa itakuwa afadhali utafune soli ya kiatu chako badala ya pweza!
 
Nna asili na kiumbe huyu....najua "kumchokoa",kumtayarisha na kumla.....sijawahi kusikia kuwa pweza akiwekwa kwenye friza anakuwa laini.Ninachojua wavuvi huwa baharini siku 4 hadi 5 kwa wiki,sasa huyo atavuliwa atapigwa kwenye chombo na kusafishwa na kuwekwa kwenye barafu,wewe ukiona wanarudi na kumuuza unajua hajapigwa...no...waulize watu wa pwani watakwambia.Huyubila kumpiga utatafuna Big G mpaka ukome....hanogi ng'o!

Uko sawA mkuu mi nakumbuka kipindi niko mtwara nilikua nikimtengeza pweza wakati namchemsha nilikua naweka ma sukari kidogo sana ili alainike.
 
Pweza wa vipande barabarani hana faida yoyote zaidi ya kukuletea maradhi.....hakuna nguvu yoyote utakayoipata hapo.Unataka msaada wa mawazo,nenda feri nunua pweza wako 1kg ni km buku 4-5 hivi.....fika nae nyumbani muoshe vizuri kwanza kwa maji ya kawaida,pili maji ya moto huwa anakuwa na michanga sana mikiani.weka jikoni usiweke maji kwanza mpaka akaushe maji yake mwenyewe,kisha weka maji kwa supu yako,tupia kitunguu kiasi kuongeza hamu na km una kitunguu saum kiasi ni bora chemsha km dk30.Hii ni zaidi ya "mkuyati" hutotumia Viagra tena!

Aisee!!!!Noted with thanks
 
Mkuu moja ya matayarisho ya pweza ni kumchezesha judo,kumpa kichapo kikali akiwa amekufa la sivyo haliki atagangamaa na akipikwa itakuwa afadhali utafune soli ya kiatu chako badala ya pweza!
hahahaaa... Duh! Watu wavumbuzi kweli. Aliyevumbua hiyo staili ya kupiga sijui alikuwa anawaza nini
 
Ukimuona Pweza akiwa hai sijui hata kama utatamani kumla, kumbe Pweza anaongeza nguvu za kiume? Hii ni kweli au Iman tu?
 
Pweza wanasifika kwa kuongeza nguvu za kiume, lakini kwa upikaji huu ninaouona ni wazi kuwa nguvu zetu ziko mashakani. Wakati wa kuwaandaa, vijana hawa huwafunika kwa nailoni wakiwa jikoni hadi waive. Kuna usalama hapo? Kazi kwenu walaji wa pweza mnaosaka nguvu za ziada
Wakifunikwa kwa nailoni ndo saafi, ndulele husimama kama nguzo ya Tanesco siku mbili mfululizo!
 
Pweza wanasifika kwa kuongeza nguvu za kiume, lakini kwa upikaji huu ninaouona ni wazi kuwa nguvu zetu ziko mashakani. Wakati wa kuwaandaa, vijana hawa huwafunika kwa nailoni wakiwa jikoni hadi waive. Kuna usalama hapo? Kazi kwenu walaji wa pweza mnaosaka nguvu za ziada

Shida si wakati wa kuwapika tabu ni wakati wa kuserv maana hapo ndo mnapishana na nzi,, ila kama wako jikoni hata kama wako wazi si shida maana hilo joto lake hakuna bacteria ata suvive
 
mimi ni mlaji mzuri wa pweza kila jioni, ila si kweli kuwa wanaongeza nguvu, uwezo wa uwanja wa seremala ni saikolojia yako, mfumo wa vyakula, mazoezi. ila hizo theory zingine za pweza, nyagi, zanzi mhhhhh. imani.
 
akina dada wakishaona mume au boyfriend wake yuko busy na pweza, wanahaha mno, sijui wanaogopa gwaride
 
Pweza wa vipande barabarani hana faida yoyote zaidi ya kukuletea maradhi.....hakuna nguvu yoyote utakayoipata hapo.Unataka msaada wa mawazo,nenda feri nunua pweza wako 1kg ni km buku 4-5 hivi.....fika nae nyumbani muoshe vizuri kwanza kwa maji ya kawaida,pili maji ya moto huwa anakuwa na michanga sana mikiani.weka jikoni usiweke maji kwanza mpaka akaushe maji yake mwenyewe,kisha weka maji kwa supu yako,tupia kitunguu kiasi kuongeza hamu na km una kitunguu saum kiasi ni bora chemsha km dk30.Hii ni zaidi ya "mkuyati" hutotumia Viagra tena!

Duuuuh Kwel noma
 
Back
Top Bottom