Tahadhari kwa walaji wa Pweza

Tahadhari kwa walaji wa Pweza

Nchi Kavu

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2010
Posts
4,289
Reaction score
2,472
Pweza wanasifika kwa kuongeza nguvu za kiume, lakini kwa upikaji huu ninaouona ni wazi kuwa nguvu zetu ziko mashakani. Wakati wa kuwaandaa, vijana hawa huwafunika kwa nailoni wakiwa jikoni hadi waive. Kuna usalama hapo? Kazi kwenu walaji wa pweza mnaosaka nguvu za ziada
 
Ngoja waje watetezi wa marijali bandia hapa uone povu la kutosha!!hili jambo la nguvu za kiume kila kukicha ni mtihani,tatizo ni ulaji wa ovyo na kila mtu sasa hivi amekuwa doctor wa nguvu za kiume.Hebu wenye hii taaluma tunaomba mtoe darasa la kutosha.
 
Nackia na mwanza wameanza kuletwa hao pweza hebu nielekezeni maandalizi yake ili nijenge heshima
 
Ngoja waje watetezi wa marijali bandia hapa uone povu la kutosha!!hili jambo la nguvu za kiume kila kukicha ni mtihani,tatizo ni ulaji wa ovyo na kila mtu sasa hivi amekuwa doctor wa nguvu za kiume.Hebu wenye hii taaluma tunaomba mtoe darasa la kutosha.


Huo ni mfadhaiko wa Akili na Mawazo kamuone Daktari
 
Pweza wa vipande barabarani hana faida yoyote zaidi ya kukuletea maradhi.....hakuna nguvu yoyote utakayoipata hapo.Unataka msaada wa mawazo,nenda feri nunua pweza wako 1kg ni km buku 4-5 hivi.....fika nae nyumbani muoshe vizuri kwanza kwa maji ya kawaida,pili maji ya moto huwa anakuwa na michanga sana mikiani.weka jikoni usiweke maji kwanza mpaka akaushe maji yake mwenyewe,kisha weka maji kwa supu yako,tupia kitunguu kiasi kuongeza hamu na km una kitunguu saum kiasi ni bora chemsha km dk30.Hii ni zaidi ya "mkuyati" hutotumia Viagra tena!
 
Scrony bora umetoa somo. Hawa wa njiani ni majanga tupu. Supu yenyewe imejaa particles za nailoni
 
Kwenye freezer anakaa muda gani akiwa mbichi bila kuharibika s.crony
 
Last edited by a moderator:
Yaani huyu mdudu nisipopata ujue siku haijaisha.
Ila siyo kwa ajili ya nguvu za kiumee, aaaah mi napenda tu.
 
Pweza wanasifika kwa kuongeza nguvu za kiume, lakini kwa upikaji huu ninaouona ni wazi kuwa nguvu zetu ziko mashakani. Wakati wa kuwaandaa, vijana hawa huwafunika kwa nailoni wakiwa jikoni hadi waive. Kuna usalama hapo? Kazi kwenu walaji wa pweza mnaosaka nguvu za ziada

mi nakula kujenga afya na sio nguvu kwani nguvu ni genye zako tu..
 
Usipo ijulia upishi wa Pweza !! utaathirika na kukumbwa na food poision, tafadhali kuwa mwangalifu.!
 
Kwenye freezer anakaa muda gani akiwa mbichi bila kuharibika s.crony

Km freezer yako ni nzuri anakaa muda mrefu tu...mi naweka wa2/3 natumia mwezi mzima,lkn kwa Tanesco yetu hii na kwa vyakula vya baharini unashauriwa kutumia haraka mara baada tu ya kununua kuepuka food poisoning nk.Jaribu kutayarisha hii kitu utakuja niambia hapa hapa.hakikisha unanunua aliyepigwa tayari jaribu kuuliza kabla hujanunua....
 
Km freezer yako ni nzuri anakaa muda mrefu tu...mi naweka wa2/3 natumia mwezi mzima,lkn kwa Tanesco yetu hii na kwa vyakula vya baharini unashauriwa kutumia haraka mara baada tu ya kununua kuepuka food poisoning nk.Jaribu kutayarisha hii kitu utakuja niambia hapa hapa.hakikisha unanunua aliyepigwa tayari jaribu kuuliza kabla hujanunua....
mfafanulie vizuri kuhusu aliyepigwa, sio kupikwa
 
mi nakula kujenga afya na sio nguvu kwani nguvu ni genye zako tu..

sasa ndugu, si nimeeleza uandaaji wake? Hizo nailoni hazibagui pa kudhuru. Fuata ushauri wa scrony. Nenda kanunue upike nwenyewe
 
Pweza wa vipande barabarani hana faida yoyote zaidi ya kukuletea maradhi.....hakuna nguvu yoyote utakayoipata hapo.Unataka msaada wa mawazo,nenda feri nunua pweza wako 1kg ni km buku 4-5 hivi.....fika nae nyumbani muoshe vizuri kwanza kwa maji ya kawaida,pili maji ya moto huwa anakuwa na michanga sana mikiani.weka jikoni usiweke maji kwanza mpaka akaushe maji yake mwenyewe,kisha weka maji kwa supu yako,tupia kitunguu kiasi kuongeza hamu na km una kitunguu saum kiasi ni bora chemsha km dk30.Hii ni zaidi ya "mkuyati" hutotumia Viagra tena!

kaka kilo moja ya pweza???? unataka kukesha???
 
Back
Top Bottom