TAHADHARI: Kituo cha Mafuta Triple A Arusha ni wezi

TAHADHARI: Kituo cha Mafuta Triple A Arusha ni wezi

Preta

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2009
Posts
24,320
Reaction score
18,884
Kwa kuwatahadharisha tu wale weekenders wezangu, epukeni kuweka mafuta pale hasa nyakati za usiku.

Kuna kaka mmoja yeye ndio bingwa wa kuchezea pump, baada ya kumshtukia alidai pump sio nzima ni mbovu na kuifunga muda ule ule.

Kwa anaemfahamu mmliki wake (Laseko) tafadhali amjulishe kuwa wafanyakazi wake si waaminifu.

EWURA tafadhali tunaomba mpite eneo lile mkague zile pump
Niliweza kupata picha kidogo ya muonekano wake..

FDBBF623-BC6D-4094-AE3A-21DE3F6C6939.jpeg
 
Harufu ya kituo kufungwa naisikia masikini ungeomba hata ka takrima ili ufunge mdomo!
 
Kwa taarifa yako, vituo takribani vyote vina pump kwa ajili ya gari za daladala/bodaboda na pump kwa ajili ya 'wakuja'.
Hata siku moja pump za 'wakuja' daladala/bodaboda hazielekezwi kuweka mafuta kwan watastukia mchezo. Makonda na madereva wanajua hizo pump. Waulize watakwambia.
 
Kama wamechoka na biashara bora wauze mayai nasikia yanalipa
 
Kwa kuwatahadharisha tu wale weekenders wezangu, epukeni kuweka mafuta pale hasa nyakati za usiku. Kuna kaka mmoja yeye ndio bingwa wa kuchezea pump, baada ya kumshtukia alidai pump sio nzima ni mbovu na kuifunga muda ule ule. Kwa anaemfahamu mmliki wake (Laseko) tafadhali amjulishe kuwa, wafanyakazi wake si waaminifu
EWURA tafadhali tunaomba mpite eneo lile mkague zile pump
Niliweza kupata picha kidogo ya muonekano wake


Ahsante sana mkuu kwa tahadhari.

Juzikati niliweka mafuta ya shs 20,000 baada ya kutoka Tripple A, break ya kwanza ilikuwa Babylon Club, ila kabla ya kupark nikaona kama kuna dalili za mafuta kuisha, ikabidi nifanye kucheck upya ikiwa ni pamoja na kwenda pale Mount Meru Petroleum Meru Posta.

Sikufanikiwa kufika kwani niliishiwa mafuta pale Benson & Company. Later niligundua kuwa hakukuwa na mafuta kwenye gari (hapo dumu la mafuta na toyo ya kuyafuata mafuta petrol station viliokoa jahazi).

Baada ya kuweka upya mafuta (na kutoa upepo kwenye fuel system) nikarudi tena kule tTriple A na kuwapigia kelele pale nilipokuwa nimeweka mafuta earlier (Triple A) ndipo nilipofuatwa na madereva taxi na toyo wakanituliza kuwa ndio tabia ya pale ila nisiwataje.

Tabia kama hizi ni mbaya sana na ni vema vyombo vinavyohusika vikafuatilia kwa siri na wakigundua kuwa tunaibiwa wakifungie kituo hicho na vituo vyenye tabia hizo kwani ndio uwajibikaji wa jumla kwani waajiri ndio wanaowapa wafanyakazi/mfanyakazi nafasi za kutekeleza majukumu ya kazi zake.

Kwa kifupi, mwajiri ndiye nayebeba dhamana ya mfanyakazi wake.

Hii tabia ikomeshwe nchi nzima kwa waathirika kuifichuliwa pindi wafanyavyo tukio kama hili.
 
Basi wote tutahamia Manjis (japo pia sina uhakika wa uaminifu wao).......
Hakuna hela ya rahisi tena....hakuna kuchakachua. Ni kuiba sasa. Tuende kwenye makampuni yanayoeleweka. Haya ya wenzangu na mimi ambao hawataki kujua tunapambana na hali zetu ni tatizo
 
Kwa kuwatahadharisha tu wale weekenders wezangu, epukeni kuweka mafuta pale hasa nyakati za usiku.

Kuna kaka mmoja yeye ndio bingwa wa kuchezea pump, baada ya kumshtukia alidai pump sio nzima ni mbovu na kuifunga muda ule ule.

Kwa anaemfahamu mmliki wake (Laseko) tafadhali amjulishe kuwa wafanyakazi wake si waaminifu.

EWURA tafadhali tunaomba mpite eneo lile mkague zile pump
Niliweza kupata picha kidogo ya muonekano wake..

View attachment 637449
Kwa kuwatahadharisha tu wale weekenders wezangu, epukeni kuweka mafuta pale hasa nyakati za usiku.

Kuna kaka mmoja yeye ndio bingwa wa kuchezea pump, baada ya kumshtukia alidai pump sio nzima ni mbovu na kuifunga muda ule ule.

Kwa anaemfahamu mmliki wake (Laseko) tafadhali amjulishe kuwa wafanyakazi wake si waaminifu.

EWURA tafadhali tunaomba mpite eneo lile mkague zile pump
Niliweza kupata picha kidogo ya muonekano wake..

View attachment 637449
 
Usiku wa kuamkia leo nilifika pale nipate kucheki kama mtindo ule unaendelea ila waliniwekea mafuta vizuri tu kwa kweli ila nikajua baada ya Preta kuwaanika naona wamefokewa na wamejiboresha mara moja!
 
Dawa na kwenda na kidumu chako cha lita tano unaweka unaona kabisa hii ni lita tano unaenda unaweka kwenye gari yako unasepa
 
Hapo Arusha vituo navyoweka mafuta ni kwenye vituo vya Total, Oryx na Puma.
 
Unatembea na dumu hadi linakuwa kero si bora kuhama kituo. Ukiona wanakuelekeza kwa kujaza kataa. Jichagulie wewe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom