TAHADHARI: Kituo cha Mafuta Triple A Arusha ni wezi

TAHADHARI: Kituo cha Mafuta Triple A Arusha ni wezi

Arusha vituo vingi wanaiba mafuta sio hicho kimoja tuu karibu 70% ya wanaouza mafuta wanaiba sana...
 
Nashukuru sana sana kaka kwa kuleta uzi huu mimi ni muhanga wa hiyo petrol station ilioko mataa karibu na triple A niliweka mafuta ijumaa moja hivi usiku ya sh 20000 cha ajabu nikashangaa geji ya mafuta haikusogea kabisa nikajiuliza inamaana hakuna kilichoingia? Niliibiwa nikahisi kitu

Kwa hili sitorudi pale tena na tena kujaza mafuta kwa wezi kama hawa

Naipenda sana JF kwa kufahamishana mambo ya maana
 
Ahsante sana mkuu kwa tahadhari.

Juzikati niliweka mafuta ya shs 20,000 baada ya kutoka Tripple A, break ya kwanza ilikuwa Babylon Club, ila kabla ya kupark nikaona kama kuna dalili za mafuta kuisha, ikabidi nifanye kucheck upya ikiwa ni pamoja na kwenda pale Mount Meru Petroleum Meru Posta.

Sikufanikiwa kufika kwani niliishiwa mafuta pale Benson & Company. Later niligundua kuwa hakukuwa na mafuta kwenye gari (hapo dumu la mafuta na toyo ya kuyafuata mafuta petrol station viliokoa jahazi).

Baada ya kuweka upya mafuta (na kutoa upepo kwenye fuel system) nikarudi tena kule tTriple A na kuwapigia kelele pale nilipokuwa nimeweka mafuta earlier (Triple A) ndipo nilipofuatwa na madereva taxi na toyo wakanituliza kuwa ndio tabia ya pale ila nisiwataje.

Tabia kama hizi ni mbaya sana na ni vema vyombo vinavyohusika vikafuatilia kwa siri na wakigundua kuwa tunaibiwa wakifungie kituo hicho na vituo vyenye tabia hizo kwani ndio uwajibikaji wa jumla kwani waajiri ndio wanaowapa wafanyakazi/mfanyakazi nafasi za kutekeleza majukumu ya kazi zake.

Kwa kifupi, mwajiri ndiye nayebeba dhamana ya mfanyakazi wake.

Hii tabia ikomeshwe nchi nzima kwa waathirika kuifichuliwa pindi wafanyavyo tukio kama hili.
Hiyo nayo juzi imemkuta rafiki yangu Dodoma hajaniambia ni sheli gani lakini inaonekana kuna mchezo unaoendelea kwa wauza mafuta wa sheli.
 
.....
.....asante kwa taarifa Mkuu niko Lamadi napiga supu ya Sato vichwa vimekuja kuona Nyanza
piga kazi mwana.....umepita shambani lakini wakaona kina msumeno.....masikio.....wa juu....sharubu.....na wa chini.......?.....
 
Nashukuru wakuu. Mimi juzi nilipita kituo cha mafuta jirani na Eland hotel nikakaza mafuta lakini kucheki gauge bado inasoma Empty nikaondoka baru bila kulipa. Siku ya pili nikaenda mchana nikauliza kama Yule aliyeniwekea mafuta Jana yake nikaambiwa kaachishwa kazi asubuhi baada wa wateja kumlalamikia kwa kuwaibia
 
Nadhani hii ni biashara binafsi. Sasa kama muajiri kaona haya malalamiko na bado anasubiri tume shauri yake wafanyabiashara ni wengi wanaopigania fursa na vyuma havijaachia bado.
 
Dawa ni kwenda na dumu transparent halafu unapaki pembeni unamimina
 
Hivi lile Zoezi la kukagua vituo vya mafuta linaendelea au Ilikuwa kik tu

Ova
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom