MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 705
Moderators, sijui kama hapa ni mahala pake, lakini mtajua wenyewe pa kuipeleka hii. Nimeinyaka sasa hivi!
Kuna aina mpya ya utapeli ambayo imeingia jijini Dar. Kuna wajanja fulani ambao wanatumia fursa ya kwamba kila anayepigiwa kelele za Mwizi Mwizi Mwizi hadharani atasulubiwa bila ya kuhojiwa, wamezua mtindo wa kuwaomba watu simu zao, wajifanye wanabip, kisha wanapigiwa, wanawaomba waliowapigia wawatajie namba ya simu waliyoitumia - kwa kuwa ni washirika wenzao katika dili - ili baadaye waje kudai kuibiwa simu.
Katika purukushani ya kumtafuta Mwizi huyo wa simu, ambaye si mwizi, ila yule ambaye anayedai kuibiwa ndiye mwizi halisi, inatajwa namba ya simu inayodaiwa kuibiwa. Inapolia, inaita kwa mtu ambaye si mhusika, hapo hapo anaanza kusulubiwa bila kuhojiwa.
Hii tabia mbaya yetu sisi kuamua kuchukua sheria mkononi pasi na kuhoji ukweli wa tuhuma sasa inawafikia pabaya raia wema. Kaeni chonjo, msije kuitwa wezi. Ushauri: Mtu usiyemfahamu akikuomba simu yako akabip kataa kata kata, mwambie simu yako haibip hata siku moja, anakushusha hadhi! Akisema si wewe unayebip, unamwambia hata kama si wewe! Akileta za kuleta unamkata kibano cha nguvu na kumpigia kelele za Mwizi Mwizi, wamsulubu yeye!
./Mwana wa Haki
Kuna aina mpya ya utapeli ambayo imeingia jijini Dar. Kuna wajanja fulani ambao wanatumia fursa ya kwamba kila anayepigiwa kelele za Mwizi Mwizi Mwizi hadharani atasulubiwa bila ya kuhojiwa, wamezua mtindo wa kuwaomba watu simu zao, wajifanye wanabip, kisha wanapigiwa, wanawaomba waliowapigia wawatajie namba ya simu waliyoitumia - kwa kuwa ni washirika wenzao katika dili - ili baadaye waje kudai kuibiwa simu.
Katika purukushani ya kumtafuta Mwizi huyo wa simu, ambaye si mwizi, ila yule ambaye anayedai kuibiwa ndiye mwizi halisi, inatajwa namba ya simu inayodaiwa kuibiwa. Inapolia, inaita kwa mtu ambaye si mhusika, hapo hapo anaanza kusulubiwa bila kuhojiwa.
Hii tabia mbaya yetu sisi kuamua kuchukua sheria mkononi pasi na kuhoji ukweli wa tuhuma sasa inawafikia pabaya raia wema. Kaeni chonjo, msije kuitwa wezi. Ushauri: Mtu usiyemfahamu akikuomba simu yako akabip kataa kata kata, mwambie simu yako haibip hata siku moja, anakushusha hadhi! Akisema si wewe unayebip, unamwambia hata kama si wewe! Akileta za kuleta unamkata kibano cha nguvu na kumpigia kelele za Mwizi Mwizi, wamsulubu yeye!
./Mwana wa Haki