Tafsiri ya 'Hapa Kazi Tu'

Tafsiri ya 'Hapa Kazi Tu'

Wakati wa kampeni Mh Pombe alipiga pushapu, wakati mwingine alicheza kiduku akiwaambia wananchi hasa wale wanyonge mimi nitafanya kazi usiku na mchana na nitatengeneza serikali rafiki kwa wanyonge akasema "HAPA KAZI TU" Wananchi wanyonge wasioijua michezo ya wanasiasa wakapiga makofi na kushangilia hadi kuombwa wanyamaze!

Nawauliza wanyonge vipi serikali hii ni rafiki kwetu?

Hebu nenda mabibo na kariakoo au nenda soko kuu Arusha au pale Kilombero kaulize bei ya kitu chochote alafu uje uniambie unaona nini mbele?

Majambazi wakivamia watu siku hizi wanakauli mbiu moja tu "HAPA KAZI TU" ndo maana nauliza kauli hii hasa ina maana gani?

Waziri mmoja akasema hata kama unavibali nyumba itabomolewa tu "Hapa kazi tu" akasema eti mimi raiya nikamshitaki yule aliyenipa vibali! Very interesting:🙁 yaani afisa wa serikali mwenye mamlaka na aliyepewa dhamana na serikali na wakampa mihuri ya serikali ili afanye maamuzi leo eti mimi raiya nimwajibishe!

Swali la mwisho kwa leo::hivi hii kauli ya "HAPA KAZI TU" inamuhusu kila anayeenda kinyume au ikifika maeneo Ofisi za CCM Lumumba, majengo ya wahindi upanga, ofisi za DART na KEBY´S HOTEL itageuka na kuwa HAPA PITA TU?
Hivi kubadili gia angani maana yake nini??
 
Mtaisoma namba. Lazima Magufuli awanyooshe. Mlizoea kupora maeneo ya wazi. Lazima mbomolewe
 
Chadema kila siku wanaponda viongozi Wa ccm kuwa ni wabovu lkn cha kushangaza ukifika uchaguzi chadema haohao wanaazima wagombea ccm.!?!!

Mgombea wao alitoka ccm

Wabunge Wa viti maalumu chadema wameteuliwa kutoka ccm
 
Unataka nimjibu nini? Wewe usiye na kazi waweza mjibu mjinga mwenzio.

Kutwa kucha mshinda mitandaoni na viherehere kibao vya kupost ujinga... Mmeharibu hata maana ha great thinkera.
Khaaa ndiyo jibu Thinkera ndiyo kisomi?
 
Eti Pumba
kwa nini unataka kuitafsiri kwa "kingerza" (hivyo ulivyoandika) ????
Uitafsiri kwa makalori - hii maana ya kazi!
 
Habar zenu wanajamiii wenzangu

nimekwama nilikua naomba msaada kwa anayejua kingerza cha HAPA KAZI TU,,,

Mara nyingi wanasiasa wanaogea sana kuliko wanavyoweza kutenda! Dr. Magufuli, alitaka kujitenga na wanasiasa wa aina hiyo. Kwa kusema yeye yuko tayari kutenda kila anachoamini kitakidhi matarajio ya wapiga kura. Kwa tunaweza kusema "For action"
 
Hapa kazi tu inatoa nafasi kwa watu wabaya. ningependa iwe KAZI NA UTU. kila mtanzania mkubwa kwa mdogo anaweza kukumbwa na wimbi la hii kauli. ni mmoja ambaye hatakumbwa nayo naye ni mwanzilishi wake.
 
Kiingereza chenywe hujui masikini wewe lakini kiherehere hakikuishia!!

Kazi yako kuiga tu, unangoja wenzio waseme ili udakie, acha dharau kwa mkuu wetu WA nchi, wenzio tumeshaweka pembeni tofauti zetu zamani sasa tunajipanga kujenga nchi yetu wewe umeng'angana na propaganda zisizo na maana.

Kama huna kazi sema tukuajiri huenda ujinga ukakutoka.
Hongera... hata wale wa milembe wanadhani sisi ndo vichaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom