Hili ni swali napenda tu kujua tafiti zinasemaje kuhusu ulaji wa nyama ya ndege huyu.
Amekuwa kero kila kona na walio wengi wanajua kero zake sasa sitaki kuzungumzia hilo ila napenda kujua kwa yeyote anayejua kama ulaji wa nyama yake una madhara yoyoye kiafya.
Ikiwa ina madhara kiafya basi tuendelee tu kuikabili adhaa ya ndege huyu, ila kama hana madhara basi tujuzwe tujifarij na nyama yake. Ni hayo tu
Mkuu wewe unataka nani akujuze wakati wewe mwenyewe unaweza kufanya utafiti kujua kwamba nyama yake inafaa kwa matumizi ya Binadamu.
Fanya hivi; kamata Kunguru, chinja, muandae kwa kumnyonyoa jinsi vile kuku anavyoandaliwa na kisha mpe mbwa au paka, hao wanyama wakila basi hiyo itakuwa ni hatua ya kwanza, hakafu endelea hivyo kwa kama wiki 2-3 kukamata kunguru na kuwapa hao wanyama, baada ya muda huo angalia maendeleo ya kiafya ya hao wanyamaa,kama wanapenda sana kula hiyo nyama na hakuna madhara basi hiyo ni hatua kubwa sana.
Hatua ya pili ni kukamata kunguru na kuwaandaa halafu kupika nyama yao na kuwapatia tena hao wanyama na ufanye hivyo kwa muda fulani hadi utakaporidhika kwamba hakuna madhara yaliyojitokeza kwao.
Hatua inayofuata ndiyo hatua kubwa na ngumu sana, kamata kunguru, chinja, muandae na chukua nyama ya kidari ikaange na bizari na pilipili kichaa, ndimu na chumvi nk, basi hapo unaweza kula wewe mwenyewe kiduchu huku ukisikilizia kwa mbali kama kwamba unaonja sumu, kama ladha yake itakuwa muruwa basi kesho tena endelea kufanya hivyo kidogo kidogo hatimaye unaweza kujigundua kama kuna au hakuna madhara yoyote mwilini mwako-- hatua hiyo ndiyo itakuwa mwisho wa utafiti wako kwamba KUNGURU NI MBOGA AU SIYO MBOGA.
Ni katika kujitoa kwa aina hiyo ndipo watu tumeweza kujua kwamba kumbe hata mende, Panya,dagaa, samaki,nk ni vyakula bora kwa Binadamu.
Basi mkuu wakati ndiyo huu wa kufanya hilo jaribio.