Tafakuri Pembuzi: Ni rahisi kupunguza Mawaziri ila siyo Wizara

Halfcaste

JF-Expert Member
Nov 28, 2010
972
215
Nimesikia na nimepitia maoni ya watu wengi kuhusu Mh.Rais JPM kuhusu kupunguza Wizara hadi 15. Lakini wengi wetu hatuelewi kuwa hata Wizara ukiipa jina sijui Tume au Idara au Agency bado gharama za uendeshaji ni zile zile, watumishi ni walewale na gharama za uwekezaji katika Kitengo hicho ni hizo hizo.

Mfano, Unaunganisha Wizara ya Maji, Kilimo, Mifugo na Biashara. Hapa hujapunguza Wizara umepunguza Mawaziri tu, Tena utaongeza Wakurugenzi na Makatibu Wakuu waweze kumsaidia Waziri. Gharama za uendeshaji wa kila Idara sijui Kitengo utakavoita wewe zipo palepale.

Narudia siyo rahisi kupunguza Wizara labda idadi ya Mawaziri.

Nakaribisha michango bila mahaba na mihemko ya kisiasa.
 
Nimesikia na nimepitia maoni ya watu wengi kuhusu Mh.Rais JPM kuhusu kupunguza Wizara hadi 15. Lakini wengi wetu hatuelewi kuwa hata Wizara ukiipa jina sijui Tume au Idara au Agency bado gharama za uendeshaji ni zile zile, watumishi ni walewale na gharama za uwekezaji katika Kitengo hicho ni hizo hizo.

Mfano, Unaunganisha Wizara ya Maji, Kilimo, Mifugo na Biashara. Hapa hujapunguza Wizara umepunguza Mawaziri tu, Tena utaongeza Wakurugenzi na Makatibu Wakuu waweze kumsaidia Waziri. Gharama za uendeshaji wa kila Idara sijui Kitengo utakavoita wewe zipo palepale.

Narudi siyo rahisi kupunguza Wizara labda idadi ya Mawaziri. Nakaribisha michango bila mahaba na mihemko ya kisiasa.
Kwa Tanzania ni upuuzi kupunguza wizara.....madaraka yote yapo kwa magufuli hivyo akipunguza wizara imekula kwake ataona kazi aiendi heri niongeze ndio maana walipata kuongeza na kuongeza.Pili hakuna tamko la kisheria
 
Unapunguza gharama za kumhudumia waziri.Pili unaongeza watendaji badala ya wanasiasa.Inasaidia kupunguza urasimu kwanı waziri ata-delegate madaraka kwa watu wa chini.
 
Halfcaste
Hivi umewaza sawa sawa kabla ya kuja na hicho kichwa cha habari? Tangu lini Wizara 2 zinazojitegemea ukiunganisha zinabaki kuwa 2. Yaani Wizara ya Maji + Kilimo na Chakula zikizaa Wizara inaitwa Maji, Kilimo na Chakula bado kwako tafsiri ni 2. Adha, tambua kuwa gharama za uendeshaji ndizo zinatazamwa sio hiyo tafsiri....mfano idadi ya Mawaziri, Katibu wakuu na Wakurugenzi jumlisha na viambata vyao kama Drivers, wasaidizi na huduma nyingine. Vinginevyo zungumzia kubaki kwa majukumu yale yale ya Serikali na si idadi ya Wizara.
 
Kwa Tanzania ni upuuzi kupunguza wizara.....madaraka yote yapo kwa magufuli hivyo akipunguza wizara imekula kwake ataona kazi aiendi heri niongeze ndio maana walipata kuongeza na kuongeza.Pili hakuna tamko la kisheria

Nakuelewa lakini siyo rahisi kupunguza Wizara labda idadi ya Mawaziri tu. Ukiunganisha Wizara ya Nishati,Madini, Maji, Viwanda na Biashara je umrpunguza Wizara au umeunganisha Wizara? Huwezi kuiua Wizara ya Maji kwa gharama zake au utendaji wake au uwekezaji wake. Sana sana Utaongeza Wakurugezi zaidi na Makatibu. Sasa utakuwa umeokoa gharama gani?
 
Je unajua gharama za kumgharimia waziri na naibu wake?
Mfano, wakati wa kikwete aligharamua mawaziri na manaibu mawaziri jumla kama hamsini na kitu, je ilimgharim kiasi gani?
 
Nimesikia na nimepitia maoni ya watu wengi kuhusu Mh.Rais JPM kuhusu kupunguza Wizara hadi 15. Lakini wengi wetu hatuelewi kuwa hata Wizara ukiipa jina sijui Tume au Idara au Agency bado gharama za uendeshaji ni zile zile, watumishi ni walewale na gharama za uwekezaji katika Kitengo hicho ni hizo hizo.

Mfano, Unaunganisha Wizara ya Maji, Kilimo, Mifugo na Biashara. Hapa hujapunguza Wizara umepunguza Mawaziri tu, Tena utaongeza Wakurugenzi na Makatibu Wakuu waweze kumsaidia Waziri. Gharama za uendeshaji wa kila Idara sijui Kitengo utakavoita wewe zipo palepale.

Narudi siyo rahisi kupunguza Wizara labda idadi ya Mawaziri. Nakaribisha michango bila mahaba na mihemko ya kisiasa.

Kwa Tanzania ni upuuzi kupunguza wizara.....madaraka yote yapo kwa magufuli hivyo akipunguza wizara imekula kwake ataona kazi aiendi heri niongeze ndio maana walipata kuongeza na kuongeza.Pili hakuna tamko la kisheria

Tulieni kabisaaa!!! kama Uwezo wenu umeishia hapo, ulizeni badala ya kuleta thrd inayoonyesha ufahamu juu ya wizara na idara zake, wakati hamuelekei kujua maana ya kupunguza wizara.

Mtu anajiandikia tu eti makatibu wakuu wanabaki walewale! Kwa nini? Unaamini kabisa kwamba unahitaji wizara ya jinsia na watoto na wapewe waziri, naibu, katibu mkuu, wakurugenzi, nk.? Yaani unadhani makatibu wakuu waote lukuki tulionao hawawezi kuongezewa kazi na wakaziweza?

Magufuli, futa wizara.
-Jinsia na watoto + maendeleo ya jamii weka pamoja liwe desk ndani ya wizara ya elimu
-Futa wizara ya mifugo na uvuvi. Mifugo weka pamoja na kilimo kama ilivyo ndani ya FAO. Uvuvi rudisha idara ndani ya maliasili na utalii
-Madini peleka maliasili. zote hizi ni malia asili.
-Maji unganisha na Nishati kama zamani
-Elimu unganisha na sayansi na technolojia. huko ndo kuna vyuo vikuu wanaofanya tafiti za sayansi na technolojia yake
-Hao TAMISEMI wanahitaji kutawaliwa kivingine maana ni mchwa!!!!!! hii naomba unipe consultancy ili niwakague vizuri
-Afya weka pamoja na mazingira kama ilivyo nchi nyingi maana hii nayo imekuwa kama ni wizara ya Muhimbili badala ya Afya.
-Uchukuzi na ujenzi, funga pamoja. wote ni kazi moja inafanana!
-Afrika mashariki weka ndani ya mambo ya nje.
-Mambo ya ndani ongeza mambo ya Sheria. Katiba haitakiwi iwe ndani ya wizara!
-Ulinzi futa waziri weka chini ya ofisi ya rais na hapo kuna makamu wa rais ambaye hana kazi za kila siku. Lazima alee wizara hii. kuweka waziri haina tija anaishia kusoma hotuba tuuuuu!
-Weka wizara ya mawasiliano, futa!!!! tangu lini wizara ikawa ni ya kuzungumzia simu za mkononi tuuuuuuu! tume ya mawasiliano ndani ya wizara ya ujenzi na miundombinu inatoshaa!

Hizi zingine, nakuja hapo tutete kidogo lakini nina wazo zuri sana juu ya kuwa na naibu waziri wengi ktk wizara wanaoishia kutumwa na mawaziri. Waziri lazima awe na afya nzuri na akili nzuri na aweze kufanya kazi masaa yote! anayeshindwa OUT! na waingie vijana lakini siyo hawa wanaoishia kuchora katuni mitandaoni.
 
Halfcaste
Hivi umewaza sawa sawa kabla ya kuja na hicho kichwa cha habari? Tangu lini Wizara 2 zinazojitegemea ukiunganisha zinabaki kuwa 2. Yaani Wizara ya Maji + Kilimo na Chakula zikizaa Wizara inaitwa Maji, Kilimo na Chakula bado kwako tafsiri ni 2. Adha, tambua kuwa gharama za uendeshaji ndizo zinatazamwa sio hiyo tafsiri....mfano idadi ya Mawaziri, Katibu wakuu na Wakurugenzi jumlisha na viambata vyao kama Drivers, wasaidizi na huduma nyingine. Vinginevyo zungumzia kubaki kwa majukumu yale yale ya Serikali na si idadi ya Wizara.

Nadhani umenielewa tu. Huwezi kupunguza Wizara labda Mawaziri. Sana sana utaunganisha hizo Wizara lakini gharama za uendeshaji na uwekezaji zitakuwa palepale.
 
Nimesikia na nimepitia maoni ya watu wengi kuhusu Mh.Rais JPM kuhusu kupunguza Wizara hadi 15. Lakini wengi wetu hatuelewi kuwa hata Wizara ukiipa jina sijui Tume au Idara au Agency bado gharama za uendeshaji ni zile zile, watumishi ni walewale na gharama za uwekezaji katika Kitengo hicho ni hizo hizo.

Mfano, Unaunganisha Wizara ya Maji, Kilimo, Mifugo na Biashara. Hapa hujapunguza Wizara umepunguza Mawaziri tu, Tena utaongeza Wakurugenzi na Makatibu Wakuu waweze kumsaidia Waziri. Gharama za uendeshaji wa kila Idara sijui Kitengo utakavoita wewe zipo palepale.

Narudia siyo rahisi kupunguza Wizara labda idadi ya Mawaziri.

Nakaribisha michango bila mahaba na mihemko ya kisiasa.

Gharama haziwezi kuwa zile zile hata kidogo.

Chukulia mfano kutoka Wizara 26 had 15. Idara ni zile zile sawa, lakini kuna gharama za mishahara ya mawaziri, makatibu wakuu, maafisa utumishi wa wizara nk vinapungua. Pia magari yao, mafuta ya magari pia vinapungua. Siku za kuwasilisha budget zao bungeni zinapungua. Wakati mwingine wizara mpya huitaji majengo yake!

Kwa hiyo ukubwa wa serikali, kwa maana ya idadi ya wizara ni suala nyeti sana. Kuna nchi wameliona hilo na wamelipatia ufumbuzi kikatiba. Kuna njia mbili. Wengine idadi ni fixed (India) na wengine wameweka kikomo kwamba isizidi idadi fulani (Kenya).
 
Je unajua gharama za kumgharimia waziri na naibu wake?
Mfano, wakati wa kikwete aligharamua mawaziri na manaibu mawaziri jumla kama hamsini na kitu, je ilimgharim kiasi gani?

Sasa ni kusaidie hivi huwezi kupunguza Wizara labda idadi ya Mawaziri. Na ukiunganisha Wizara tatu au nne ni lazima uongeze Wakurugenzi na Makatibu wakuu ili wamsaidie huyo Waziri mmoja. Je, umesave nini hapo? Kuku ni kuku jogoo jina tu.
 
Gharama haziwezi kuwa zile zile hata kidogo.

Chukulia mfano kutoka Wizara 26 had 15. Idara ni zile zile sawa, lakini kuna gharama za mishahara ya mawaziri, makatibu wakuu, maafisa utumishi wa wizara nk vinapungua. Pia magari yao, mafuta ya magari pia vinapungua. Siku za kuwasilisha budget zao bungeni zinapungua. Wakati mwingine wizara mpya huitaji majengo yake!

Kwa hiyo ukubwa wa serikali, kwa maana ya idadi ya wizara ni suala nyeti sana. Kuna nchi wameliona hilo na wamelipatia ufumbuzi kikatiba. Kuna njia mbili. Wengine idadi ni fixed (India) na wengine wameweka kikomo kwamba isizidi idadi fulani (Kenya).

Kwahiyo ukiunganisha Wizara, Wizara ya Maji, Nishati, Madini, Viwanda na Biashara makatibu wakuu, Watumishi na Wakurugenzi wa Wizara/ Vitengo hivo wanaachishwa kazi? Ndugu yangu hakuna kitu kama hicho.

Presentation na discussion ya Bajeti ya Wizara kubwa kama hiyo Bungeni lazima ile siku kibao kaka, huwezi kujadili sijui " Idara ya Maji au Kitengo cha maji kwa masaa mawili. Huyu bado anaitwa kuku jogoo jina tu.
 
Tulieni kabisaaa!!! kama Uwezo wenu umeishia hapo, ulizeni badala ya kuleta thrd inayoonyesha ufahamu juu ya wizara na idara zake, wakati hamuelekei kujua maana ya kupunguza wizara.

Mtu anajiandikia tu eti makatibu wakuu wanabaki walewale! Kwa nini? Unaamini kabisa kwamba unahitaji wizara ya jinsia na watoto na wapewe waziri, naibu, katibu mkuu, wakurugenzi, nk.? Yaani unadhani makatibu wakuu waote lukuki tulionao hawawezi kuongezewa kazi na wakaziweza?

Magufuli, futa wizara.
-Jinsia na watoto + maendeleo ya jamii weka pamoja liwe desk ndani ya wizara ya elimu
-Futa wizara ya mifugo na uvuvi. Mifugo weka pamoja na kilimo kama ilivyo ndani ya FAO. Uvuvi rudisha idara ndani ya maliasili na utalii
-Madini peleka maliasili. zote hizi ni malia asili.
-Maji unganisha na Nishati kama zamani
-Elimu unganisha na sayansi na technolojia. huko ndo kuna vyuo vikuu wanaofanya tafiti za sayansi na technolojia yake
-Hao TAMISEMI wanahitaji kutawaliwa kivingine maana ni mchwa!!!!!! hii naomba unipe consultancy ili niwakague vizuri
-Afya weka pamoja na mazingira kama ilivyo nchi nyingi maana hii nayo imekuwa kama ni wizara ya Muhimbili badala ya Afya.
-Uchukuzi na ujenzi, funga pamoja. wote ni kazi moja inafanana!
-Afrika mashariki weka ndani ya mambo ya nje.
-Mambo ya ndani ongeza mambo ya Sheria. Katiba haitakiwi iwe ndani ya wizara!
-Ulinzi futa waziri weka chini ya ofisi ya rais na hapo kuna makamu wa rais ambaye hana kazi za kila siku. Lazima alee wizara hii. kuweka waziri haina tija anaishia kusoma hotuba tuuuuu!
-Weka wizara ya mawasiliano, futa!!!! tangu lini wizara ikawa ni ya kuzungumzia simu za mkononi tuuuuuuu! tume ya mawasiliano ndani ya wizara ya ujenzi na miundombinu inatoshaa!

Hizi zingine, nakuja hapo tutete kidogo lakini nina wazo zuri sana juu ya kuwa na naibu waziri wengi ktk wizara wanaoishia kutumwa na mawaziri. Waziri lazima awe na afya nzuri na akili nzuri na aweze kufanya kazi masaa yote! anayeshindwa OUT! na waingie vijana lakini siyo hawa wanaoishia kuchora katuni mitandaoni.

Utafanikiwa kuungunisha lakini bado hujapunguza Wizara labda umepunguza Mawaziri na lazima uongeze Makatibu wakuu na Wakurugenzi. Gharama za uendeshaji na uwekezaji katika sijui idara au kitengo zipo palepale kuanzia Wizarani mpaka Wilayani. Kuku ni Kuku jogoo jina tu.
 
Au mimi ndo sielewi! Yaani wizata ukizikombaini gharama iwe sawa,you must be crazy,Umepunguza mawaziri unahudumia wazr mmoja mshahar nyumba umeme na ulinzi,Bado makatibu wakuu wanaghalama sana nayo ni faida pia accomodation za mawaziri watatu si sawa na mmoja.Unafikiri tofauti.Faida ni kubwa sana kupunguza wizara.

Pia usisema eti ikiitwa idara gharama ni ileile No. Idara ni Idara na Wizara ni wizara tu tofauti kabisa.
 
Cha msingi ni kaz tu. Hizo gharama za kuwalipa mawazir sio issue kama wanaleta tija zaidi.
 
Back
Top Bottom