Tafakari: Vitambulisho vya taifa

Kisusi Mohammed

JF-Expert Member
Aug 10, 2009
563
468
Assalaamu alaykum, hongereni kwa swaum. Hili zoezi la vitambulisho vya taifa sijalifatilia kwa undani, ila kwa mtazamo wa jumla linaonekana kuwa na nia njema na wananchi wa Tanzania. Kinachonipa tabu katika zoezi hili ni kuhusu mchakato wa utoaji taarifa kwa wananchi, uandikishaji, vitendea kazi vya zoezi, rasilimali watu na uwezo wao na kubwa zaidi ni vigezo vya mwananchi muandikishwaji. Kwa mfano: Mimi sikubahatika kupitiwa na wale vilaza waliokuwa wanaandikisha watu nyumba kwa nyumba, nilipokwenda ofc za serikali ya mtaa wakaniambia kuwa, kwa waliokosa kuandikishwa mtaani wataandikishwa tar. 28, 29 na 30. Waende na vivuli vya viambatanisho (kadi ya mpiga kura au leseni ya udereva au cheti cha kuhitimu shule). Kwa bahati leo asubuhi nikawa mtu wa kwanza kufika kituo cha kuandikisha nikiwa na vivuli vya viambatanishi vyote walivyohitaji, nilipofika kwa muandikishaji ananiambia sina barua ya kunitambulisha toka kwa mjumbe wangu! Nimeshindwa kuelewa kwa nini hawakuorodhesha kigezo hicho cha barua ya utambulisho ya mjumbe toka zamani kwny matangazo yao ya vipeperushi?! Kwa kweli imenikera, na kwa upuuzi huo, nimeahidi kuwa, sihitaji tena hicho kitambulisho chao kwa sbb hata taifa lenyewe limeshauzwa na kutaifishwa na walafi wachache wenye madaraka, ndio maana hata zabuni yenyewe ya hivi vitambulisho wamepeana kishemeji ili waendelee kutumaliza kabisa. Imeniuma sana.
 
Mbona wengine hatukuulizwa ujinga huo wa barua ya utambulisho?Iweje wewe tu?.Na ni wapi ulienda kujiandikisha?
 
Nafikiri wamekuomba hivyo kwa kuwa hukuandikishwa kwa mara ya kwanza na mjumbe wako. Kosa ninaliliona hapa, ni la wao kushindwa kuwaambia kuwa hiyo tarehe husika muende mkiwa na huo utambulisho kutoka kwa mjumbe wenu.
 
ukiona hivyo ujue uraia wako una walakini!

Sio kweli kuwa uraia wake una walakini; mimi pia nimepatwa na masahibu hayo huku Mbezi Beach!! Tuliambiwa kwanza hao waandikishaji wangepita nyumbani kwetu na hawakufanya hivyo, tulipokwenda ofisi ya serikali ya mtaa tukaambiwa waandikishaji walihamia shule ya msingi Mbezi beach tuende huko kujiandikisha. Tulipofika kule tukaambiwa tumtafute mjumbe wetu tuongozane nae mpaka hapo kituoni; lakini mjumbe mwenyewe haonekani full time kwenda kulewa hivyo tumeshindwa kujiandikisha kwa kuwa sasa imekuwa ni kero!!
 
Back
Top Bottom