Tabora ni sawa na Torabora

Tabora ni sawa na Torabora

Duh! Kumbe na mwaka huu tumeshika mkia matokeo ya Darasa la saba?
 
Na ikiwekwa mada ya kaskazini hapa nyie nyie ndio wa kwanza kuponda teh. Ati torabora duh! Elimu. Elimu. Elimu.
 
Tumbaku ni kisingizio tu, mfano tabora mjini hakulimwi tumbaku lakini mji umekaa kimwinyi tu, watoto wa kike wanawaza kuolewa tu na sio kusoma, mzazi yupo tayari kumtoa mtoto shule ampeleke kwa bwana bila kujali umri wa mtoto, Tabora kukikucha wazee wanakaa vibarazani kucheza bao na kunywa kahawa sio kufikiria kipato kinaongezwaje kwenye kaya na mtot kwenda shule ni mapenzi yake, kifupi hakuna familia inayotoa msisitizo wa elimu kwa watoto.
 
Kweli Tabora inahitaji ibadilike kwanza kifikra,kabla ya kuwa na ufaulu mzuri.Yaan wale watu bora tu wangehamia Zanzibar maana ni kama waswahili sana isee.
 
Inauma sana wadau sasa nin kifanyike jaman maana kila nikipitaga mitaa ya ng'ambo huwa nashindwa kujizuia kulia kwa nguvu
 
Hee mdugu wane mnya Sikonge selesele.........
Itatizo lya ntola ni hostoria ya mwalawo niswe bila komanya kwa copy na kopest ka utaratibu kavo, kofuma ndiyo kosapa ipango do mpa mpende, lkn genekele gina madoka na biashara zenge, masula malavo
 
Duh! Kumbe na mwaka huu tumeshika mkia matokeo ya Darasa la saba?

Can You imagine??? Yaani hapana hili halikubaliki. Inatakiwa kuwabana wabunge kwa kushirikiana na viongozi wa Mkoa Wa Tabora lazima walifanyie kazi suala hili. Kwanza wafanye rapid assessment angalau kujua sababu za kuufanya mkoa wa Tabora kushika nafasi yamwisho( nina hakika ina-correlate na marks hafifu) na Prof. Ndalichako tafadhali hakikisha elimu ya TZ inapanda kama huko miaka ya nyuma! bahati mbaya sijayaona matokeo ili kujua pamoja na TBR kushika nafasi ya mwisho wamepata alama gani? Nafahamu ma-professor wengi waliotokea mkoa wa Tabora ( kina Professor Dr. Nhonoli (RIP), Prof. Shija, Prof. Maganga (RIP) na wengineo, hii inaonyesha kuwa tatizo sio IQ huenda ni Mazingira. All in all utafiti ufanyike, wadau washirikishwe ( sisi kama wana JF tuwashinikize wafanye kazi na motto uwe endapo TBR itakuwa ya mwisho, wabunge wote tutahakikisha wanaangushwa). elimu ni muhimu let us join our hands!
 
Kweli Tabora inahitaji ibadilike kwanza kifikra,kabla ya kuwa na ufaulu mzuri.Yaan wale watu bora tu wangehamia Zanzibar maana ni kama waswahili sana isee.
kabisa mkuu, waswahili kwisha kazi, wao wanaona maendeleo ni anasa mtu karithi nyumba anachofanya ni kununua mikeka tu ya kukalia kupiga soga, mi sielewi ule usemi mzigo mzito mpe mnyamwezi ulitokana na nini?
 
Kama shilole yupo vile basi hao wengine si watakuwa vichaa kabisaa
 
Watu walikwenda Tobhorwa wakapata elimu na kurudi sehemu nyingine kuendesha maisha mazuri.Watumishi hawapewi morali ya kazi na wakuu wao.Usisahau wenyeji hasa wazee wanapenda umwinyi na kutokuwa na malezi mazuri kwa watoto wao.
Watu tulioishi na kusoma Tabora hatupati hamasa ya huo mji.Barabara mbovu/usafiri mgumu mno.Wenyeji halisi nao si wazalishaji mali wazuri.Wanazidiwa na wageni hasa waha ambao huchuma mali na kujiondokea.
Viongozi wakubwa wakipelekwa huko wanawaogopa wenyeji.Haifurahishi.Bado kuna tabia ya udokozi,wizi na ujambazi wa hali ya juu na wa kutisha mnoo....!
Watu wa hapo Mbokamanyema wanahitaji kusafisha negative attitudes na hata kuiga mazuri ya wengine si vibaya.Na vilevile uchaguzi wa viongozi wa siasa ufanywe kwa akili na moyo.Bila hayo mkoa utabaki kuwa wa hovyo.
 
Ila kuna vyombo mixer mnyamwezi mmanyema na burushi si mchezo.Alie sema umwinyi namuunga mkono kujitambua bado sana ndo maana hata wazawa wa hapo huhamia sehemu nyingine na kubakia kuja kusalimia.
 
Unajua kuna vitu huwa pia vinachangia mkoa kuwa na mwamko wa kielimu.Ukiondoa sera nzuri za elimu, vitendea kazi, uwezo wa wazazi kuwagharamia watoto wao elimu, kuna kitu watu wanakisahau ambacho mimi huwa nakina ni cha muhimu sana yaani uwepo wa watu mashuhuri ambao wanafunzi watapenda kwenda shule ili wawe kama wao. Sasa huko tabora wanafunzi wakiangalia watu wao ambao ni maarufu kama prof kapuya,prof lipumba, sitta, Dr kitila mkumbo,rage wanafeli wakiwa darasa la kwanza.So sishangai kwa haya yanayotokea.
teh teh te nimeishia kucheka tu
 
wanatabora mpambane kwasababu mwenye nacho huongezewa na kama huna jitahidi kuwanacho ili uongezewe

Na pia kila moja anapojitahidi kujitoa katika hali ya chini nchi inakuwa na watu wenye elimu zaidi
 
Mkoa wa Tabora wenye mkoa wao hawajitumi kufanya kazi.Je wanategemea watu wa kutoka mikoa mingine waje wawaletee maendeleo?
 
Watu hawana muamko wa elimu. Sasa elimu bure tuone kama watachangamkia hiyo elimu ya bure.Nashauri Afisa elimu wa Mkoa ,Wilaya washirikiane na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa pamoja na mjumbe wapite nyumba hadi nyumba ili wenye haki ya kwenda shule waipate.
 
Back
Top Bottom