Table manners - tusaidiane

Table manners - tusaidiane

ukichokonoa meno mdomo. ukiwa wazi;ziba mdomo kwa mkono usikenue utawatia kinyaa wengine kuyaona meno yako.

ukipaliwa sitisha kula kwanza mpaka kipalio kipoe.

usilalamikie chakula mbele ya mpishi..mfano chakula hakijaiva, chakula kina chumvi, chakula kina mafuta mengi n.k kufanya hivi kutamkatisha tamaa mpishi pengine akashindwa kula..

yashanikuta,yani siku home kwa bahati mbaya nimeboronga kupika ,kuzidisha chumvi nk wanasemajee,hadi appetite inapotea yote
 
1. Ukitafuna chakula jitahidi usifanye ile - che che che che/cha cha cha cha

2. Ukiwa unakula na wenzio jitahidi kujizuia - ghaaaa (mbweo/mbwewe) sijui

3. Muda wa kula jitahidi usiwe mtu wa kuonge ongea - mvua tafadhali/mimate inaruka

4. Jitahidi kutokuenda haja ndogo/kubwa kati kati ya chakula yaani unaacha msosi katikati kisha unarudi tena

5. Usipende kuwaangalia wenzio usoni muda wa kula wewe macho yako elekeza kwenye chakula, sababu utaanza kumjaji mwenzio sahani yake imejaa, mara ameweka nyama nyingi nk

aseee mm nachukia sana mtu kula kama mbwa na kujilamba hadi vidole tena kama mwanaume asee ndo nakushusha thaman kabsa...mshua wang yeye kula huku unamwangalia usoni wakati uko mezani anakurushia kijiko.
 
15. Kama utakuwa ukitumia uma na kisu kwa wakati mmoja uma hushikwa na mkono wa kushoto na kisu kiwe mkono wa kulia
16. Angalau mda wa dak 25-30 upite katika kutofautisha aina za vyakula ambavyo huliwa/kunywa vikiwa aidha vya moto au baridi.

Hii iko applicable pia sisi left handed?
 
Koma!!!

Ila kwa sababu mtani usikome.

Table manners zetu zinaendana na mazingira yetu, kutupika kwa knife and fork ni kutuchosha tu.

Kuna watu wanatafuna kama mchwa, inakera sana.
hapa ni ngumu kwa watani wangu wasukuma wako ovyo sana mezani
 
Hivi ni chache nazovikumbuka tuongeze mingine

1. Tafuna ukiwa umefunga mdomo

2. Usiongee ukiwa na chakula mdomoni

3. Usipitishe mkono/mikono juu ya chakula cha mwingine.

4. Usiongeze chumvi au pilipili kabla hujaonja chakula

5. Unapokunywa supu kijiko cha supu hakitakiwi kuingizwa mdomoni, supu hunywewa toka kona ya kijiko.

===================================================================================

Huku kwetu uswahilini chakula kinawekwa kwenye sahani/sinia moja na mboga kwenye bakuli moja Twende kazi hakuna kujisevia asiye kuwepo siku imepita hiyo.
 
Usigonge gonge kijiko kwenye sahani..

usichague chague chakula mfano nyama/andazi kutafuta kubwa kwenye hotpot!

Usiondoke mezani kabla wengine hawajamaliza kula especially your hosts

shukuru ukimaliza kula
 
Mie kuchovya mkate kwenye chai, kutia maandazi kwenye kikombe cha chai au kuchovya biskuti kwenye chai siachiii! Hata msemeje! ILA nikienda kwa watu ntaacha, ofcn na home siachi!


ILA Kuna muungwana alinitembelea sijui bia zilizidi? Kumaliza kula akasukutua maji ya bomba kwenye sinki la kunawia mikono na kutema hapo hapo. Kidogo nizimie. Baada ya mlo usafi WA vim ulifuatia.

cc The Boss
7.

13. Usisukutue maji mdomoni kabla hujameza

14. usichovye mkate kwenye chai unless una miaka minne
 
Last edited by a moderator:
1)Ukikohoa unaholea pembeni na unaweka mkono

2)Ukila ni vidole tu vinachafuka katikati na kijanja safiii

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Hizo za kizungu banaa, toa za kiafrika mfano:
1. Usile bila kunawa mikono
2. Tonge la ugali marufuku kutengeneza semi-tela (dabo tonge)
3. Ukisha ng'ata ugali marufuku kuurudisha tena kwenye bakuli ya mboga
4. Sahani ya baba/kiti cha baba hakitumiwi na mwingine hata iweje labda awe ametangulia
5. Kujamba, kutoa kasoro chakula mkiwa mezani mwiko.

Sasa nyie mnaleta stori za wazungu, utakulaje mrenda na uma, kande kwa kuunga mayonanaiza
 
aseee mm nachukia sana mtu kula kama mbwa na kujilamba hadi vidole tena kama mwanaume asee ndo nakushusha thaman kabsa...mshua wang yeye kula huku unamwangalia usoni wakati uko mezani anakurushia kijiko.

Te te tee kama ungekuwa bara hili huku 96% wanajiramba vidole, yaani ndio culture yao. Wanasema their food is always yummiest in the world
 
Usishike nywele au pua wakati wa kula...

Usipenge wakati wa kula au wakati wenzako wako mezani

te te tee


hizi theory tuuuu....

siku hizi watu wanakula huku wako kwenye computer....mwingine rum mwinge dinning mwingine sebuleni anaangalia TV...
 
ivi kuongea na simu au kuchat sms sio table manner enheee? maana mie simu imeunganishwa na kiganja uwa haibanduki
 
15. Kama utakuwa ukitumia uma na kisu kwa wakati mmoja uma hushikwa na mkono wa kushoto na kisu kiwe mkono wa kulia
16. Angalau mda wa dak 25-30 upite katika kutofautisha aina za vyakula ambavyo huliwa/kunywa vikiwa aidha vya moto au baridi.

eti mi nnavyojua kisu kishikwe mkono ulio strong lets say we ni mashoto mkono strong ni kushoto kamata kisu na mkono wa kushoto
 
Back
Top Bottom