Tabia ya watu kupewa majina ya vyakula

Tabia ya watu kupewa majina ya vyakula

Mr. Mangi

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2014
Posts
1,512
Reaction score
771
Hii tabia ya watu kupewa haya majina imekuwa ikibeba historia zao ila mi yamekuwa yakinishangaza na kunifurahisha pia mfano hapa kwetu kuna jamaa anaitwa "machapati" huyu jamaa asubuhi tu anauwezo wa kula chapati kama kumi+ na maharage ya kutosha. Kuna mwingine anaitwa "uji" huyu alikuwa na tabia ya kunyang'anya uji watoto waliokuwa wakitumwa kupeleka hospitali. Kuna kiongoz wa dini kapewa jina ya "majogoo" huyu ana tabia ya kupenda kupewa zawad ya jogoo pind anapotembelea familia flan. Mwingine anaitwa "Ali maukoko" huyu ktk sherehe anahakikisha kala wali wa kutosha na kusubiria sufuria kuoshwa ale ukoko. Vp wewe umesikia yap na historia zake
 
kuna dada mmoja nilikua nakaa nae Jiran anaitwa "EMMY VIGULU" yn alikua anapenda kula MIGUU YA KUKU ILE INAUZWA USWAZI KWENYE SINIA na yeye alivoo ana vigoko kama miguu ya kuku bac ndio ikawa jina lake hiloo..
 
kuna dada mmoja nilikua nakaa nae Jiran anaitwa "EMMY VIGULU" yn alikua anapenda kula MIGUU YA KUKU ILE INAUZWA USWAZI KWENYE SINIA na yeye alivoo ana vigoko kama miguu ya kuku bac ndio ikawa jina lake hiloo..

duh! Huyo ni noma
 
Ahahhaa usinikumbushe kuna jamaaa tulkua tunamuitaaa iddy manyiguuu ahaha yaan iddy maukoko
 
hapa kwetu kuna jamaa anaitwa 'Domokande' huyu anapenda sana kula kande badala ya kazi!
 
Umenikumbusha shemeji yangu anaitwa Grace Kitalolo.
 
kuna jamaa m1 jiran ye2 hapa anaitwa matonge, yaan huyu bwana wakati wa kula anatabia ya kumega matonge makubwa km ubuyu
 
kuna jamaa m1 jiran ye2 hapa anaitwa matonge, yaan huyu bwana wakati wa kula anatabia ya kumega matonge makubwa km ubuyu
haa ha ha ha dah!
hapa kwetu kuna mmoja anaitwa Ima tonge huyu ilitokea akapigana na mwenzie wakat wa kula cha ajab walipoamuliwa japo alikuwa kapigwa vibaya bado alikuwa na tonge la ugali mkononi
 
Hii tabia ya watu kupewa haya majina imekuwa ikibeba historia zao ila mi yamekuwa yakinishangaza na kunifurahisha pia mfano hapa kwetu kuna jamaa anaitwa "machapati" huyu jamaa asubuhi tu anauwezo wa kula chapati kama kumi+ na maharage ya kutosha. Kuna mwingine anaitwa "uji" huyu alikuwa na tabia ya kunyang'anya uji watoto waliokuwa wakitumwa kupeleka hospitali. Kuna kiongoz wa dini kapewa jina ya "majogoo" huyu ana tabia ya kupenda kupewa zawad ya jogoo pind anapotembelea familia flan. Mwingine anaitwa "Ali maukoko" huyu ktk sherehe anahakikisha kala wali wa kutosha na kusubiria sufuria kuoshwa ale ukoko. Vp wewe umesikia yap na historia zake

Mie kwa jina jengine naitwa JIKO LA SHAMBA HALICHAGUI KUNI
 
Da mmenkumbusha jama angua anaitwa pombe maji
Akishika hta bapa ya konyagi anaigida kama maji

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom