habari zenu wapendwa!
jamani mie nimeletewa hili jambo na mdogo angu wa damu kabisa akiniomba ushauri na kwa kweli nimeona nije kwenu mnisaidie tumshauri cha kufanya kutokana na yeye kukata tamaa na kufikiria kuondoka kwenye ndoa yake.
Ameolewa miaka 3 iliyopita na ana mtoto mmoja.
Kwa muda mrefu tabia za mume wake zimekuwa zinamkosesha raha sana na kumfanya ajute kuolewa ingawa Ndoa ni baraka kutoka kwa Mungu.kwanza anasema kuna mengi sana anayofanyiwa na mume lakini hili kalinyooshea mikono,Mwanaume anaweza kununa hata wiki nzima bila kuongea ndani,akitoka kazini mwanamke atapika,atamuandalia maji ya kuoga,atakula na ataangalia TV huku kanuna ,akienda kitandani basi ndio kulala pembeni kabisa ya kitanda,ikitokea ukamgusa hata kwa bahati mbaya ntakavyosukumwa daah..
Alishajaribu sana kumuuliza mwenzie kama kuna tatizo na husema hakuna,akamwambia basi kama hakuna tatizo kwa nini awe hivyo mpaka mwanamke anakosa raha na amani moyoni?alimweleza kuwa tabia hiyo huwa inamkwaza na kujiona labda mwenzie hampendi tena na anamuona kero pale nyumbani,hapo Mwanaume anabadilika kwa muda na kuwa wa kawaida na baada ya muda mfupi hali ni ileile inajirudi.
Ukienda hata upande wa kufanya tendo la ndoa ni mpaka mwanaume aamue yeye,ameshamchunguza sana kama ana mwanamke mwingine lakini kwa asilimia 100 hana mtu.
kwanza anasema hakumbuki mara ya mwisho mwanaume amemkiss ni lini,amekuwa anamiss vitu vingi sana kutoka kwa mumewe lakini asilimia kubwa ya mume ni mkali na busy,anatamani hata wale sahani moja huku wanaongea lakini hataki.
Ikitokea mtoto akalia hata kidogo mume anamfokea mwanamke hata mbele za wageni..na pia hajali ni wakwe wala shemeji.
Na anachoshangaa nyumba anahudumia vizuri kwa chakula ingawa kikiisha mama huwa ana kazi ya ziada kujieleza katumiajetumiaje mafuta yakaisha na hii kumpelekea hata vikiisha kutoomba tena kwa hofu.
Ameshamsihi sana kuhusu hiyo tabia lakini mabadiliko yameshindikana ,kamwambia kama kamkosea ni bora akamwambia kwani yeye si malaika,lakini anasema hapana,amejaribu kutafuta detail za kazini kwake kama kuna tatizo lakini hakuna lolote na mara nyingi kununa huku hukufanyia nyumbani tuu.Nyumbani kwao na mume haoni wa kumuomba ushauri kwani wako familia ya Mama yake,dada yake na yeye wa mwisho kuzaliwa,Wote hao mara nyingi wana matendo ya kuwasiliana na mumewe kwa chinichini wakieleza shida zao na hawataki yeye ajue iwapo anawatumia fedha,huku hilo nalo linamsononesha kwa kuona mama mkwe labda anamuhisi yeye kuwa anaweza kumkataza mtoto ake asimsaidie,anatamani mama mkwe angekuwa huru kwake basi angeomba ushauri.
Kwakweli mie mwenyewe aliponisimulia mwili umesisimka na kuogopa nimtie moyo kwa neno lipi,Samahani kwa maneno mengi na kama ntakuwa nimechanganya maelezo mnisamehe...Karibuni tusaidiane kuokoa taasisi yetu ya ndoa.
Mbarikiwe sana kwa Michango mtakayotoa.
jamani mie nimeletewa hili jambo na mdogo angu wa damu kabisa akiniomba ushauri na kwa kweli nimeona nije kwenu mnisaidie tumshauri cha kufanya kutokana na yeye kukata tamaa na kufikiria kuondoka kwenye ndoa yake.
Ameolewa miaka 3 iliyopita na ana mtoto mmoja.
Kwa muda mrefu tabia za mume wake zimekuwa zinamkosesha raha sana na kumfanya ajute kuolewa ingawa Ndoa ni baraka kutoka kwa Mungu.kwanza anasema kuna mengi sana anayofanyiwa na mume lakini hili kalinyooshea mikono,Mwanaume anaweza kununa hata wiki nzima bila kuongea ndani,akitoka kazini mwanamke atapika,atamuandalia maji ya kuoga,atakula na ataangalia TV huku kanuna ,akienda kitandani basi ndio kulala pembeni kabisa ya kitanda,ikitokea ukamgusa hata kwa bahati mbaya ntakavyosukumwa daah..
Alishajaribu sana kumuuliza mwenzie kama kuna tatizo na husema hakuna,akamwambia basi kama hakuna tatizo kwa nini awe hivyo mpaka mwanamke anakosa raha na amani moyoni?alimweleza kuwa tabia hiyo huwa inamkwaza na kujiona labda mwenzie hampendi tena na anamuona kero pale nyumbani,hapo Mwanaume anabadilika kwa muda na kuwa wa kawaida na baada ya muda mfupi hali ni ileile inajirudi.
Ukienda hata upande wa kufanya tendo la ndoa ni mpaka mwanaume aamue yeye,ameshamchunguza sana kama ana mwanamke mwingine lakini kwa asilimia 100 hana mtu.
kwanza anasema hakumbuki mara ya mwisho mwanaume amemkiss ni lini,amekuwa anamiss vitu vingi sana kutoka kwa mumewe lakini asilimia kubwa ya mume ni mkali na busy,anatamani hata wale sahani moja huku wanaongea lakini hataki.
Ikitokea mtoto akalia hata kidogo mume anamfokea mwanamke hata mbele za wageni..na pia hajali ni wakwe wala shemeji.
Na anachoshangaa nyumba anahudumia vizuri kwa chakula ingawa kikiisha mama huwa ana kazi ya ziada kujieleza katumiajetumiaje mafuta yakaisha na hii kumpelekea hata vikiisha kutoomba tena kwa hofu.
Ameshamsihi sana kuhusu hiyo tabia lakini mabadiliko yameshindikana ,kamwambia kama kamkosea ni bora akamwambia kwani yeye si malaika,lakini anasema hapana,amejaribu kutafuta detail za kazini kwake kama kuna tatizo lakini hakuna lolote na mara nyingi kununa huku hukufanyia nyumbani tuu.Nyumbani kwao na mume haoni wa kumuomba ushauri kwani wako familia ya Mama yake,dada yake na yeye wa mwisho kuzaliwa,Wote hao mara nyingi wana matendo ya kuwasiliana na mumewe kwa chinichini wakieleza shida zao na hawataki yeye ajue iwapo anawatumia fedha,huku hilo nalo linamsononesha kwa kuona mama mkwe labda anamuhisi yeye kuwa anaweza kumkataza mtoto ake asimsaidie,anatamani mama mkwe angekuwa huru kwake basi angeomba ushauri.
Kwakweli mie mwenyewe aliponisimulia mwili umesisimka na kuogopa nimtie moyo kwa neno lipi,Samahani kwa maneno mengi na kama ntakuwa nimechanganya maelezo mnisamehe...Karibuni tusaidiane kuokoa taasisi yetu ya ndoa.
Mbarikiwe sana kwa Michango mtakayotoa.