Tabia hii ya mke wangu inaashiria nini?

Tabia hii ya mke wangu inaashiria nini?

Kati ya tabia nisizozipenda kwa mwanaume ni kususa susa na kujinunisha nunisha..Watoto wanune nawe jitu zima unune aaah!!!!
 
Duh wanaume tumebakia wachache, tuliobakia kuna dalili tukaitwa nyara za taifa. Mtoto wa kiume unazila na kumsusa mkeo????

Wanaume kama mabinti, asante Lady jaydee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo anakuoenda sana.....tena zaidi ya sana

Sent using i phone x
 
Kiongozi una bahati ya mtende lkn hujitambui. Mkeo ana busara Sana lkn Wewe wenyewe unataka kuleta dhahma katika ndoa yako. Sawa kuudhiana kupo lkn Wewe kama mwanaume usinuneee nune kamanda mwambie kosa Lake halafu mkanye endelea na maisha mengine. Kwa taarifa yako mwanamke akichoka tabia yako akapata mtu wa kumliwaza utarudi hapa unalia kilio cha samaki. Mpende na kumjali mkeo hasa wakati huu anaponyonyesha.
 
Inaonekana wewe ulidekezwa na wazazi wako,Ipo siku mkeo atachoka kukuvumilia na atakua sugu.Ukisusa yeye atakula chote,kikibaki atawapa kuku wala hatakuuliza, atakua busy na simu yake.Ukimtenga kitandani atasinzia kwa raha zake,utalala sebuleni mwenyewe wala hatakusemesha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi ni kijana ambaye niko kwenye ndoa naelekea mwaka wa pili sasa. Kama kawaida kwenye ndoa kuna milima na mabonde ya kupitia, na pia kwenye ndoa kuna Raha na karaha. Ila kwa Mke wangu kila anaponikwaza adhabu ambayo inamtesa nikimpa ni kususia chakula,na kumtenga kitandani yaani adhabu hizi huwa zinampa sana Tabu adhabu hii. Alishawahi kuniambia kwamba hata kama unakasirika ila kula chakula changu halafu endelea kununa, kuna siku aliniudhi usiku nikamtenga kitanda nilichukua mkeka nikatandika sebuleni, kuja kusituka usiku wa manane namuona pembeni yangu kalala ikabidi nimuamshe tukalale kitandani. Sasa leo ameniuzi tokea asubuhi sijala na yeye pia tokea asubuhi mpaka jioni ya leo hajakula kitu na ananyonyesha. Je tabia hii ya mke wangu inaashiria nini?

Sent using Jamii Forums mobile app

Una homoni za kike kike kwasababu mwanaume aliyekamilika hana tabia hizo.acha utoto
 
Nimecheka kifala,sasa mbona wewe kama una Tabia za kike mkuu, yani bora hata huyo mkeo anaonekana shupavu, yani unasusa kula lol!!
Nakuhakikishia wewe bado ni mvulana kama unabisha ebu ahirisha kususa ndani ya mwezi tu utakuwa Gent.
Na usiombe atokee dume mwingine aanze kumuonja mkeo alaaaa, utasuswa kibabe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi ni kijana ambaye niko kwenye ndoa naelekea mwaka wa pili sasa. Kama kawaida kwenye ndoa kuna milima na mabonde ya kupitia, na pia kwenye ndoa kuna Raha na karaha. Ila kwa Mke wangu kila anaponikwaza adhabu ambayo inamtesa nikimpa ni kususia chakula,na kumtenga kitandani yaani adhabu hizi huwa zinampa sana Tabu adhabu hii. Alishawahi kuniambia kwamba hata kama unakasirika ila kula chakula changu halafu endelea kununa, kuna siku aliniudhi usiku nikamtenga kitanda nilichukua mkeka nikatandika sebuleni, kuja kusituka usiku wa manane namuona pembeni yangu kalala ikabidi nimuamshe tukalale kitandani. Sasa leo ameniuzi tokea asubuhi sijala na yeye pia tokea asubuhi mpaka jioni ya leo hajakula kitu na ananyonyesha. Je tabia hii ya mke wangu inaashiria nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
wee jamaa una matatizo, mtoto wa kiume haupaswi kununa hivyo. afu mwanamke ananyonyesha lazima anachangamoto nyingi sana.

mvumilie kipindi hiki kigumu kwake, kwanza lazima atakuwa anakuhisi unapiga nje kulingana na hali yake jiongeze

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dume zima kweli unasusa kula huku umebinua mdomo kama bashite,kweli wanaume wa dar mna shehena ya vituko,sijui hiyo tabia ya kususa umeirithi kwa dingi yako
 
Likely anaupendo sana na wewe. Unfortunately by doing what you're doing to her indicates that you are not MAN ENOUGH, UNMATURED, & CHILDISH kind of a person. On top of that unaonekana una GUBU which is a very bad attitude/character to be shown by a MAN. You need to change and act bravely.
 
Back
Top Bottom