Tabia hii ya mke wangu inaashiria nini?

Tabia hii ya mke wangu inaashiria nini?

Mimi ni kijana ambaye niko kwenye ndoa naelekea mwaka wa pili sasa. Kama kawaida kwenye ndoa kuna milima na mabonde ya kupitia, na pia kwenye ndoa kuna Raha na karaha. Ila kwa Mke wangu kila anaponikwaza adhabu ambayo inamtesa nikimpa ni kususia chakula,na kumtenga kitandani yaani adhabu hizi huwa zinampa sana Tabu adhabu hii. Alishawahi kuniambia kwamba hata kama unakasirika ila kula chakula changu halafu endelea kununa, kuna siku aliniudhi usiku nikamtenga kitanda nilichukua mkeka nikatandika sebuleni, kuja kusituka usiku wa manane namuona pembeni yangu kalala ikabidi nimuamshe tukalale kitandani. Sasa leo ameniuzi tokea asubuhi sijala na yeye pia tokea asubuhi mpaka jioni ya leo hajakula kitu na ananyonyesha. Je tabia hii ya mke wangu inaashiria nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
Chai hizi kama sio chai bas unaakili za kitoto

Ila bado siku 4 shule zifunguliwe tutavumilia tu
 
Ni na amin kuwa wanaume ni viumbe ambao wapo mbioni kuto weka kwenye huu uso wa Dunia

We mwanaume kabisa na ndevu zako nyingi tuu una Anza kususa kula?

Una kimbia kitanda kisa mkeo kakukera?

We jamaa wewe jiangalie Sana
Moja Kati ya udhaifu mkubwa kwa mke wako ni huo unatakiwa..

Usimame kama mwanaume sio mume

Unajua kuwa wewe ndio kichwa cha Familia? Sasa mbona wee unakuwa mkia badala ya kichwa?

Badilika kaka simama kiume izo sio adhabu bora ukae kimya tuu ila mambo mengine fanya kama Kawa show piga msosi piga ukiweza Ata upike mwenyewe kabisa

Ume ni elewa sijuh?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwanza baba wa familia unafanya nn asubui paka jioni nyumbani.. uskute umehamishia ugomvi na housegirl mnagombania rimoti ya tv!


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Dah nimecheka sana broo kwanini ulikimbilia kuowa unaisi utamuowa mkamilifu raha ya kukosea ni kuelezana ukweli na kumkanya kumbuka makosa mkiwa mnaishi pamoja hayaishi kwaiyo kukanyana, kukumbushana, na kusamehana ndyo njiya ya kuzidi kutete ndoa yenu

Sent using Jamii Forums mobile app
Umetoa ushauri mzuri, shida ipo kwenye huu mcharazo wako [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] baba uandishi huu daaah!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: RTI
Uzuri wa JF, kila mtu Nyuma ya keyboard ana busara

Goite
 
Kwakifupi hayo ndio mahaba. Raha ya ndoa ndio vitu kama hivyo mnafanyiana utoto huku mnajaliana......

Kama hapo umesusa, umelala sebuleni, amekufuata mkaamshana mkaja kulala hadi asubuhi.

Mradi tu usipige mtoto wa watu wala usimfyatukie au kuwa mkali. Fanya mbwembwe za namna hiyo huku na yeye akikubembeleza na wewe akikununia unambembeleza pia.... Hayo ndio mahaba.

Sent using Jamii Forums mobile app
Atauwa mama na mtoto we mshauri vibaya tu.... Mtu amesema mke ananyonyesha na hajala chakula kisa mume kasusa unategemea nini kitazaliwa hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona hiyo inaashiria wewe ndio una matatizo zaidi yake
 
Wewe jamaa ulitakiwa ukae miaka 20 mbele ndiyo uoe kwasababu bado unaakili za kivulana. Unasusia chakula na haulali na mkeo. Shukuru umepata mke mzuri ila watu wakijajua thamani ya mkeo watambeba na kumuoa na utamkumbuka sana. Ningekuwa karibu nikupiga ngumi ya mdomo
Mimi ni kijana ambaye niko kwenye ndoa naelekea mwaka wa pili sasa. Kama kawaida kwenye ndoa kuna milima na mabonde ya kupitia, na pia kwenye ndoa kuna Raha na karaha. Ila kwa Mke wangu kila anaponikwaza adhabu ambayo inamtesa nikimpa ni kususia chakula,na kumtenga kitandani yaani adhabu hizi huwa zinampa sana Tabu adhabu hii. Alishawahi kuniambia kwamba hata kama unakasirika ila kula chakula changu halafu endelea kununa, kuna siku aliniudhi usiku nikamtenga kitanda nilichukua mkeka nikatandika sebuleni, kuja kusituka usiku wa manane namuona pembeni yangu kalala ikabidi nimuamshe tukalale kitandani. Sasa leo ameniuzi tokea asubuhi sijala na yeye pia tokea asubuhi mpaka jioni ya leo hajakula kitu na ananyonyesha. Je tabia hii ya mke wangu inaashiria nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimpate mke kama huyo nitamlinda mpaka mwenyewe achanganyikiwe kuwepo duniani. Kumpata mke mwenye upendo wa hivyo dunia ya leo. Una bahati sana. Sasa kwa sababu umeuliza,dawa ni ndogo tu. Badirika kidogo tu,kwanza punguza hasira,pili jitahidi sana kila unapoona umekwazwa ksbb wewe ndio kichwa cha nyumba,mwite mke wako jadirini pamoja bila jaziba.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom