Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,096
- 828,939
Ni mara chache mno kukuta bosi na msaidizi wake wakipendana na kuwa marafiki..wengi hawapendani kabisa..! Ukikuta hao wawili ni washikaji basi tambua kuna mambo yanayowaunganisha, Ama mmoja ni superior kuliko mwingine na mwingine hana kinyongo
Mabosi wengi muda mwingi hawawaamini wasaidizi wao wakuu wakiamini kuwa wanawapangia mbinu za kuwapokonya kiti... Wasaidizi wengi hawawapendi mabosi zao wakiamini kuwa wao ni bora zaidi na hupenda kuwasimanga kila wanapopata nafasi
Matamanio kaumbiwa mwanadamu.. Daima hutaka zaidi na hapati vyote mpaka kifo.. Madaraka ni matamu hasa madaraka ya kisiasa yasiyohitaji ujuzi wa kusomea darasani! Kwa kila nafasi unayopanda unatamani na ya juu zaidi na aliyeko hapo unatamani umpopoe mawe aanguke ukae wewe
Kufa ni kufaana ndio maana kuna urithi na mirathi, kugawana vya marehemu na vingine kurithishana.. Mali hata ukuu.. Si wote waliao misibani ni vilio vya majonzi na huzuni.. Wengine ni machozi ya mamba na vilio vya furaha!
Kwa makasiriko haya.. Kwa magumu haya.. Tulitegemea kuona wale tulio pamoja walau tukipeana neno la faraja.. Lakini aah wapi tuko busy tukijipanga na kuomba sana ili litokee la kutokea lile linalotupa matamanio ya kila siku... Mimi ndio nafaa kukaa pale...!
Maono ni mengi lakini machache hubeba unabii
www.jamiiforums.com
Mabosi wengi muda mwingi hawawaamini wasaidizi wao wakuu wakiamini kuwa wanawapangia mbinu za kuwapokonya kiti... Wasaidizi wengi hawawapendi mabosi zao wakiamini kuwa wao ni bora zaidi na hupenda kuwasimanga kila wanapopata nafasi
Matamanio kaumbiwa mwanadamu.. Daima hutaka zaidi na hapati vyote mpaka kifo.. Madaraka ni matamu hasa madaraka ya kisiasa yasiyohitaji ujuzi wa kusomea darasani! Kwa kila nafasi unayopanda unatamani na ya juu zaidi na aliyeko hapo unatamani umpopoe mawe aanguke ukae wewe
Kufa ni kufaana ndio maana kuna urithi na mirathi, kugawana vya marehemu na vingine kurithishana.. Mali hata ukuu.. Si wote waliao misibani ni vilio vya majonzi na huzuni.. Wengine ni machozi ya mamba na vilio vya furaha!
Kwa makasiriko haya.. Kwa magumu haya.. Tulitegemea kuona wale tulio pamoja walau tukipeana neno la faraja.. Lakini aah wapi tuko busy tukijipanga na kuomba sana ili litokee la kutokea lile linalotupa matamanio ya kila siku... Mimi ndio nafaa kukaa pale...!
Maono ni mengi lakini machache hubeba unabii
Job Ndugai bado una nafasi ya kutubu na kujirudi
Muda unakwenda kasi na hausubiri mtu...! Mapito ya maisha yana simulizi nyingi za kuogofya sana na za kufurahisha sana.. Halafu kuna za kuhuzusha sana! Hizi hutia na kuleta simanzi, majonzi na kuumia roho..! Daima ukiwa mtu wa haki utatenda kwa weledi, utatenda kwa tafakuri kwakuwa maisha ni...