Taasisi ya Urais iheshimiwe

Taasisi ya Urais iheshimiwe

Nadhani hapa Tulipofika watanzania tunahitaji zaidi Viongozi wanaotuunganisha badala ya kuwa na viongozi wanaotugawa kwa kauli zao. Pande zote hivi sasa zina matatizo ya matamshi toka kwa viongozi hasa wa ngazi za juu. sasa sijui nani amfunge 'paka' kengele. Ushabiki unaofanywa na wale wanaojiita UVCCM na BAVICHA dhidi ya kauli ovu zinazotolewa na viongozi wao dhidi ya wengine ni kielelezo tosha kuwa jamii imepotoka hivyo tunahitaji wa kuturudisha kwenye Mstari. Wale ambao wenye uwezo wa kuwaambia viongozi wetu hapa unakosea mzee hawapo maana nguzo yetu imeliwa na mchwa nayo ilikuwa Baba wa taifa pekee. Tumlilie nani?

....angekuwepo hai mngekuwa mnamtukana...waswahili unafiki mmezaliwa nao............
 
....angekuwepo hai mngekuwa mnamtukana...waswahili unafiki mmezaliwa nao............
Nadhani wewe umeathirika na virusi vya uchama. Unfortunaltely mimi sio miongoni mwa wale wanoamini katika chama chochote mimi ni mzalendo tu na hata ukiangalia post zangu tangu juu huoni bias yoyote. Kama wewe ni BAVICHA au UVCCM basi siasa hazijakusaidia badala yake zimekuharibu. Tena mimi ni Muumini mzuri sana wa falsafa ya Mwalimu Nyerere. Nina zaidi ya nusu ya machapisho yake ambayo yanafundisha mengi kwenye jamii. Si dhani kama wewe hata kama unasoma chochote cha kukupanua mawazo yako zaidi ya post za kwenye JF .Nadhani wewe ndiyo unastahili kuitwa MNAFIKI badala yangu kwani unachoamini na kukitetea ni unafiki mkubwa. Sikutegemea kama JF kuna watu wenye mapungufu upstairs kama wewe
 
Ng'ombe wa ccm bana, acha ung'ombe wewee, hii nchi siyo ya rais ni ya watanzania na hakuna aliye juu ya sheria rais akiongea upupu inabidi aambiwe kaongea upupu..
 
Katiba iheshimiwe katiba ndio kila kitu washaurini viongozi Na wananchi wafuate katiba hilo la ni dogo sana muhimu katiba ya nchi iheshimiwe hasa Na viongozi wote walioko madarakani
 
Frey Cosseny, Kila mtu anastahili heshima bila kujali ana wadhifa gani. Heshima haipatikani kwa mabavu kejeli na vitisho.
Mimi hapo ndo huwa nashangaa mtu kulazimisha aheshimiwe. Kama yeye hajiheshimu usitegemee ataheshimika. Hata kama wakija na vitisho vya aina gani, bado watu wataendelea kusema. Lugha anazotumia hazina staha kabisa. Ndo maana watu hawamheshimu. After all yeye siyo the supreme omniponent and benevolent. He is a human being with a lot of weaknesses that why most of his speeches are pure malarkey.
 
Soma kalete
Tafadhali uende Ikulu ukamfundishe haya:
(1) Every person is entitled to freedom, subject to the laws of the land, to freely and peaceably assemble, associate and cooperate with other persons, express views Publicly, and more specially to form or join associations or organisations formed for the purposes of preserving of Person's freedom of association Act No. 15 of 1984 s.6 furthering his beliefs or interests or any other interests
 
Tafadhali uende Ikulu ukamfundishe haya:
(1) Every person is entitled to freedom, subject to the laws of the land, to freely and peaceably assemble, associate and cooperate with other persons, express views Publicly, and more specially to form or join associations or organisations formed for the purposes of preserving of Person's freedom of association Act No. 15 of 1984 s.6 furthering his beliefs or interests or any other interests
MIMI MAIMUNA
 
Kuna jambo linakera sana mtandaoni kuona MTU kwa makusudi anaamua kumtusi Mh Rais Dr john pombe Joseph Magufuli tena anamdhalilisha kwa kumuita majina ya ajabu ajabu mi nadhani ifike wakati waheshimu taasisi ya urais km hawataki kuheshimu taasisi hiyo vyombo vilivyoundwa maalum kwa kazi hiyo kama TISS, Polisi na JWTZ iwashurutishe kwa nguvu kutii taasisi ya urais.

Nasema hivi kwasababu nimesoma maandiko aliyoandika mtu anayeitwa Ben Sanane na nimewaambia ni mfanyakazi wa cdm makao makuu km mkuu wa kitengo cha utafiti na mtu wa karibu sn na Mh Mbowe kiukweli machapisho yake ya Jana naleo mtandaoni inapasa kabisa kumfikisha ktk vyombo vya usalama hasa kile chombo kilichopewa mamlaka kulinda taasisi ya Urais. Tukiacha watu kuchezea taasisi ya urais kuna hatari kubwa taasisi hiyo kutoheshimika milele. Watanzania pamoja na demokrasia ya vyama Vingi kuanzishwa nchini lkn hiyo haitoi nafasi kwa kutusi Mh Rais.

Nimeamua kuandika kwa uchungu kwasababu haya yote yanafanyika wakuu wa wilaya wapo mdogo wangu Ally Salum Hapi DC kinondoni yupo kimya mh rais anadhalilishwa wilayani kwake hajachukua hatua, mkuu wa Mkoa Mh Paul Makonda yuko kimya wakati majeshi yote ya kulida taasisi ya Urais wanayo, cjui wanasubiri mpk Mwigulu Nchemba Waziri wa mambo ya ndani au naibu wake Hamad Masauni ndiyo wachukue hatua?

Jamani ninyi viongozi mliyopewa mamlaka mkishindwa tuachieni sisi vijana wa CCM tufanye kazi hiyo hatuta kubali kuona Rais wetu anadhalilishwa . Muda sasa umefika wa kusema no no no.

Tunataka kuona hatua zikichukuliwa haraka iwezekanavyo
Respect is a double edged sword! Huwezi sema taasisi ya urais iheshimike wakati yenyewe haiheshimu watu, hiyo taasisi ndio bingwa wa uchochezi! Ukiheshimu utaheshimiwa otherwise dawa ya moto ni moto
 
Ben inawezekana una malezi ya kilevi na inawezekana unaandika umelewa lkn ujue taasisi ya Urais ina hadhi yake na inalindwa kisheria Mimi nimewaambia wasipotaka kuulinda hadhi ya taasisi Ya urais kama hawatafanya ivyo sisi wanaccm tutafanya ivyo. Bahati nzuri nishafanya utafiti nakuwafahamuvwalinzi wenu wote na CV yao.
Hah ccm bana, yaani wewe ndo mwenye malezi ya ulevi unamsingizia mwenzio... Taasisi ya urais taasisi ya urais,,,
 
Tatizo kuna watu hawawezi kutofautisha rais na m/kiti wa chama, labda kwa vile vyeo hivi vinashikiliwa na mtu mmoja. Mtoa post unaposema nyie UVCCM mtachukua hatua unamaanisha hatua za kisheria za kulinda taasisi ya urais au hatua za kisisasa za kumlinda m/kiti wenu?
 
Yan ukiamka asbh na kitu cha kwanza ukaona picha ya Magufuli basi ujue siku hiyo itakuwa na NUKSI mwanzo mwisho!
 
Ben inawezekana una malezi ya kilevi na inawezekana unaandika umelewa lkn ujue taasisi ya Urais ina hadhi yake na inalindwa kisheria Mimi nimewaambia wasipotaka kuulinda hadhi ya taasisi Ya urais kama hawatafanya ivyo sisi wanaccm tutafanya ivyo. Bahati nzuri nishafanya utafiti nakuwafahamuvwalinzi wenu wote na CV yao.
Tasisi ya urais inaitwaje kwa jina rahisi! hivi ukimtaja rais kwa jina lake unakuwa umetaja taasisi! huu msamiati binafsi bado unanichanganya!
 
Weak mbadala....kabla ya taasisi hiyo kuheshimiwa...ianze yenyewe kuwaheshimu wananchi waliyoiweka hapo ilipo..namaaanisha wapiga kura na watanzania wengine wakiwamo wake watoto wa udom waliotimuliwa na kuitwa ****** wanahitaji kuheshimiwa maana ndio walioiweka taasisi ya Urals nchini.
Kwa hiyo unatangaza uasi hadharani si ndio?
 
Mleta mada, elewa kuwa heshima huwa hailazimishwi ina tabia ya kumfuata mtu anayejiheshimu.
 
Unategemea wanaosema ukikuta watu porini ua tuwaheshimu??? Subiri athari ya kauli zao imkute mamako anakata kuni porini ndio utajua kuwa wanakosea.
 
Ben inawezekana una malezi ya kilevi na inawezekana unaandika umelewa lkn ujue taasisi ya Urais ina hadhi yake na inalindwa kisheria Mimi nimewaambia wasipotaka kuulinda hadhi ya taasisi Ya urais kama hawatafanya ivyo sisi wanaccm tutafanya ivyo. Bahati nzuri nishafanya utafiti nakuwafahamuvwalinzi wenu wote na CV yao.
Brother pole sana maana umebeba mzigo mzito rohoni unakuumiza hivi unadhani wote uliowataja kuwa hawachukui hatua unadhani hawaoni? Au in wajinga? Au hapendi Kazi zao? Unasema vijana wa Ccm ulikaa nao wapi mkakubaliana hayo. Kwa ujumla haya ni ya kwako binafsi usiwasemee watu nakushauri nenda ufungue kesi mahakamani tofauti na hapo ni Shida.
 
Unataka kuwafanya watu wengine hawajui maana ya kukosoa na kutukana? Unakosoa kwa kutumia maneno ya kejeli na matusi?
Nyie vijana wa Uvccm acheni ujuha mmeambiwa mlete matusi aliyotukanwa rais hamna hata mmoja anayeleta, sasa mnalialia kitu gani hapa mnataka polisi iwaonee huruma?

Yaani rais asikosolewe yeye ana miaka 5 tu anaondoka, baada ya yeye kuondoka tunataka atuachie Tanzania kama alivyoikuta siyo Tanzania ya vipande vipande.
 
Back
Top Bottom