Zamazamani
JF-Expert Member
- Jun 13, 2008
- 1,903
- 828
Nadhani hapa Tulipofika watanzania tunahitaji zaidi Viongozi wanaotuunganisha badala ya kuwa na viongozi wanaotugawa kwa kauli zao. Pande zote hivi sasa zina matatizo ya matamshi toka kwa viongozi hasa wa ngazi za juu. sasa sijui nani amfunge 'paka' kengele. Ushabiki unaofanywa na wale wanaojiita UVCCM na BAVICHA dhidi ya kauli ovu zinazotolewa na viongozi wao dhidi ya wengine ni kielelezo tosha kuwa jamii imepotoka hivyo tunahitaji wa kuturudisha kwenye Mstari. Wale ambao wenye uwezo wa kuwaambia viongozi wetu hapa unakosea mzee hawapo maana nguzo yetu imeliwa na mchwa nayo ilikuwa Baba wa taifa pekee. Tumlilie nani?
....angekuwepo hai mngekuwa mnamtukana...waswahili unafiki mmezaliwa nao............