Taasisi ya Kigoda cha Mwalimu Nyerere ijitathimini

Taasisi ya Kigoda cha Mwalimu Nyerere ijitathimini

Jamani hawa wazee wana watoto wao na wanatamani sana waje wawe viongozi wa hii nchi, na ili kuwa viongozi wameandaliwa sana wapitie ccm walikopita wao ndio itakuwa rais lakini kikiingia chama kingine itakuwa vigumu wao kupenya maana huko kuna watu wengine kabisa haswa damu mpya kabisa katika uongozi. Ndio maana wanakomaa ccm ibaki ili wawapenyeze watoto wao ila wamebugi kwa hilo
 
Ndo wakina nani hao mbona .me siwafahamu. Ivi wanaushawishi mkubwa hapa nchini zaidi ya watu tunaoitaji mabadariko. Watu tunaitaji mabadiriko . haturudi nyuma.
 
hawa kigoda cha mwalimu si ndo mlikua mnawasifu sana,leo wamekuwa wabaya?,,,kila mtu mnasema mbaya,wariba,lubuva,star tv,itv,cloud etc...
kila mtu akitofautiana na chadema huyo ni mbaya

Mtu yeyote akifanya vzr anapongezwa na akikosea anakosolewa...... Ht mi Leo hii japo magufuli sitampa kura si kwamba sijui mazuri yake.
 
Ukweli siku zote huwa unauma na hasa unapomfika mlengwa moja kwa moja. Na vilevile ukweli huwa haugawanyiki, lazima utegemea upande mmoja.

Tanzania ina watu wengi wanaoitakia mema nchi yetu, na wengine huthubutu hata kutumia muda wao bure kutufahamisha mambo ambayo tunapaswa kuyafannya kwa mustakabali wa nchi yetu.

Wakati wa bunge maalumu la katiba, walijitokeza watu kutueleza ni nmna gani ccm ilivyopora na kuweka kando maoni ya wananchi si watu wa ukawa tu waliokuwa wanafurahia midahalo hiyo bali wa ccm walikuwa wanafurahia. Tulielezwa mambo mengi ambayo mengine sidhani kama tungeyafahamu bila watu hawa kutuelewesha. Tumeambiwa hata madesa mengi kwenye bunge la katiba, akina Mbatia, walikuwa wanayatoa kwa Polepole tena kwa kuwaandikia.

Mambo yaliendelea vizuri wakati wa mchakato wa kumpata mgombea atakaye peperusha bendera ya ccm kwenye urais. Polepole kupitia channel Ten aliweka wazi msimamo wake kuhusu ccm kuchagua mtu ambaye ana tuhuma za rushwa na ufisadi na ambaye kwa wakati ule alisika kila kona kwa dhana ya kukubalika na watu wengi. Lakini Polepole pamoja na uccm wake alisema angezunguka kuwaambia wananchi kama ilivyokuwa kwenye katiba kwamba mtu huyo hafai na asichaguliwe. Hali kadhalika kwa ukawa nako alisema wakimpitisha mtu ambaye hafai nako angefanya hivyohivyo.

CCM pamoja na kukubalika kwake, wakafuata vigezo walivyojiwekea ili kumpata mgombea wa urais, kweli Lowassa akakatwa. Haya maamuzi kwa ccm yaliwakera wanaccm wengi, lakini kwasababu ccm ilitaka kuanza kujisafisha mbele ya wanachama wao na wananchi kwa ujumla ilibidi wafanye haya maamuzi magumu.

Cha ajabu na kushangaza ni kwamba, maneno ya Polepole kumpinga hadharani mgombea ambaye atapitishwa ama na ccm au na ukawa ambaye atakuwa hafai kwa mustakabali wa taifa hili, angempinga hadharani, aliyasema kabla ya michakato ya vyama vyote kupata wagombea wao. Sasa najiuliza, je, alivyotangaza dhamira yake hiyo, ukawa hawakumwelwa? Maana watu walewale walikuwa wanamshangillia Polepole kwenye mambo ya katiba, ndio hao hao wanaomtukana kwenye suala ambalo aliliweka wazi kabla. Maana kama kununuliwa, ni upi upande uliokuwa na pesa wakati wa bunge la katiba, je, ni upande wa wananchi ambao Polepole alikuwa anautetea, au wa ccm ambao walipora maoni ya wananchi na kuyaweka kando? Na kwenye mchakato wa urais, ni nani ambaye alikuwa na uwezo wa kumyamazisha kwa kumnunua, kama sio huyo alivenunua nafasi ya kugombea dakika za mwisho kupitia chadema.

Nadhani kuna haja ya hata vyama kupunguza huu mlolongo wa kuwa na wanachama wengi ambao kwa siasa tulizonazo sasa kazi yao ni kuongeza ushabiki usio na tija na ambao unaweza kutuletea kiongozi asiyefaa kuongoza taifa hili
 
mbona bado mnaomboleza Msiba! huyu jamaa alikatwa na kamati ya maadili kwa kukosa uadilifu full stop! UKAWA Mkampokea na yupo kwenye kampeni ambayo mnaamini anafanya vizuri ingawa hajafikisha kutembelea hata nusu ya majimbo ya uchaguzi! MAGUFULI TUMAINI LETU..... SIO MDINI! SIO MKABILA! ANACHOJUA NI KUKEMEA NA KUCHAPA KAZI TU!

Nasema tu matokeo wengi yatawashangaza.
 
Achana na hao wazee washahidiwa watoto wao kupewa vyeo wanarudi kuipigania CCM. Mfano warioba mtoto wake wamemvalisha kaa la moto kugombea ubunge KAWE ambako hapiti hata kwa dawa. Nilichogundua hawa wazee wanapigania matumbo yao tu walipoachwa kwenye utawala wa JK alikuwa wanaidiss sana ccm Saa hizi watoto wao wameahidiwa vyeo na kupewa nafasi za ubunge wanaikampenia ccm. Aibu sana kuwa na wazee wa Taifa wasiojitambua huu utawala wa kikoo utaisha lini tukatae watanzania kama walivyokataa Arumeru mashariki
 
%60 ya watanzania wamwzaliwa baada ya nyerere kutoka madarakani na kama kama ukifuatlia vizuri hii misimamo ya nyerere foundation watakuja watu na data za kweli juu ya hatamu zote za tanzania iliyoongozwa na nyerere kisha watu watafakari kama hiyo taasisi hawakubaki pekee yao na ubinafsi wao wengine wana watoto au ndugu ambao wanagombea nafasi kupitia ccm, sasa hesabu zao waonekane wanafanya kampeni nzuri ili wapendwa wao waje wapate nafasi za uwaziri ila wanashindwa kuelewa muamko wa wanainchi kwenye uchaguzi huu. Hivyo wapendwa wao wao wana nafasi chini ya % 20 kupata huo ubunge wanaogombea.
Pia kama wanafuatilia mambo yanavyotokea duniani hasa iran %80. Wamezaliwa baada ya mapinduzi, leo kizazi kipya kinahitaji mabadiliko ya kuwa huru kielimu, kusoma, kupiga kura na hata kuwa na haki ya kuperuzi internet bila kufuatiliwa na vyombo vya dola, matokeoa yake wanatumia muda na nguvu nyingi kuzuia mabadiliko ambayo mafuriko yake yanawakumba muda si mrefu source kama ukufuatilia mazungumzo ya nuclear kuhusu iran.
Regards.
 
Achana na hao wazee washahidiwa watoto wao kupewa vyeo wanarudi kuipigania CCM. Mfano warioba mtoto wake wamemvalisha kaa la moto kugombea ubunge KAWE ambako hapiti hata kwa dawa. Nilichogundua hawa wazee wanapigania matumbo yao tu walipoachwa kwenye utawala wa JK alikuwa wanaidiss sana ccm Saa hizi watoto wao wameahidiwa vyeo na kupewa nafasi za ubunge wanaikampenia ccm. Aibu sana kuwa na wazee wa Taifa wasiojitambua huu utawala wa kikoo utaisha lini tukatae watanzania kama walivyokataa Arumeru mashariki

Hivi, kati ya Warioba, Butiku na Lowassa, nani kati yao ambaye hajitambui. Definitely, jibu litakuwa asiye jitambua hapo ni lowassa. Lowassa hana tofauti na kupe aliyemng'ata ng'ombe, ng'ombe akichinjwa kupe hana habari, ng'ombe anachunwa ngozi kupe hana habari, ngozi inaanikwa kupe hana habari, mpaka ngozi ikianza kukauka kupe ndo anashtuka kuwa kumbe ng'ombe kachinjwa.

Ni sawa na lowassa aliambiwa ccm watakukata, akasema hawawezi ccm is ny life na asiyenitaka ccm aondoke yeye, anaambiwa hata huku ulikokimbilia huwezi kuwa rais, anasema watu wanamahaba na yeye. Sasa atakapoona Dr. John Joseph Pombe Magufuli anapigiwa mizinga 21 ndipo atakapogundua kwamba mwenzake kaapishwa
 
Hivi, kati ya Warioba, Butiku na Lowassa, nani kati yao ambaye hajitambui. Definitely, jibu litakuwa asiye jitambua hapo ni lowassa. Lowassa hana tofauti na kupe aliyemng'ata ng'ombe, ng'ombe akichinjwa kupe hana habari, ng'ombe anachunwa ngozi kupe hana habari, ngozi inaanikwa kupe hana habari, mpaka ngozi ikianza kukauka kupe ndo anashtuka kuwa kumbe ng'ombe kachinjwa.

Ni sawa na lowassa aliambiwa ccm watakukata, akasema hawawezi ccm is ny life na asiyenitaka ccm aondoke yeye, anaambiwa hata huku ulikokimbilia huwezi kuwa rais, anasema watu wanamahaba na yeye. Sasa atakapoona Dr. John Joseph Pombe Magufuli anapigiwa mizinga 21 ndipo atakapogundua kwamba mwenzake kaapishwa

Ni ndoto Ni ndoto Ni ndoto! mjiandae kisaikolojia kuwa wapinzani 2015-2020 na bahati nzuri mmeanza mapema kwenye kampeni zenu bahati mbaya Upinzani wenu ni ule ambao hauna tija kwa Taifa maana ninyi ni matusi na kumshambulia mtu mwilini. Badilikeni muwe wapinzani kwa hoja kama za akina Lissu, Mnyika, Kafulila, Mdee na wengineo Taifa linahitaji upinzani imara 2015/20 badilikeni ili kwenye CCM tupate mbadala wa akina Lissu, Mnyika, Kafululia na wengineo. TUKUTANE OCTOBA 25
 
kweli kabisa! Kweli tupu...
NCCR yapoteza majimbo yote Kigoma.... CCM yarudi kwa kishindo Moshi and Arusha..... ACT chama rasmi cha upinzani Bungeni!

Maumivu ya kichwa huanza pole pole
 
nimefuatilia mjadala uliotayarisha na wakina Butikuna akina Polepole nimebaini kwamba kinaweza kusababisha vurugu nchini kwa sababu wanataka kuwaaminisha watanzania kwamba ili nchi iwe na amani ni lazima wananchi waichague CCM tu.

Vinginevyo kama watachagua chama tofauti na CCM nchi itaingia vitani yaani amani kwao ni ccm tu,na yote hii eti kwa sababu chama kama chadema mgombea wake ni Lowasa ambao kwa maoni yao wanaona hafai.

Hivi kweli hii ndio kazi ya hiyo taasisi?[/QUOTE

kama kawaida yetu wa Watanzania hii taasisi ni kama mradi wa kuingizia vijisenti ,kuna nyingine inaitwa sijui Twaweza
 
Back
Top Bottom