Wale mnaosema huu ni wakati wa vijana naomba mfikirie tena.
Kauli za Nape si za kiungwanahata kidogo. Huu ni msiba mkubwa kwa taifa.
Sidhani kuna mtoto anaajua siasa ni nini. Na hata kama anajua kuna ubaya gani yeye kushiriki shughuli za kisiasa kama mtu anayejifunza?
Leo Nape anatumia damu za watoto hao na raia wengine wasio na hatia kutangaza habari za siasa.
Lile bomu lingeangukia na kuua viongozi wa CDM sijui kama angesema limepangwa.
Nape labda tukukmbushe haya
1. Mwakyembe kutaka kuuawa na kutaja hadi wahusika tukio lile lilipangwa na nani?
2. Mengi na mtoto wake kuwekewa mtego, tukio lile lilipangwa na nani?
3. Ulimboa kung'olewa kucha na meno tukio hilo lilipangwa na nani?
4. Mwangosi kutolewa roho, tukio hio lilipangwa na nani?
5. Kibanda kung'olewa meno na jicho, tukio hilo limepangwa na nani?
6. Mbwambo kuchinjwa kwa msumeno kule Tengeru, tukio hilo lilipangwa na nani?
7. Kule Igunga mtu kutoweka, tukiolilipangwa na nani?
Orodha ni ndefu na katika matukio yote hayo hakuna majibu hadi sasa.
Si chama au serikali ya chama chako imewahi kutolea majibu. Majibu ni upepo utapita.
Nape wewe unaishi Tanzania, na nyadhifa zako pamoja na maisha yako ni kwasababu upo Tanzania .
Yakitokea yasiyotarajiwa na yasiyo ombewa si wewe si mimi au yule atakayekuwa salama.
Hakuna shujaa kati kati ya vita na vurugu
Nakusihi sana mdogo wangu iangalie Tanzania kwanza halafu ndipo uangalie mambo mengine.
Unaandika kwa jeuri na dharau kwasababu upo ndani ya Tanzania iliyotulia na inayolekea kuchafuka.
Kwanini kijana wa umri wako unafikia mahali pa kujisahau namna hiyo?
Kama Nyerere alisema CCM si mama yake, wewe ni nani nakwa uwezo upi unadhani CCM ni bora kuliko roho za Watanzania wasio na hatia.
Hivi wanajamvi, hawa ndio vijana tunaowapigia debe waliongoze taifa kweli!
Kama Nape kasema hivi nani kabaki na kabaki na busara ipi?
Nape, ubinadamu ni bora kuliko bendera za chama. Utangulize ubindamu na usilewe na dunia hii.
Leo unaona roho za watu na damu zao ni nyepesi kwasababu una rungu, umesahau kuwa unaishi ndani ya nyumba ya glass.
Mungu akusadie uone kile uischokiona sasa hivi, na heri ya kukaa kimya ili watu wawe na shaka nawe kuliko kuongea na kuwatoa mashaka waliyokuwa nayo juu yako.
Bado ni mdogo Nape, tuulize tumeyaona mengi, tumewaona wafalme wakipaa na kuanguka.
Inaumiza sana kichwa kumuona kijana anayeonekana mwenye afya njema ya mwili lakini akili yake kuonekana haiko sawa. Tuache siasa katika masuala ya hatari kama haya. Jamani jirudini maana kama mchangiaji mmoja hapa alivyosema Nape unalo jukwaa na kuzungunza na una cheo ulicho nacho kwa sababu uko Tanzania yenye amani!
Lakini tuendako kama hatutajirudi hasa watawala wetu wasipojirudi vyeo hivi na midomo yenu itatoa harufu mbaya muda wote maana hamtakuwa na majukwaa ya kuzungumzia maana mtakuwa wakimbizi ukimbizini wakati watanzania tulio wengi tutakuwa tumeteketea...,
Tuache siasa tukemee kwa nguvu zote ugaidi huu. Na serikali kama inasema ni CHADEMA wamejilipua, sawa lakini waliokufa ni watanzania na serikali yoyote duniani ina jukumu la kulinda raia wake, basi kamateni hao chadema kwa ushaidi uliopo na si wa mh. Mwigulu Nchemba bingwa wa kutengeneza filamu za ushahidi wa popote hata mbinguni. Inakera sana jamani.
Naunga mkono maneno ya nape.
Chadema mnatafuta public sympathy
nngu007
Ni kibaya kipi alichosema Nape Nnauye? nyie hamtaki kuelezwa ukweli lakini huo ndio ukweli wenyewe!