Taarifa ya Tamko la CHADEMA Jana

Nyamigota

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2011
Posts
365
Reaction score
152
Wadau, jana kulikuwa na mbwembwe nyingi sana eti waandishi wa habari waliitwa kwenda makao makuu ya CHADEMA kwenda kusikiliza tamko la Sekretarieti ya CHADEMA.

Katika fuatilia yangu kwenye vyombo vya habari, yaani channel zote za taarifa ya habari jana usiku sikuona tamko lolote, leo pia katika kusikiliza magazeti RFA asubuhi hii pia sijasikia kabisa tamko hilo. Je waandishi wa habari hawakupewa posho ya kutoa habari kama walivyozoweshwa na CCM?

Naomba kuwasilisha!
 
.......mtu yeyote aaanzaye kuuliza swali kwa kutumie.."ETI" ni wakumwogopa kama ukoma......huwa ni mnafiki mara zote..!
Mkuu K.Msese, "eti" ni kitangulizi cha ishara ya ama "not sure" yaani huna uhakika, au "don't belive!", yaani huamini!.

Kwa mujibu wa ile "eti" yangu kule, kwa vile taarifa hizo nimezisikia kutoka source isiyo na uhakika, then zilipandishwa kwa kuitwa ji "tetesi", ukakika au uthibitisho ukishapatikana, neno tetesi huondolewa na "eti" pia huondoka!.

P.
 
Hata wafarisayo walikuwa wakitumia neno "eti" mara nyingi wakati wakimwuliza YESU maswali ya kumtega ili tu wafanikishe malengo yao....eti hutumiwa na ibilisi, mtu mnafiki ambaye hulijua jambo mwanzo mwisho, hivyo huja kwako akitumia "eti" ili kusikia una mtazamo gani juu ya hiyo ishu.

Mara zote, ETI hutumika kwa mtu mwenye taarifa ya hicho anachokuuliza nacho, hivyo usijibu swali hilo!....mkuu Pasco nadhani utakuwa umenielewa.....!
 
tutajuaje kama waandishi hao hao hawakuitwa kwa mlango wa nyuma na Nape wakapewa bahasha za khaki ili wasitoe tamko la Chadema! maana uandishi wa habari wa digitali unajali nani anatoa fungu ili habari ziandikwe au zisiandikwe na zikiandikwa ziandikwe kwa uelekeo upi! hakunaga kama 'Mwanahalisi'!

halafu wewe na hizo 'eti' zako hatuzitaki. leta uzi uliokamilika. usituletee ushushushu wako humu JF!
 



Kwani Nyamigota na Pasco ni ID za mtu mmoja!!!!!

Mbona hizi kauli zina utata???

Naomba kujulishwa tafadhari!!!!!


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Last edited by a moderator:

Vyombo vyenye nasaba na CCM/mafisadi havitatoa tamko hilo kamwe
 
Eti hivi ndivyo ulivyouliza kwamba lile tamko likowapi?? Inawezekana kuwa tamko hilo linawahusu wao (waandishi) tu, hivyo baada ya kusikia tamko husika hawakuona haja ya kulivujisha kwa umma coz ingekua ni mis-use of resourses (vyombo vya habari).
 
Kwani Nyamigota na Pasco ni ID za mtu mmoja!!!!!

Mbona hizi kauli zina utata???

Naomba kujulishwa tafadhari!!!!!

MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
Mkuu Mizambwa, kwa mujibu wa sheria za jf, huruhusiwi kumfananisha member yoyoye na member mwingine yoyote hata kama wanashabihiana kwa kiasi gani!. Hili ni kosa linaitwa "name calling" na adhabu yake ni ban!.
Pasco.
 
cdm matamko kila kukicha na mwendelezo wake huwa haufahamiki kisayansi mtu akipata ulemavu akili yake inakuwa sio pure .mfano dk slaa
 
Hata wasipotoa habari watanzania wameshaelewa SSM kupitia maisha ya umaskini na mateso wanayoishi huku matabaka ya matajiri na maskini yakikua kwa kasi!!! Kwa hakika waandishi wa habari njaa zinawafanya wanapoteza sifa. Ukimwalika tu kwa kazi anataka hela ili akatoe habari. Weledi hawa na tena ni chumia tumbo tu. Wahariri wenyewe wananunulika kirahisi sana na kwa sasa naona dalili SSM wameshawanunua wote!!! Wao ndo madikteta wa habari ipi itoke na ipi ifukiwe!! Rafiki yangu wa Mwananchi ameshapokea kitita!! Mpaka afike 2015 atakuwa billionaire!!
 
Mkuu Mizambwa, kwa mujibu wa sheria za jf, huruhusiwi kumfananisha member yoyoye na member mwingine yoyote hata kama wanashabihiana kwa kiasi gani!. Hili ni kosa linaitwa "name calling" na adhabu yake ni ban!.
Pasco.

Pasco, usijitie kuwatisha watu kwa kujifanya unakimbilia sheria/kanuni za JF. Umejiumbua mwenyewe na Mizambwa yeye kapiga mistari kauli zako mbili-kwa ID tofauti zikirejea kitu kimoja. Wewe ndiye Nyamogota.

Katika uzi huu, eti ya kwanza inatolewa na ID ya Nyamigota. Anaposhambuliwa na K.Msese juu ya matumizi ya eti, wewe unaibuka na kutetea. Humtetei Nyamigota kama nafsi ya tatu bali unamtetea kama nafsi ya kwanza. Angalia kauli yako...
"Kwa mujibu wa ile "eti" yangu kule, kwa vile taarifa hizo nimezisikia kutoka source isiyo na uhakika,"

Tuambie wapi katika uzi huu wewe ulitumia 'eti' ikiwa wewe ni mtu wa pili kuchangia na pakiwa na tofauti ya dakika 28 toka mtoa (muanzisha) mada kuiweka? Vinginevyo leo nitajua nitajua Kitabu cha SARUFI na FASIHI cha Fr Nkwera hakikuwa na msaada kwangu zama zile nikisoma Kiswahili darasani.

Shukrani Mkuu Mizambwa, umeona vema. Pasco ndiye Nyamigota hawezi kukana kama ni muungwana. Ila kwa jinsi alivyombishi, bado atakuja na kuendelea kubisha.
 
Wewe bado unategemea tv, radio na magazeti kupata habari za kuaminika?

Wenzio tupo jf na hapa ndio kila kitu
 
Mkuu Mizambwa, kwa mujibu wa sheria za jf, huruhusiwi kumfananisha member yoyoye na member mwingine yoyote hata kama wanashabihiana kwa kiasi gani!. Hili ni kosa linaitwa "name calling" na adhabu yake ni ban!.
Pasco.

Fafanua alichouliza. au ndo ...........,, au?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…