Taarifa ya Mh.Godbless Lema bungeni.

Hapa Spika alishachemsha na kwa hatua yeyote itakayofuata itamsafishia njia Lema na CDM.hii ni nafasi nzuri ya ukweli kuwa wazi ili hata wale walioshindwa kusikia basi wasikie na kuelewa.
 
Kutoa mawazo si kiburi.
Ongelea hoja, kama Lema hana elimu ya kutosha tusiseme?

duh sasa wewe mwenye elimu mbona umeshindwa kutambua kuwa kama kigezo cha kuwa mbunge ni elimu basi wengi wasinge kuwa wabunge.Ndugu yetu Lameck Airo(mbunge CCM) mbona anaelimu ya darasa la saba na anawatumikia watu na ni mmiliki wa mahotel makubwa tu ya LAKAIRO.Usiwe mbaguzi wa elimu leo umeanza elimu kesho itakuwa dini,jinsia kesho kutwa rangi.
 
Hana jipya.

Lema bado ni kinda kisiasa. Anadhani siasa zinaendeshwa kihuni.

Semina aliyohudhuria Ubungo ilikuwa bure, pesa za serikali zilipotea pale.

Bila shaka upeo wake ulivyo unatokana na elimu yake pamoja na malezi aliyopewa na chama chake.

Hatuna cha kufanya, machalii wa Arusha wamemchagua.

Hata hivyo bado kidogo tu watatambua kuwa imekula kwao - ni hasara ya miaka 5.
Mtazamo wangu nakuona kishongo hufikirii vizuri,na kama unafikiria basi ni kinyume,hivi wewe huoni kama PM alijibu lile jibu kisiasa? Unajua fika wenzetu wamekufa kwa uzembe wa polisi?Hivi polisi yetu ingepelekwa tunisia au misri kutuliza maadamano ingeua watu wangapi? Polisi arusha walitumia nguvu zaidi kutokana na maelekezo ya dola,tumeona nchi mbalimbali zenye polisi wenye maarifa wanavyopambana na waandamanaji ambao ni hatari na wanafaulu kuwatuliza
bila kuua.Hivyo polisi wetu walikosea moja kwa moja.Hivyo kwa yaliyotokea arusha OCD,RPC,IGP na waziri wa mambo ya ndani ilitakiwa wajiuzuru au wafukuzwe kazi kama hawajajiuzuru.Sasa PM ameeleza juujuu na siasa nyie mumemuelewa kuwa mkweli kutokana na akili yenu kuwa zembevu.PM amezungumza bila usahihi na ameelemea upande wa kuilaumu chadema bila kuangalia upande wa pili ambayo ni serikali,Siasa ni utendaji wa kazi na sio uzoefu kwani hujaona hosni mubarak anauzoefu wa miaka 30 lakini hamna kitu.Pia angalia squad ya CCM wote ni wazoefu na ndio wameiweka nchi hapa ilipo kwa kutumia uzoefu wao wote.KISHONGO UWE UNAWAZA SAWASAWA.
 
Unatumia basis ipi kusema hawezi kufanya alichoanzisha. take it from me Last week tayari wanafunzi zaidi ya 500 walikuwa wameshajaza fomu za kusaidiwa na mfuko tayari umeshachangiwa mamilioni ya hela na wapiga kura wapenda maendeleo wa Arusha na mimi ni shahidi kwani tumekuwa tukifanya very close follow up. Mfuko ni well coordinated na kama unabisha nenda ofisi ya Mbunge wa arusha iliyoko ofisi ya mkuu wa wilaya ya Arusha. Batilda asingeweza haya kwani alikuwa anatafuta ubunge kama ngazi ya kuwa waziri na hiyo ndiyo ilikuwa END GOAL YAKE TUU.

Kama kweli wewe ni mdau kwenye huo mfuko utakuwa umeshasikia malalamiko kuwa 90% ya wanafunzi waliojaza fomu ni Wachagga na wanachama wa Chadema.

Ndiyo sera ya cdm kujenga matabaka ya kikabila na kichama?

Arusha kuna Wamasai, Waarusha, Wasonjo, Wameru nk nk. Kwa nini wao watengewe 10% tu?

Tunatilia shaka madhumuni ya kuanzisha mfuko huo.
 
Nyerere alikuwa amekwenda shule.
Ni mtu aliyekuwa anaona mbali na kupanga mikakati sawia - dunia ni mashahidi.
Kumlinganisha Nyerere na Lema ni tusi kubwa...kwa Mwalimu mwenyewe na kwa WaTz.

Ukweli ni kwamba Lema na majority ya viongozi wa cdm ni immature kisiasa. They are just political opportunists.
Bahati mbaya ni kwamba mashabiki wao watakuja kugundua hili wakati imeshakula kwao.

heshima kwako Kishongo,
nimekusoma sana mkuu na kukufuatilia kwenye thread nyingi, unaonekana una chuki binafis na Chadema tena kubwa sana iliyoota mizizi moyoni mwako.

ningefurahi kama ungekuwa huru katika mawazo yako. Lakini unaonyesha ushabiki na kupenda chadema ikosee na kufa kabisa.

kwa taarifa yako viongozi wa Chadema ni makini na werevu kuliko ndg zako wapendwa wa ccm, unapowaponda viongozi wa chadema una maana wa ccm ndio makini??

kinachowasaidia watu kama nyie na ccm yenu ni ujinga na umasikini wa wa tz bt one day yes tutapata ukombozi wa kweli. Na Mnara wa Babeli lazima utaanguka kwani hiyo ni saturation point yao na imekaribia.

nitafurahi sana kama utakuwa mjenga nchi na sio kuishambulia Chadema hata kama wana haki(kama hii isu ya Arusha) una tuaminisha wengi kwamba wewe na wenzako mnatumiwa au kununuliwa muharibu muv za kimapinduzi na kimageuzi.
 
M... Hivi polisi yetu ingepelekwa tunisia au misri kutuliza maadamano ingeua watu wangapi?.

Polisi wetu wana ujuzi mzuri kama wa nchi zingine. Tatizo ni pale wanasiasa wanapowachochea wafuasi wao wavamie vituo vya polisi. Hata kule Tunisia na Misri walikiufa watu waliojaribu kuvamia vituo vya polisi kama Arusha.

Kwa ufupi, wanasiasa ndio tatizo, hasa wale wenye siasa za uchochezi kama wa cdm.

Wanaowaponza watu wasio na hatia kufa ili wao wapate umaarufu wa kisiasa. Dhambi kubwa hii!
 
hivi hawa wanaosema suala la uzoefu, mbona unakuwa na mawazo ya kizamani. hoja hii ya uzoefu ndo inawafanya wazee waendelee kung'ang'ania madaraka. lema tayari ni mtu amabaye anajua anafanya nn, huyu ndo mwanamapinduzi halisi
 
We kishongo acha pumba zako, wewe ni wale wale ccm nadhani wewe ni Rostam a.k.a myemen.unakuja kumtetea waziri mkuu dhaifu zaidi kuwahi kutokea hapa Tanganyika tangu enzi za uhuru kaa kimya mnaua kwa risasi watanganyika wenzenu na nyie siku yenu yaja subirini.
 
Kama kweli wewe ni mdau kwenye huo mfuko utakuwa umeshasikia malalamiko kuwa 90% ya wanafunzi waliojaza fomu ni Wachagga na wanachama wa Chadema.

Ndiyo sera ya cdm kujenga matabaka ya kikabila na kichama?

Arusha kuna Wamasai, Waarusha, Wasonjo, Wameru nk nk. Kwa nini wao watengewe 10% tu?

Tunatilia shaka madhumuni ya kuanzisha mfuko huo.

we mwenyewe mbaguzi unaposema elimu ya Lema ndogo hastahili kuchaguliwa.Lete ushahidi wa allegations zako usiendeshwe na hisia.Naona mmeongezwa idadi kwenye kitengo cha propaganda.
 
heshima kwako Kishongo,
nimekusoma sana mkuu na kukufuatilia kwenye thread nyingi, unaonekana una chuki binafis na Chadema tena kubwa sana iliyoota mizizi moyoni mwako.

ningefurahi kama ungekuwa huru katika mawazo yako. Lakini unaonyesha ushabiki na kupenda chadema ikosee na kufa kabisa.

kwa taarifa yako viongozi wa Chadema ni makini na werevu kuliko ndg zako wapendwa wa ccm, unapowaponda viongozi wa chadema una maana wa ccm ndio makini??

kinachowasaidia watu kama nyie na ccm yenu ni ujinga na umasikini wa wa tz bt one day yes tutapata ukombozi wa kweli. Na Mnara wa Babeli lazima utaanguka kwani hiyo ni saturation point yao na imekaribia.

nitafurahi sana kama utakuwa mjenga nchi na sio kuishambulia Chadema hata kama wana haki(kama hii isu ya Arusha) una tuaminisha wengi kwamba wewe na wenzako mnatumiwa au kununuliwa muharibu muv za kimapinduzi na kimageuzi.

Pole. Inaonekana mapenzi yako kwa cdm yamekufanya kipofu hata huoni wala hutaki kusikia mapungufu yake na ya viongozi wake.
Siku moja utajua.
 
duh sasa wewe mwenye elimu mbona umeshindwa kutambua kuwa kama kigezo cha kuwa mbunge ni elimu basi wengi wasinge kuwa wabunge.Ndugu yetu Lameck Airo(mbunge CCM) mbona anaelimu ya darasa la saba na anawatumikia watu na ni mmiliki wa mahotel makubwa tu ya LAKAIRO.Usiwe mbaguzi wa elimu leo umeanza elimu kesho itakuwa dini,jinsia kesho kutwa rangi.

Sijasema kuwa elimu yake haimruhusu kuwa bungeni, la hasha, anastahili kuwepo kama walivyo profesa Maji M,arefu na Airo uliyemtaja.
Nilichosema ni kwamba elimu yake na malezi yake ya kisiasa (siasa za cdm) yanamfanya afanye vituko vya kipuuzi bungeni.
 
Angalia cv yake ndio ushahidi.

nataka ushahidi kuhusu hiyo 90% ya wanafunzi wanaotaka kusaidiwa na mbunge Lema kuwa ni wachaga maana usije ukawa mzushi tu.Suala la elimu linaelezwa kwenye sifa za mgombea wa ubunge ndio maana kawa mbunge kwani sifa hizo hazina ubaguzi wa elimu kama wewe ulivyo mbaguzi kwa hiyo sina haja ya CV yake.
 
Hii kweli siasa!Lema amekuwa mbumbu akidhani taarifa atakayowasilisha bungeni kulingana na maagizo ya Spika itamnusuru kwa Waziri Mkuu kuonekana kweli kadanganya Bunge na wananchi.Lema hatokuwa na cha ziada mbali na taarifa ileile iliyofahamika kama “Tamko la Chadema” juu ya Mauaji Arusha ambayo imekwisha tolewa na Viongozi wa Chadema na kutaka Nahodha na Mwema kujiuzuru.Mambo yatakuwa kama ifuatavyo:

1)Lema atawasilisha utetezi wake ambao nadhani hautakuwa na jipya mbali ya yale tuliyoyasikia katika media na wengine kujionea.Hapa msingi mkuu wa Lema itakuwa kusisitiza kuwa ilikuwa haki ya kikatiba chadema kuandama na kwa kuwa ilikuwa imekubalika na Kamanda wa Polisi Wilaya ya Arusha.Hapa kosa la Polisi ni kuuwa Raia japo mpaka sasa haijajibiwa kama wenzetu waliuwawa kabla ya kutolewa amri na Viongozi wa Chadema kwa wafuasi kwenda kuwakomboa Lema na wenzie ama baada ya kauli hiyo ya ukombozi.

2)Upande wa Serikali ni dhahiri sababu zao zimekwisha tolewa kuwa maandamano yalikuwa haramu isipokuwa mkutano ulikuwa halali kutokana na kauli ya IGP Mwema kabla ya kikao cha tarehe 5/1/2011.Polisi walilazimika kutumia nguvu pindi Chadema walipolazimisha maandamano na matukio ya vifo vya wenzetu yalitokana na uchochezi wa Viongozi wa Chadema hasa baada ya kuamuru Lema na wenzie wawe wamekombolewa kutoka katika kituo cha Polisi na kufikishwa katika viwanja vya Unga Ltd ndani ya saa moja.Polisi walitumia risasi kama “final resolution” baada ya kuona wanazidiwa nguvu na vijana wa Chadema waliokuwa na “munkari” wa hali ya juu wakitaka kuvamia kituo chenye silaha lukuki.Ni dhahiri hapa ndipo serikali inasema “bahati mbaya” wenzetu watatu waliuwawa.


Bungeni huu ni mtego tu ili haki ionekane kutendeka na Lema ameadhibiwa kwa kufungiwa kuhudhuria vikao visivyopungua vitano bungeni na kulazimika kufuta kauli yake.Na imani kwa bunge ninaloliona mchango wa kile atakacho kiwasilisha Lema uta kuwa ule wa Mudhihir na Zitto kabwe.Lema ata kama anadhani utetezi wake utakuwa “extraordinary” asitarajie maamuzi yatam-favour.

Hii kweli siasa!

Nionavyo mimi hatima ya suala hili ni pale tutakapo pata jibu la kuku na yai kipi kilitangulia?.

Ni vigumu kujadili wananchi kama hawa wanao andika hizi opinions zao humu ndani ya JF kwa kukaa upande mmoja wa CCM siku zote. Hivi nyie ni binadamu au? Acha kuwa "Political" mahali pasipo political. Kitu gani kili walazimisha polisi kwenda kuzuia maandamano? Kibali kilitolewa na siku moja baada ya maandalizi ya wananchi wa Chadema kujiandaa kukutana na kusikiliza viongozi wao mnakuja kusema kuna hatari imetoka kwenye kitelejinsia. Tunaomba huo utelejensia mliokuwa nao nini? Hili ndilo swali Pinda na CCM lazima mjibu kwa sababu uonevu na vitisho kwa wananchi mnafikiri vitaendelea mpaka lini. Jeshi la polisi na FFU sio la chama kimoja ni vyombo vya wananchi na humo FFU kuna wanachama wa Chadema kama hamjui. Tukienda kwenye tukio lenyewe la kupiga risasi, tuaona wananchi walikuwa wanatembea na kufurahia siku yao mpaka polisi walipo jitokeza kama nyoka shimoni. Polisi walipotokea na kuanza kupiga risasi na kuwachukua viongozi na wanachama wa Chadema hapo ndio "hell" ilioanza na kila Mtanzania aliekuwepo atakueleza hili. Kuna mashahidi wananchi na kuna videos za hili tukio na huu ujuzi wa kutumia ofisi za serikali, polisi na sasa bungeni kuwadanganya wananchi hatutakubadikila kamwe. Tunataka ushahidi wa Pinda uje mbele ya taifa na Chadema watatoa wao pia. Wanachama wa CCM mnaonekana kama akili zenu na upofu wenu hata televisions hamkuzifungua kuona Misri, Pharaoh Mubarak alipoanguka na kufukuzwa na wananchi wake. Kilicho tokea Misri ni kwamba wananchi walikuwa wanaishi kwenye "military emergency laws" na Fear ndio ilikuwa inawafanya kuogopa kwenda hata kuandamana, hii Fear ilipoondoka tumeona Tahrir Square ilivyobadilisha Misri na prospective ya dunia. Wananchi wa Tanzania wapo karibu ya Tahrir Square na tunasogea tupo hatua kumi tu. Nyie ccm endeleeni kujitia kamba shingoni...
 
Hana jipya.

Lema bado ni kinda kisiasa. Anadhani siasa zinaendeshwa kihuni.

Semina aliyohudhuria Ubungo ilikuwa bure, pesa za serikali zilipotea pale.

Bila shaka upeo wake ulivyo unatokana na elimu yake pamoja na malezi aliyopewa na chama chake.

Hatuna cha kufanya, machalii wa Arusha wamemchagua.

Hata hivyo bado kidogo tu watatambua kuwa imekula kwao - ni hasara ya miaka 5.

Ni aheri ukinda wa Lema kuliko uzoefu wa CCM wa kushindwa kusimamia uchumi na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viongozi na watendaji serikalini, karibu kila mahali kuwa wachumia tumbo, wasio na lengo wala dhamira ya kuijenga Tanzania kama Taifa. Lema anaweza kukosa uzoefu lakini ana dhamira, wakati CCM wana uzoefu mkubwa wa mbinu mbalimbali za wizi wa mali ya umma, ufifishaji wa haki za binadamu na demokrasia, na hila mbalimbali za kuwadanganya wananchi.

Uzoefu wa CCM ni adui mkubwa wa kila Mtanzania anayeipenda nchi hii. Tutafute watu wasio na uzoefu wa CCM hata chembe ili walibadilishe Taifa.
 
Nimegundua kwanini watu ambao wanaheshimika ndani ya JF hwachangii kwenye thread kama hizi. And I will follow suit!!
 
Sijasema kuwa elimu yake haimruhusu kuwa bungeni, la hasha, anastahili kuwepo kama walivyo profesa Maji M,arefu na Airo uliyemtaja.
Nilichosema ni kwamba elimu yake na malezi yake ya kisiasa (siasa za cdm) yanamfanya afanye vituko vya kipuuzi bungeni.

sasa ndugu yangu kishongo mbona unataka kukosa hoja,hebu tueleze hayo mambo ya ajabu ya mh.Lema,kuomba mwongozo ili kujua anaweza kuchukua hatua gani kama kiongozi mkubwa kama waziri mkuu atalidanganya bunge na taifa?subiri alete utetezi wake.
 
On a serious note mbunge yeyote wa upinzani ata aongee scrap huwa naisi ameteleza kidogo tuu bse wao kuwa bungeni ni suala la kuwapongeza.
Kwa mtazamo wangu Lema aliomba muongozo wa speaker na wala hakusema kuwa Pinda muongo.
Yaani hii inanikumbusha yesu alipoulizwa wewe uu mfalme wa wayahudi akamwambia muuliza swali wewe wanena.
Infact mama Makinda ndo amezua hoja ya Pinda kadanganya
 
Sijasema kuwa elimu yake haimruhusu kuwa bungeni, la hasha, anastahili kuwepo kama walivyo profesa Maji M,arefu na Airo uliyemtaja.
Nilichosema ni kwamba elimu yake na malezi yake ya kisiasa (siasa za cdm) yanamfanya afanye vituko vya kipuuzi bungeni.

Sidhani katika nchi yetu kama kuna yeyote aliyewahi kufanya vituko vikubwa kuliko viongozi tulio nao, hawa wa CCM. Kuifanya nchi kama Tanzania yenye kila aina ya rasilimali daima kuwa kati ya nchi 3 masikini kuliko zote Duniani, nadhani hiki ni kituko ambacho kitaendelea kusimuliwa kwa miaka mingi ijayo. Na sidhani hata kama tukimchagua mtu mbumbu kiasi gani, anaweza kufanya haya ambayo CCM wamefanya kwa miaka mingi. Viongozi tulio nao ndani ya CCM, hata kama ukasikia ana PhD, kwa kiasi kikubwa anaitumia hiyo PhD yake kuhakikisha anaiba bila kutambulika lakini siyo kwajili ya kuliendeleza Taifa. Musomi mwenye dhamira mbaya ni mbaya mara mia kuliko mbumbu mwenye dhamira njema.
 
Nyerere alikuwa amekwenda shule.
Ni mtu aliyekuwa anaona mbali na kupanga mikakati sawia - dunia ni mashahidi.
Kumlinganisha Nyerere na Lema ni tusi kubwa...kwa Mwalimu mwenyewe na kwa WaTz.

Ukweli ni kwamba Lema na majority ya viongozi wa cdm ni immature kisiasa. They are just political opportunists.
Bahati mbaya ni kwamba mashabiki wao watakuja kugundua hili wakati imeshakula kwao.
Ni kichaa atakae subutu kumlinganisha Nyerere na kiongozi yoyote wa hapa Tanzania....
Nilicho kuwa nakizungumuzia ni Uzoefu kama ulivyo sema yakuwa Lema hana uzoefu kwenye siasa....
 
Back
Top Bottom