G-Mdadisi
Senior Member
- Feb 15, 2018
- 157
- 99
WATU watatu wamekufa na wengine zaiidi ya 28 wamelaza katika Hospitali ya wilaya Micheweni wakiendelea kupatiwa matibabu baada ya kula samaki aina ya KASA katika shehiya ya Msuka.
Akizungumuzia tukio hilo daktari wa Wilaya ya Micheweni Mkubwa Habibu amesema kuwa tayari wagonjwa waliofika wanapatiwa matibabu huku akibainisha changamoto ikiwa kukosa ushirikiano pamoja na taarifa sahihi kutoka kwa waathirika wa tukio hilo.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya amesema kuwa mpaka sasa hajapata idadi ya wananchi ambao wametumia samaki huyo.
Aidha amewataka wananchi waliotumia samaki huyo kuweza kujisalimisha katika kituo cha afya ili waweze kupatiwa matibabu.
Naye Seif Mzee Khamis mzazi wa watoto wawili waliofariki kutokana na tukio hilo amesema yupo tayari kutoa ushirikiano ili kuweza kunusuru maisha ya wengine.