Taarab inaelekea pabaya

Taarab inaelekea pabaya

Yusomwasha

JF-Expert Member
Joined
Dec 5, 2014
Posts
2,092
Reaction score
844
Wakuu muziki wa taarabu umeanza kuelekea pabaya zaidi tofauti na mwanzo ilianza taarab asilia ikaja #modern #taarab na sasa ni #modern #taradance.

Muziki umegeuka vijembe,matusi ya live yaso na mfano angalau hata mwanzo walikuwa wakitumia lugha ya mafumbo, kiduku, kuvaa mavazi ya ajabu nayo yameikumba taarab imekuwa ni vurugu tosha muziki huu umegeuzwa dance na rhumba utunzi mbovu wa mashair usiozingatia mizani wala vina kibaya zaidi juzi kati wakati wa tuzo za KTMA/Kill Music Award walishangaza Tanzania kwa kitendo cha kusikitisha cha kuutaja wimbo wa rhumba alioimba isha mashauz kuwa eti ndo wimbo bora wa taarab.

Wimbo huo unaitwa #mapenzi #hayana #dhamana ni wimbo wa rhumba ulioingza kwenye taarab kuwa eti ndo wimbo bora, hii imeleta manung'uniko makubwa kuuweka wimbo ambao una mashair mabovu kuwa ndo wimbo bora.

Hizi #modern #taradance zitatupeleka pabaya, nini kifanyike kuikoa taarab?

Nawasilisha
 
taarab tunataka iwepo kwa faida ya vizaz vijavyo
 
taarab tunataka iwepo kwa faida ya vizaz vijavyo si kwa maslah 2
 
Taarab ilikuwa enzi za JKT ya kina marehemu Issa Matona (Kimasomaso), Patricia Hillary (njiwa), bila kuwasahau kina Shakila (macho yanacheka moyo unalia)... Siku hizi ni vurugu mechi tupu!
 
Kuna kitu kingine cha kichekesho kabisa kinaitwa taarabu
 
Huo wimbo aloimba isha unaoitwa wimbo bora wa taarab ukiusklza utabak ukicheka ktk taarab haujawah kushuhudiwa wimbo wa ajab hvyo ingia Tubidy Mobile Video Search Engine then kwenye search andika isha mapenzi hayana dhamana au angalia youtube kiukwel utabak kinywa wazi
 
Sabaha Salumu.... fimbo ya Mungu na nyinginezo... yupo poa sana
 
Back
Top Bottom