System aliyoitegemea Lowassa ilivurugwa na Kikwete!

System aliyoitegemea Lowassa ilivurugwa na Kikwete!

Anayeichagua CCM anamaanisha kuwa anayo hela ya kumlipia mwanaye A level na Chuo Kikuu.
 
Sasa si ufurahi kimya kimya ?unamweleza nani na kwa nia gani?mkubali msikubali CCM Tz haijapata Kuwa na upinzani wa kiwango hiki tangu uchaguzi wa vyama vingi.Hadi sasa CCM hawana uhakika wa kushinda Ndo maana wanatengeneza goli la mkono.Jiulize wanaogopa nini watu wakikaa Mita 200?Hata wakiponea chupu chupu ha watakuwa na Kiburi cha madaraka tena.Lowassa kawapa funzo hawatakaa wasahau.Mungu akisimamia upande wa haki hakuna binadamu wa kupinga.Viva Lowassa viva.

Naona unakubaliana kuwa Lowasa will loose the game
 
Nakubaliana na mantiki yako ya lowassa kuleta upinzani kwa ccm just like Mrema na ninakubaliana na mantiki yako ya kwamba ccm imefunzwa adabu kwa tishio feki!

Lakini kuna issue ya Upinzani kuvurugika na kuanza upya kwa kuwa umewekeza kwa lowassa kama lowasa lakini haujaweza kumtumia lowasa kuchukua viti vingi vya ubunge...wabunge wa chadema wako hoi katika kampeni majimboni.

Ni muda wa kuwakumbusha watawala wetu kujitambua na kutafakali kwa kina nini hatma ya Tanzania yetu lowassa amekutana na watu wenye kitu ya mabadiliko kwa kuwa watawala wameshindwa kuwasikiliza watawaliwa ni muda wa watawaliwa kusema hapana imetosha
 
Makongoro Mahanga bado ni waziri au?

Hivi wewe mbona mbishi tu? We lete hoja pinzani kwanini JK hajavunja Baraza la mawaziri. Hata mtoto wa primary anajua Makongoro Mahanga si Waziri kwani si mwana CCM tena!
 
Ni ukweli usiopingika kuwa lowasa ameanza harakati za kuusaka urais muda mrefu pengine toka 1995.

Mwaka 2005 akimsindikiza kikwete lowassa alijiwekea mizizi au tuseme alitengeneza mtandao ambao ulimuingiza kikwete madarakani na kumfanya yeye kuwa waziri mkuu.

Baada ya kutemwa uwaziri mkuu system ya lowassa iliendelea kuwa madarakani kwa muda mfupi kabla ya JK kuanza kuivuruga na kuisambaratisha kabisa.

Mpaka tunafika 2015 JK alifanikiwa kabisa kuiondoa system ya lowassa serikalini.

Nadhani alifanya hivi kwa maandalizi ya kumkata katika kinyang'anyiro cha uchaguzi ndani ya ccm pengine kwa maelekezo maalum


Chadema na Team lowassa wamedanganyika na kile kilichoitwa nguvu ya waziri mkuu bila kujua ilishafutiliwa mbali.

Wengi wa wakurugenzi na wakuu wa taasisi ambao waliwekwa na lowassa walishatemwa siku nyingi.

MaDC na MaRC loyal kwa lowassa walishatemwa siku nyingi.

Kwa hiyo ile nguvu ya mamba baharini haipo kwani bahari ilishakaushwa.

Kwa sasa lowassa amebakia na usanii tu kuaminisha watu kuwa ana mahusiano na system kumbe hamna kitu ni maigizo tu.

Hili laweza thibitishwa na kauli kinzani kutoka UKAWA...Mbowe anasema lindeni kura wakati lowassa alisema pigeni kura na kazi ya kuzilinda aachiwe.hizi ni sentensi mbili kinzani kutoka katika taasisi moja.

Vijana wanapaswa kutambua lowassa hana influence yoyote kwenye chama au serikali kwa sasa....makapi ya lowassa yako nje na yanajaribu kurudi ndani ili kuweka mirija ya kula hela zetu tu.

Im so disappointed with Chadema baada ya kuuvaa mkenge huu wa kihuni ambao unaenda kuirudisha nyuma miaka 20.

Wafikirie waliohamia Chadema au Ukawa na uhusiano wao na CCM au serikali in the past 5years ndio utanielewa.

Kwa sasa Chadema wajikite katika kampeni za ubunge zaidi ili kuokoa jahazi..operesheni ya siku nne...mission impossible!

Wewe mpuuzi kweli
Sidhani kama Lowasa anategemea wahuni wa system bali anategemea nguvu ya umma

Unataka kutuaminisha kuwa MAGUFULI anategemea SYSTEM nawe unashangilia kwa hilo hivi kweli una akili. Kuwa mzalendo acha upumbavu, unafikiri magufuli akipita atakupa nn? Hupati chochote
 
Umeandika kama una haki miliki ya Tanzania.F.Y.I Hata JK hana haki miliki,na mbaya zaidi anaweza kuvuruga kila mfumo,lakini hawezi kufuta mahaba waliyonayo Watanzania katika mioyo yao!!Kwa kuwa JK alivuruga mfumo uliomweka akidhani anamkomoa ENL anajikuta amekumbatia mzinga wa nyuki!!..LOWASSA ANATOSHA.

Sema mahaba uliyo kuwa nayo wewe usiseme watz kwa huyo maumvi wako watu hawataki mahaba wanataka kazi bwana magufuli hoyee
 
Lawrance Masha alishatemwa kitambo!

Sumaye hakuwa na ubavu kwa merry Nagu

Kingunge aliwekwa pembeni!

nawashangaa cdm eti leo wanamtema dr slaa ili wamkumbatie masha...makongoro mahanga...kingunge..mgeja....guninita
 
Wewe mpuuzi kweli
Sidhani kama Lowasa anategemea wahuni wa system bali anategemea nguvu ya umma

Unataka kutuaminisha kuwa MAGUFULI anategemea SYSTEM nawe unashangilia kwa hilo hivi kweli una akili. Kuwa mzalendo acha upumbavu, unafikiri magufuli akipita atakupa nn? Hupati chochote

Hakunaga hao unaowaita wahuni wa system
 
Back
Top Bottom