Synovate: Vinara tisa urais 2015

Synovate: Vinara tisa urais 2015

Hawa wakenya waache unafiki.
Sasa hivi wanatoa matokeo haya, ikifika kipindi cha uchaguzi, kila kitu in favour of magamba. Narabuuuku!
 
Nilipoona huu utafiti kitu cha kwanza kujiuliza umefanywa na kina nani? Kumbe ni tawi la CCM propaganda, Synovate!
 
Mi nashaur Josephine km kweli ana nia ya dhati na chama angebaki km mchumba wa Dr na mwanachama wa CDM bas mpaka labla atakapochaguliwa kwa hiar ya wanachama kushika wadhfa wowote mana kiukweli kwa kias flan anampunguzia Dr kura badala ya kumuongezea pia kuleta migongano isio ya lazima. Huu ni mtazamo wangu.
 
Haieleweki, hapa asilimia zimekaaje wakuu mbona jumla haifikii 100. Au ndio synovate wanatuonyesha jinsi kura za dr Slaa zitakavyochakachuliwa!
 
Hivi mtu unawezaje kuandika habari yooooote hii, na kuweka asilimia zooote hizo, bila kutoa sample space ilikuwa vipi (watu wangapi, kutoka wapi etc) na methodology iliyotumika ( wamepewa questionnaires, wamepigiwa simu etc).

Gazeti lina mhariri hili?

Tutajuaje kama sample space si madarasa mawili ya shule moja ya sekondari yanayojumuisha wanafunzi waliojichokea na kujaza questionnaires randomly kama sehemu ya adhabu ya utovu wa nidhamu?

Ni kweli kabisa tungeelezwa hiyo "study" ilifanyikaje, na pia njia iliyotumika kupata hayo majina; je kulikua na majina watu waliyopewa kutoa maoni yao, au ilikua "reseach questions" hazikutaja majina badala yake zilikua wazi kwa watu kutaja majina! Bila "methodology" na hasa "sampling techniques" taarifa ya utafiti huu haitaeleweka vema.
 
Katoka walitajwa hapo, waliowahi kugombea urais ni Slaa na Lipumba tu. Zitto ametamka kuwa anataka kugombea, Pinda na Magufuli hawajawahi hata kutamka kuwa wanataka kugombea.

Synovate wanatumia vigezo gani kumfananisha mtu aliyewahi kufanya kampeni ya Urais nhci nzima na mtu ambaye hajawahi hata kusema kama anautaka Urais kama Magufuli?

Jimmy Carter wakati anatangaza kugombea Urais wa Marekani asilimia kubwa ya wamarekani walikuwa hawajawahi hata kulisikia jina lake...
 
Ni wahuni hawa hawako fair ni bendera fuata upepo!
Tena wanajishushia credibility
 
Mi nashaur Josephine km kweli ana nia ya dhati na chama angebaki km mchumba wa Dr na mwanachama wa CDM bas mpaka labla atakapochaguliwa kwa hiar ya wanachama kushika wadhfa wowote mana kiukweli kwa kias flan anampunguzia Dr kura badala ya kumuongezea pia kuleta migongano isio ya lazima. Huu ni mtazamo wangu.

Kunyamaza ni busara!
 
Haieleweki, hapa asilimia zimekaaje wakuu mbona jumla haifikii 100. Au ndio synovate wanatuonyesha jinsi kura za dr Slaa zitakavyochakachuliwa!

Mkuu nimefanya marekebisho kwa kuongeza na wale waliopata asilimia za chini kabisa.
 
Mbona inaonekana umaarufu wa Dr. Slaa umeporomoka kutoka 42% hadi 17%? Hii inaashiria nini? Watu wamemchoka au wameichoka CHADEMA? Umaarufu wa CHADEMA nao umeshuka! Inaonekana kama kuna negative correlation kati ya M4C na umaarufu wa CHADEMA.

Mkuu Ritz umeamka?
Nadhani uchaguzi wa serikali za mitaa next year 2014 uta-reflect uhalisia wa kama Dr. Slaa bado ni mwamba au laa,
 
Gazeti: Mwananchi
MTafiti: Synovate

Propaganda. Not worth the paper its written on
 
Synovate ni chombo cha idara ya propaganda ya CCM! Eti wanaipandisha CCM umaarufu kwa tafiti uchwara! Magazeti na vyombo vya habari vimeshindwa nyie mtaweza? Nia yenu ni kuwakatisha tamaa watanzania wenye nia ya kuleta mabadiliko nchini!
 
Mbona inaonekana umaarufu wa Dr. Slaa umeporomoka kutoka 42% hadi 17%? Hii inaashiria nini? Watu wamemchoka au wameichoka CHADEMA? Umaarufu wa CHADEMA nao umeshuka! Inaonekana kama kuna negative correlation kati ya M4C na umaarufu wa CHADEMA.

Mkuu Ritz umeamka?

Hiki ndo hasa CCM wanachotaka watanzania wafikirie, eti watu wameichoka CHADEMA, watu wamemchoka Dr. Slaa kwa lipi? Hawa wakenya wanafanya biashara na CCM, wala hatujui nani mfadhili wa hizi tafiti zao! CCM inatumia kila mbinu kuwathiri watanzania kisaikolojia ili ionekane inakubalika! CCM imefanya nini cha kurudisha imani kuwatukana viongozi wa CHADEMA, kumchagua kinana mwizi wa meno ya tembo? Hicho kimerejesha imani? Watanzania wa leo hatudanganyiki!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom