Swali Rahisi kwa Zitto Kabwe

Swali Rahisi kwa Zitto Kabwe

Filipo Lubua

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2011
Posts
339
Reaction score
578
Jamani wadau wenzangu,

Nina Swali rahisi sana kwa Mh. Zitto Kabwe. Jana baada ya taarifa kuwa Mahakama imetupilia kapuni kesi yake na kuipatia ushindi Chadema, Zitto aliandika hivi kwenye ukuta wake wa Facebook:
Kwa kazi ya ‪#‎TegetaEscrow‬ ilivyokuwa ingeshangaza waathirika kukaa bila kujaribu kunivuruga. Bahati mbaya sana sivurugiki.
Swali langu ni rahisi sana: Zitto unadhani ni nani hasa akuvurugaye? Je unadhani Chadema ndio waliochukia kazi yako katika ESCROW na ndio maana wakakufukuza uanachama? Je unadhani waliotuhumiwa katika ESCROW wametia mikono yao mahakamani na kusababisha mahakama ikunyime haki yako? Hapa unayemtuhumu kutumiwa na waathirika wa ESCROW ni Chadema au Mahakama?

Swali lingine la mwisho, mbona hili suala la ESCROW linakuvimbisha kichwa kana kwamba wewe ndiye uliyeliibua? Katika hili swali langu la mwisho, nisieleweke kwamba nahafifisha kazi nzuri ambayo kamati ya PAC iliifanya, bali nieleweke kuwa ninatamani Kafulila apewe heshima inayomstahili katika sakata hilo. Yeye ndiye aliyeitwa ngedere, yeye ndiye aliyetishiwa kushitakiwa mahakamani, yeye ndiye aliyelipigania tangu mwanzo hadi mwisho. Krediti nyingi zingepaswa zimrudie yeye. Nikipata majibu ya maswali yangu haya mawili, moyo wangu utatulia kidogo.
 
Jamani wadau wenzangu,

Nina Swali rahisi sana kwa Mh. Zitto Kabwe. Jana baada ya taarifa kuwa Mahakama imetupilia kapuni kesi yake na kuipatia ushindi Chadema, Zitto aliandika hivi kwenye ukuta wake wa Facebook:
Swali langu ni rahisi sana: Zitto unadhani ni nani hasa akuvurugaye? Je unadhani Chadema ndio waliochukia kazi yako katika ESCROW na ndio maana wakakufukuza uanachama? Je unadhani waliotuhumiwa katika ESCROW wametia mikono yao mahakamani na kusababisha mahakama ikunyime haki yako? Hapa unayemtuhumu kutumiwa na waathirika wa ESCROW ni Chadema au Mahakama?

Swali lingine la mwisho, mbona hili suala la ESCROW linakuvimbisha kichwa kana kwamba wewe ndiye uliyeliibua? Katika hili swali langu la mwisho, nisieleweke kwamba nahafifisha kazi nzuri ambayo kamati ya PAC iliifanya, bali nieleweke kuwa ninatamani Kafulila apewe heshima inayomstahili katika sakata hilo. Yeye ndiye aliyeitwa ngedere, yeye ndiye aliyetishiwa kushitakiwa mahakamani, yeye ndiye aliyelipigania tangu mwanzo hadi mwisho. Krediti nyingi zingepaswa zimrudie yeye. Nikipata majibu ya maswali yangu haya mawili, moyo wangu utatulia kidogo.
Zitto namkumbusha kauli ya waria report ya PAC ni dhaifu sana

katika bilions of money tunajadii peza zilizotka kwa rugemalila wapi pesa nyingine
 
Last edited by a moderator:
Kwamawazo yangu finyu, me nadhan ccm au serekali imechangaia kwa namna 1 AMA nyingi, kwamba amesomewa shitaka lake na kutolewa hukumu, tarehe 10 ilimajibu yarudi yakutoshiriki binge lijalo Kabla ya tarehe 17, asiwasilishe hoja inayowahusu wizara ya ujenz, juu ya Pesa walizo Piga tena mabilion hayo, "ufinyu wangu mdogo nihuwo"
 
Kwamawazo yangu finyu, me nadhan ccm au serekali imechangaia kwa namna 1 AMA nyingi, kwamba amesomewa shitaka lake na kutolewa hukumu, tarehe 10 ilimajibu yarudi yakutoshiriki binge lijalo Kabla ya tarehe 17, asiwasilishe hoja inayowahusu wizara ya ujenz, juu ya Pesa walizo Piga tena mabilion hayo, "ufinyu wangu mdogo nihuwo"
Hapa ndipo nishindwapo kuwaelewa. Kwani Zitto ndiye aliyekuwa akifanya kazi za PAC peke yake? Mbona mnawapuuza wajumbe wengine wa kamati kama akina Filikunjombe ambao nao wana uwezo wa kuendelea na shughuli za kamati? Kufa kwa imamu kunakuwaje mwisho wa sala zote msikitini?
 
Mbona alifikuzwa hata kabla ya escrow zama zake zimeisha,,,
 
walio chukuwa fedha Stanibank mbona hukuwataja?!!!!!


Zitto umepokea pesa 15million kutoka kwa Singa Singa.

Zitto umepokrea 30 million kutoka kwa Ruge.
 
Kwa nini zitto kila kitu akifanya na watu anataka aoneshe kazi ile kafanya yeye peke yake kana kwamba wengine si lolote?
Ivi tujiulize zitto asipokuwepo PAC Ina maana kamati itashindwa kuwasilisha report kisa tu zitto hayupo?
Zitto acha ubinafsi
 
Usinyee kiganja kinachokulisha. Kumbe Zitto bado anaipenda CHADEMA na nje ya CDM si chochote!. Hata kama hukumu ingetolewa mwakani bado Zitto angetoka. Kama kweli shujaa na ni maarufu kuliko Chama analalamika nini? Umezoea kujitajirisha kwa uongo sasa kazi kwako. Karibu kitaani!
 
Jamani wadau wenzangu,

Nina Swali rahisi sana kwa Mh. Zitto Kabwe. Jana baada ya taarifa kuwa Mahakama imetupilia kapuni kesi yake na kuipatia ushindi Chadema, Zitto aliandika hivi kwenye ukuta wake wa Facebook:
Swali langu ni rahisi sana: Zitto unadhani ni nani hasa akuvurugaye? Je unadhani Chadema ndio waliochukia kazi yako katika ESCROW na ndio maana wakakufukuza uanachama? Je unadhani waliotuhumiwa katika ESCROW wametia mikono yao mahakamani na kusababisha mahakama ikunyime haki yako? Hapa unayemtuhumu kutumiwa na waathirika wa ESCROW ni Chadema au Mahakama?

Swali lingine la mwisho, mbona hili suala la ESCROW linakuvimbisha kichwa kana kwamba wewe ndiye uliyeliibua? Katika hili swali langu la mwisho, nisieleweke kwamba nahafifisha kazi nzuri ambayo kamati ya PAC iliifanya, bali nieleweke kuwa ninatamani Kafulila apewe heshima inayomstahili katika sakata hilo. Yeye ndiye aliyeitwa ngedere, yeye ndiye aliyetishiwa kushitakiwa mahakamani, yeye ndiye aliyelipigania tangu mwanzo hadi mwisho. Krediti nyingi zingepaswa zimrudie yeye. Nikipata majibu ya maswali yangu haya mawili, moyo wangu utatulia kidogo.

Kaka una maelezo mazuri ila umeshindwa kuyajenga kama maswali, kitaalam hapo hakuna swali ulilouliza bali ulikua unatoa maelezo yenye mfumo wa kuhoji.
Zitto katanguliza kusema kua waliojaribu kutaka kuvuruga ni waathirika wa tegeta escrow hapo tayari kishajibu swali lako kwanza moja kwa moja.

Ungeuliza labda akutajie majina ya hao waathirika wa tegeta escrow wanaomvuruga nadhani lingekua swali zuri sana ila wewe unaanza kujijibu mwenyewe kwa kuhusisha chadema au Mahakama ndo zinazomvuruga kana kwamba una majibu ya unachokiuliza.

Swali lako la pili unauliza kitu halafu unatiririka na maelezo ya kutosha sasa sijui ajibu nini, unauliza kama zitto ndie alieibua suala la ESCROW halafu mwisho unajibu mwenyewe ni kafulila.

Kaka unapotaka kujenga hoja au kuuliza swali la msingi weka kwanza mapenzi yako ya chama kando ndipo utakapoweza kufanya hivo.
 
Siasa imemshinda arudi kigoma kwa Sindelela akalime Chikichi.
 
Usinyee kiganja kinachokulisha. Kumbe Zitto bado anaipenda CHADEMA na nje ya CDM si chochote!. Hata kama hukumu ingetolewa mwakani bado Zitto angetoka. Kama kweli shujaa na ni maarufu kuliko Chama analalamika nini? Umezoea kujitajirisha kwa uongo sasa kazi kwako. Karibu kitaani!

hata akija kitaani haitabadilisha maisha yako ila itabadilisha yake .kama kua juu atazidi kua juu tu ukweli ndio huo sio kila mtu ataona life ngumu kitaani
 
ivi swala la escrow ni la kafulila au zito..?
 
Jamani wadau wenzangu,

Nina Swali rahisi sana kwa Mh. Zitto Kabwe.
Subiri kidogo tuu, sasa hivi ZZK atakuja humu jf kujibu!.
Kusema ukweli jf raha!, nimekumbuka yule mwandishi wa habari anayemhoji majeruhi aliyeumia usoni huku atatoka damu.

Mwandishi huku amenyooshea microphone na kumuelekeza camera man, anze kushoot

Mtangazaji: "Tuko hapa eneo la tukio la ajali, tukiwaletea live kutoka jf tv, na hapa mbele yangu kuna majeruhi anatiririka damu, majeruhi... majeruhi huku anamfuata!, unajisikiaje?"

Majeruhi: "unaniona hali yangu ilivyo bado unaniuliza ninajisikiaje?!",

Mtangazaji: "Tuko live hapa, waeleze watazamaji jinsi unavyojisikia"

Majeruhi akamsogelea mtangazaji, akamtwanga ngumi moja ya shibe yule mwandishi!, mwandishi akaanguka chini, mike ikamponyoka!, yule majeruhi akamuelekezea mic mtangazaji, "unajisikiaje?"....waeleze watazamaji wako unavyojisikia!.

Msubirie Zitto akuje!.

Pasco
 
Kwa nini zitto kila kitu akifanya na watu anataka aoneshe kazi ile kafanya yeye peke yake kana kwamba wengine si lolote?
Ivi tujiulize zitto asipokuwepo PAC Ina maana kamati itashindwa kuwasilisha report kisa tu zitto hayupo?
Zitto acha ubinafsi

Hiki ndio kitu kinachomvuruga ZZK...Anaamini yeye ni mtu maalum kuliko watu wote...Ana akili na uwezo kuliko wengine...Kwamba bila yeye mambo yanakwama...

Huu ni ujuha kabisa...Ataondoka na mambo yatakwenda kama kawaida..tena yatakuwa bora zaidi...Alikuwa naibu Katibu CDM ambae haendi ofcn mbona CDM wamezidi kuongeza mitaa na vijiji serikali za mitaa bila yeye...Alikuwa Waziri kivuli wa Fedha mbona Bajeti kivuli ilisomwa na kusifiwa kuliko bajeti zote za nyuma bila yeye....

ZZK hajitambui....na washauri wake kina Pasco amewazidi sana uwezo wa kufikiri, wanamuogopa, wanashindwa kumshauri....
 
Kaka una maelezo mazuri ila umeshindwa kuyajenga kama maswali, kitaalam hapo hakuna swali ulilouliza bali ulikua unatoa maelezo yenye mfumo wa kuhoji.
Zitto katanguliza kusema kua waliojaribu kutaka kuvuruga ni waathirika wa tegeta escrow hapo tayari kishajibu swali lako kwanza moja kwa moja.

Ungeuliza labda akutajie majina ya hao waathirika wa tegeta escrow wanaomvuruga nadhani lingekua swali zuri sana ila wewe unaanza kujijibu mwenyewe kwa kuhusisha chadema au Mahakama ndo zinazomvuruga kana kwamba una majibu ya unachokiuliza.

Swali lako la pili unauliza kitu halafu unatiririka na maelezo ya kutosha sasa sijui ajibu nini, unauliza kama zitto ndie alieibua suala la ESCROW halafu mwisho unajibu mwenyewe ni kafulila.

Kaka unapotaka kujenga hoja au kuuliza swali la msingi weka kwanza mapenzi yako ya chama kando ndipo utakapoweza kufanya hivo.
Nenda ukajifunze maana ya rhetorics, na hasa ujifunze rhtorical questions. Kwa Kiswahili tunaita maswali ya namna hiyo 'balagha' na ni watu wenye uwezo wa kuyauliza maswali hayo wawezao kuyajua maswali hayo. Kama unafikiri mimi nina ushabiki wa vyama, unajidanganya. Nenda kwenye nyuzi zangu zote za huko nyuma utagundua kuwa mie nakosoa mwanasiasa yeyote. Nilishafanya hivyo kwa Slaa, Mnyika, Kikwete, Nchemba na wengine wengi. Tatizo mlio mashabiki wa vyama mmekumbwa na upofu wa kisiasa, hamwezi kuelewa mambo katika uhalisia wake.
 
Back
Top Bottom