Swali: Madhehebu ya wakristo

Swali: Madhehebu ya wakristo

Sijui kama Slaa anasali kwa Gwajima..nimeuliza baada ya kuona picha za Lowassa na Magufuli kwa TB Joshuahalafu tunaambiwa ni RC na Lutheran...nilifikiri ni walokole
Mkuu tukumbuke pia karama za watumishi zinatofautiana, ndio maana utakuja kuona kuwa Mtu kama TB Joshua anatembelewa na watu wengi japokuwa wana madhehebu yao ili kupata suluhisho la kile wanachokitafuta ... Tunajua ana deal zaidi na Prophecy, sio ajabu walikwenda kutafuta unabii juu ya maisha yao ... Pengine ni kwa sababu may be alikosekana mtu wa kuwapa direction ktk madhehebu yao ... Nakumbuka ktk biblia watu wa kawaida, na hata wafalme wa kipagani walikwenda Samaria kutafuta UNABII kwa nabii Elisha ... Sio jambo geni km unapitia maandiko.
 
Naomba tujihadhari na mihemko naomba kuuliza kuwa kujua tu niko curious.

Naomba wenye kukashifu mkae pembeni, lengo ni kuelimishana tu.

Swali langu ni hili;

Mtu anaweza kuwa mlokole na still Mkatoliki au Mlutheri?

Je, tunaweza sema mtu anasali kwa Gwajima au TB Joshua but still Mkatoliki au Mlutheri?

Je, Gwajima yeye binafsi anaweza kuwa Mkatoliki pia au Mlutheri?

Rafiki swali lako linatokana na watu wengi kutoelewa; kwanza nini maana ya neno "mlokole" hili neno haliko kwenye Biblia, asili yake ilikuwa kama neno la dharau kwa wakristo waliokuwa na ujasiri wa kukiri kwamba Yesu amewaokoa. na kama maana ya "ulokole" ndio hiyo basi kwenye madhehebu yote ya kikristo wapo! Wakatoliki wanaitwa Charismatic renewal, kwa walutheri na waprotestant wengine pia wapo, lakini kuna madhehebu mengine wanaitwa mainline pentecostals. ila kwa ufahamu wangu na uzoefu wangu watu wote hao niliowataja wakikutana mahali huwezi kuwatofautisha! Sasa hayo madhehebu yanayotutenganisha wakristo yana historia kutoka ulaya lakini kwa watu waliompokea Yesu kweli kweli huwa hawatofautiani kwenye mambo ya msingi yanayotufanya tuitwe wakristo waliompokea Yesu. I hope my little explanation has helped
 
Ulokole sio dini wala dhehebu

But i am sure ushakutana na walokole ambao sio RC wala lutheran
huduma zote kuanzia ndoa hadi msiba ni hapo hhapo kanisani kwao
na mtu akienda ku attend RC wanamzuia
 
Rafiki swali lako linatokana na watu wengi kutoelewa; kwanza nini maana ya neno "mlokole" hili neno haliko kwenye Biblia, asili yake ilikuwa kama neno la dharau kwa wakristo waliokuwa na ujasiri wa kukiri kwamba Yesu amewaokoa. na kama maana ya "ulokole" ndio hiyo basi kwenye madhehebu yote ya kikristo wapo! Wakatoliki wanaitwa Charismatic renewal, kwa walutheri na waprotestant wengine pia wapo, lakini kuna madhehebu mengine wanaitwa mainline pentecostals. ila kwa ufahamu wangu na uzoefu wangu watu wote hao niliowataja wakikutana mahali huwezi kuwatofautisha! Sasa hayo madhehebu yanayotutenganisha wakristo yana historia kutoka ulaya lakini kwa watu waliompokea Yesu kweli kweli huwa hawatofautiani kwenye mambo ya msingi yanayotufanya tuitwe wakristo waliompokea Yesu. I hope my little explanation has helped

Asante.....umenisaidia....
 
My dear
Ulokole sio dini wala dhehebu.
Ni hali ambayo baadhi ya watu hujitangazia kuwa wako ktk hali tofauti ya kiimani kuliko wengine. If that is the case then hata mkatoliki au mlutheri anaweza kujiita mlokole. Waingereza wanawaterm as born again Christians. Who is not is the matter of debate.

Haya makanisa ya watu mara nyingi ni ministries yaani vituo vya huduma maalumu. Wengine inakuwa huduma ya kufunguliwa aka delivarence kama SCOAN.
Madhehebu mara nyingi yanakuwepo kila sehemu lkn ministries ndio utasikia kwa kakobe.

Kama hivyo ndivyo mkatoliki anaweza kwenda kwenye huduma say kwa mwakasege lkn kama ni jumapili basi anatakiwa aanze kushiriki misa kanisani kwake.

Nilishaenda kwa T.B Joshua, kwa Mwakasege, na huduma mbali mbali Emaus Catholic Charismatic Center

Umejibu kama nielewavyo mimi.

Nimeona si vyema nikusome alafu nisikusalimu.
 
But i am sure ushakutana na walokole ambao sio RC wala lutheran
huduma zote kuanzia ndoa hadi msiba ni hapo hhapo kanisani kwao
na mtu akienda ku attend RC wanamzuia

Ni madhehebu ya kipentecoste hayo
 
So ni sawa kwa mkatoliki kuhudhuria ibada kwa Gwajima au TB Joshua?
na still akawa mkatoliki?
Hizo ibada za huko hazitambuliki lakini pia hazijawekewa kipingamizi.
1. Kutambulika:
Utahudhuria tu lakini kanisa la RC halitahesabu kama umesali. Ni kama vile rais mkatoliki anapoenda kuhudhuria ibada ya kusimikwa kwa askofu wa dhehebu la kilokole, hapo anakuwa anawafurahisha tu wenyeji lakini kwa RC anakuwa hajajipa baraka zozote lakini hautachukuliwa hatua zozote zaidi ya kushauriwa.
2. Kuwekewa kipingamizi:
Ukihudhuria ibada zilizotolewa tamko la kuwekewa kipingamizi unakuwa umeasi, na hapo ndipo RC itakuchukulia hatua zikiwemo za kufutiwa/ kufungiwa sakramenti zote au baadhi. Kama unakumbuka 2010 baada ya uchaguzi, Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga liliwafutia sakramenti waumini wake kadhaa walioshiriki maandamano ya CCM yaliyohusisha kuukashifu Utatu Mtakatifu. Hapo walifungiwa kwa kuwa mafundisho yanasema kumkashifu Roho Mtakatifu ni dhambi kubwa sana, na wao walishiriki ibada hiyo ya kukashifu, bahati nzuri hata Anglican na Lutheran wakasema hata nao hawatawapokea waumini hao
 
Sijui kama Slaa anasali kwa Gwajima..
nimeuliza baada ya kuona picha za Lowassa na Magufuli kwa TB Joshua
halafu tunaambiwa ni RC na Lutheran...nilifikiri ni walokole

Ulokole sio dini wala dhehebu

Ewaaaaa.....

Ni kama tunavyoenda uwanja wa Taifa kuishabikia Taifa Stars kwa pamoja mimi na wewe... Uzalendo (Imani moja-ulokole)

Na kama siku nyingine tunaenda uwanja wa taifa wewe unaishabikia Yanga na mimi naishabikia Simba (wachezaji ni walewale wanaoichezea Taifa Stars) - Ushabiki (madhehebu)

Mi hata sijui kama nimeeleweka...
 
Sijui kama Slaa anasali kwa Gwajima..
nimeuliza baada ya kuona picha za Lowassa na Magufuli kwa TB Joshua
halafu tunaambiwa ni RC na Lutheran...nilifikiri ni walokole

Oky either way, katoliki inafundisha kushika Utatu mtakatifu, sakramenti na nguzo zake inatofautiana sana na makanisa mengine hasa haya ya " Mzee wa Upako", " Ufufuo wa Uzima" n.k
nikionacho ni watu kuappeal kwenye mirracles, Imani ya katoliki ni Imani kubwa, Imani yenye kuamini bila kuona. Well kujibu swali lako yes watakua ni kondoo waliopotea.
 
Nijuavyo mimi, madhehebu yote ya kikristu, ukiondoa Roman Catholic, yanaitwa Protestants. Sasa Ukiwa Mkatoliki (kama mimi) hauwezi at the same time ukawa unaprotest against Catholic church, yaani a protestant. Sana sana utakuwa muhudhuriaji tu kwa upande mmojawapo. Hili jibu ni kwa mujibu wa mimi na linahusu Ukatoliki vs Ulokole. Kuhusu Ulokole vs other protestant churches watakuja wajibu wenyewe

Upo sawa..
 
Swala ni wenye 'MOYO SAFI' wala sio udhehebu. Ukimkiri na kumpokea kuwa bwana na mokozi wako(ukaacha njia zako mbaya) utakuwa umeokoka, tafuta penye mafundisho mazur go ahead

Kuna kanisa lenye mafundisho mabaya..??
 
Ni ngumu asee lakn unaweza kusali tu kanisa lolote inategemea na imani yako lakini kwa mkatoliki kwlkwl akihudhuria ibada za kilokole ataona utofauti mkubwa lakini pia kwa mlokole yoyote kwlkwl akihudhuria ibada za RC ataona utofauti
my intake: wengi wa waumini wa kilokole wameanzia RC
 
So ni sawa kwa mkatoliki kuhudhuria ibada kwa Gwajima au TB Joshua?
na still akawa mkatoliki?

Biblia na neno la mungu ni lilelile hamna tatizo ukaenda sali catholic,protestant au pentecoste labda tofaut ya sala
 
Back
Top Bottom