RAGNAR LOTH
JF-Expert Member
- Oct 11, 2016
- 698
- 1,589
Dhana ya nzi kufia kwenye kidonda ni Utaahira/ Mapenzi / Uhaba wa vidume, wanawake/ Uvumilivu / Ushika dini kupindukia / Kutojiamini ama ni nini?
Ushawahi kukutana na familia/ uhusiano uliogubikwa na ugomvi na migogoro isiyoisha?
Yumkini mwanamume ndiye chanzo ama mwanamke ndiye chanzo cha maugomvi yasiyoisha kila siku lkn unakuta bado wako pamoja. Unakuta kidada kizuri kimejikondea kwa mawazo na manung'uniko yasiyoisha. Ama jamaa kaisha hadi tunamshangaa kijiweni kisa mikasa ya mahusiano. Kupenda kupo lkn sio kila kitu katika maisha, Mapenzi ni sehemu tu ya maisha, dhana ya maisha sio mapenzi pekee wanandugu.
Kwa mtazamo wangu : Jifunzeni kuyapa kisogo baadhi ya mambo ktk maisha, Jifunzeni kuanza upya ktk baadhi ya mambo, Mkubali kushindwa ktk baadhi ya mambo. Acheni kufunika nyota zetu zising'are kwa kukumbatia yanayokurudisheni nyuma kwa sababu tu neno mapenzi lilishakuepo
Wangapi waliamua kuacha yaende ? Hutakua wa kwanza ktk ulimwengu, wengi walishafanya. Waliachana na vizingiki wakaanza upya wakafika mbali ktk kila affair kwenye maisha yao.
Siwashawishi mvunje mahusiano yenu lkn ikibidi kufanya hivyo ongeeni na dhamiri zenu ziwasaidie kufanya maamuzi.
Mtalia sana, mtatembea sana kwa waganga kuwabadili wenzi wenu, mtasubiri sana wenzi wenu wabadilike, mtawawekea vikao 100 kidogo, If he/she is not to change you'll end up getting stuck in the dark of despair, sorrow, and pain till we burry you.
Learn to let some things go in life.
Ushawahi kukutana na familia/ uhusiano uliogubikwa na ugomvi na migogoro isiyoisha?
Yumkini mwanamume ndiye chanzo ama mwanamke ndiye chanzo cha maugomvi yasiyoisha kila siku lkn unakuta bado wako pamoja. Unakuta kidada kizuri kimejikondea kwa mawazo na manung'uniko yasiyoisha. Ama jamaa kaisha hadi tunamshangaa kijiweni kisa mikasa ya mahusiano. Kupenda kupo lkn sio kila kitu katika maisha, Mapenzi ni sehemu tu ya maisha, dhana ya maisha sio mapenzi pekee wanandugu.
Kwa mtazamo wangu : Jifunzeni kuyapa kisogo baadhi ya mambo ktk maisha, Jifunzeni kuanza upya ktk baadhi ya mambo, Mkubali kushindwa ktk baadhi ya mambo. Acheni kufunika nyota zetu zising'are kwa kukumbatia yanayokurudisheni nyuma kwa sababu tu neno mapenzi lilishakuepo
Wangapi waliamua kuacha yaende ? Hutakua wa kwanza ktk ulimwengu, wengi walishafanya. Waliachana na vizingiki wakaanza upya wakafika mbali ktk kila affair kwenye maisha yao.
Siwashawishi mvunje mahusiano yenu lkn ikibidi kufanya hivyo ongeeni na dhamiri zenu ziwasaidie kufanya maamuzi.
Mtalia sana, mtatembea sana kwa waganga kuwabadili wenzi wenu, mtasubiri sana wenzi wenu wabadilike, mtawawekea vikao 100 kidogo, If he/she is not to change you'll end up getting stuck in the dark of despair, sorrow, and pain till we burry you.
Learn to let some things go in life.