Swali. Je baada ya kuvunjwa bunge, mawaziri wanaendelea?

Swali. Je baada ya kuvunjwa bunge, mawaziri wanaendelea?

Doto12

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2023
Posts
752
Reaction score
1,338
Kwa mujibu wa taratib naomba kujua ukomo wa ubunge, ni baada ya kuvunjwa bunge. Mtu anakuwa sio mbunge tena, je uwaziri unakaa pembeni? Tukumbushane wajuz wa mambo.
 
Nikajua anabaki rais,pm na makamu wa rais
 
Anaendelea ki vipi wakati uwaziri unatokana na ubunge?
Mbona Rais anabaki? kinachofuatwa ni katiba, kwani PM naye hatakuwepo na ulinzi utaondolewa? ni kati ya hovyo sn hii ndiyo maana Rais ni mgombea na anaweza kuteua hata makatibu wakuu
 
Tutunze majibu,tusije tukauliza tena baada ya miaka 5 ijayo tukiwa na uzima na uhai.
 
Kilichovunjwa ni Bunge na wala siyo ubunge wao.

Ubunge na uwaziri unakoma au unapaswa kukoma pale wengine wanapokuwa wamechaguliwa na kuapishwa kwa rais.

Kama ambavyo mbunge mteule hana mamlaka ya kuhusika na masuala nyeti ya Bunge hadi aapishwe, ndivyo ilivyo pia kwa mbunge anayeondoka madarakani (baada ya Bunge kuvunjwa).
 
Na uwaziri unakoma wizara zinaendeshwa na makatibu wakuu
Na mimi ndo nachojua.Bunge likivunjwa mawaziri wanakoma na ndinga zote zinarejeshwa pale kwa mwenywe.wizara zinaongozwa na makatibu wakuu
 
Baada ya Uchaguzi Mkuu, Mawaziri wote hawana kazi.
Not true. Soma Katiba ya Tanzania—Ibara ya 51(3) [kuhusu Waziri Mkuu] na Ibara ya 57(2)(f) [kuhusu mawaziri na manaibu wao]. Vibarua vyao vinayeyuka immediately before the president-elect takes oath of office! That means wanakuwa mawaziri mpaka dakika chache kabla ya Rais Mteule kuapishwa.
 
Wizara zinaendeshwa na makatibu wakuu hata kwny hotuba yke Majaliwa alisistiza hili wawe wangalifu na wafate maelezo ya miradi iliobakia walioambiwa na mawaziri wao
 
Back
Top Bottom