Sumaye: Rais ajaye apambane na madawa ya kulevya!

Sumaye: Rais ajaye apambane na madawa ya kulevya!

n00b

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2008
Posts
1,013
Reaction score
2,684
Sumaye ameipiga kijembe serikali kwa kusema mlinzi na mtetezi wa katiba wa kwanza ni rais wa nchi akifuatiwa na viongozi wengine.

"Ndivyo wanavyoapa viapo vyao vya uaminifu kwa nchi. Kwa hiyo katiba nzuri lazima iambatane na serikali adilifu inayojali maslahi ya umma na rais anayeiongoza awe mchapakazi na anayejali maslahi ya umma mpana na siyo maslahi yake binafsi, ya watoto wake au ya marafiki zake.

"Yeye mwenyewe awe na uadilifu usiotiliwa mashaka ya aina yoyote na apigane vita vya wazi dhidi ya rushwa, ufisadi, madawa ya kulevya na maovu mengineyo katika jamii. Tukifanikiwa katika yote hayo, basi tutakuwa tumevuna na kuyala matunda mema ya katiba nzuri."

Kayasema akiwa Mzumbe Campus - Mbeya
 
kwa hiyo rais wa sasa ameshindwa. ok acha tusubiri rais ajaye apambane na rushwa.madawa ya kulevya etc
 
Serikali iliyopo toka 2010 ni transitional government.
 
JK alishasema anayo orodha ya wauza unga na akaonya kama kawaida yake kuwa waache mchezo huo. Tatizo huyu Rais wetu ni msemaji sana na sio mtekelezaji. Msishangae na tambo zake hizi za kila siku lakini Kagame akatuchapa. Mie naogopa sana porojo za Jakaya kiukweli. Nchi haiendeshwi hivyo.

By the way, Sumaye si ndio huyu alisema mfanyabiashara yoyote akitaka kufanikiwa lazima ajiunge kwanza na CCM????
 
Najua wote tunapenda kusikiliza na kuzungumzia ndoto za alinacha, Hakuna cha Sumaye wala Jk hapo, Je Sumaye kesha rudisha zile eka 600 alizopora Morogoro, na ukizungumzia madawa ya Kulevya na Ufisadi hapo CCM ndio wanaongoza na hakuna mpiganaji wa kweli kwa sababu uongozi wanapata kwa kutumia pesa ambazo Chanzo chake hakuna anayejua mtu hana biashara yo yote ya wazi ila kila anachangia hapa 100m, Kule 400m, pale 510, anabiashara gani na hizo pesa yeye atarudisha vipi Tuangaliye, ,,,,,!!! Tena sasa hivi ndio wanajitahidi kweli kweli wanataka kuteka Makanisa na Misikiti
 
Sumaye ameipiga kijembe serikali kwa kusema mlinzi na mtetezi wa katiba wa kwanza ni rais wa nchi akifuatiwa na viongozi wengine.

"Ndivyo wanavyoapa viapo vyao vya uaminifu kwa nchi. Kwa hiyo katiba nzuri lazima iambatane na serikali adilifu inayojali maslahi ya umma na rais anayeiongoza awe mchapakazi na anayejali maslahi ya umma mpana na siyo maslahi yake binafsi, ya watoto wake au ya marafiki zake.

"Yeye mwenyewe awe na uadilifu usiotiliwa mashaka ya aina yoyote na apigane vita vya wazi dhidi ya rushwa, ufisadi, madawa ya kulevya na maovu mengineyo katika jamii. Tukifanikiwa katika yote hayo, basi tutakuwa tumevuna na kuyala matunda mema ya katiba nzuri."

Kayasema akiwa Mzumbe Campus - Mbeya

Chadema wake up, make a blow;

CCM sasa hivi hoi!!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mmh.! Yaani hata wenzake wameshamkatia tamaa Jk? Si ccm mwenzao lakini
 
Sumaye ameipiga kijembe serikali kwa kusema mlinzi na mtetezi wa katiba wa kwanza ni rais wa nchi akifuatiwa na viongozi wengine.

"Ndivyo wanavyoapa viapo vyao vya uaminifu kwa nchi. Kwa hiyo katiba nzuri lazima iambatane na serikali adilifu inayojali maslahi ya umma na rais anayeiongoza awe mchapakazi na anayejali maslahi ya umma mpana na siyo maslahi yake binafsi, ya watoto wake au ya marafiki zake.

"Yeye mwenyewe awe na uadilifu usiotiliwa mashaka ya aina yoyote na apigane vita vya wazi dhidi ya rushwa, ufisadi, madawa ya kulevya na maovu mengineyo katika jamii. Tukifanikiwa katika yote hayo, basi tutakuwa tumevuna na kuyala matunda mema ya katiba nzuri."

Kayasema akiwa Mzumbe Campus - Mbeya

Ningemwona wa maana kama angesema wazi kuwa "kama Raisi ameshindwa kutekeleza kiapo alichokula cha uaminifu kwa Nchi ni bora akaachia ngazi kwa hiari yake"! Kwa hali ilivyo mbaya kutokana na biashara hii haramu hatuwezi kusubiria Raisi ajae, ni lazima hatua madhubuti zichukuliwe sasa! 2015 ni mbali sana na sifa ya Taifa itakuwa imepotea kabisa!
 
Unga utakuja acha watu na aibu hadharani
 
JK alishasema anayo orodha ya wauza unga na akaonya kama kawaida yake kuwa waache mchezo huo. Tatizo huyu Rais wetu ni msemaji sana na sio mtekelezaji. Msishangae na tambo zake hizi za kila siku lakini Kagame akatuchapa. Mie naogopa sana porojo za Jakaya kiukweli. Nchi haiendeshwi hivyo.

By the way, Sumaye si ndio huyu alisema mfanyabiashara yoyote akitaka kufanikiwa lazima ajiunge kwanza na CCM????

JK si mswahili wa bagamoyo ndo maana maneno 90% matendo 10%
 
Chadema wake up, make a blow;

CCM sasa hivi hoi!!

CCM ilikufa 2000 baada ya Azimio la Zanzibar lililoua Azimio la Arusha ikumbukwe azimio hili ndilo lililozaa uadilifu, maadili ya utawala, sera za kiuchumi na misingi ya uongozi ndani ya TANU na baadae CCM....! baadaya kulizamisha bahari ya Hindi, Ukazaliwa utawala wa kiimla unaosimamiwa na DOLA ... ! sasa hivi ipo ruksa ya DOLA kujiamulia mambo bila ridhaa ya wananchi ... Leo jeshi la wananchi limekua jeshi la kutoa matamko dhidi ya chama cha siasa? Jeshi la polisi linaamini wavaaji wa "safari suits" ni CHADEMA ....Leo hii waziri mkuu anaamini maandamano ni fujo ilhali yeye ni Mwanasheria! isitoshe ameapa kuitumikia katiba amabayo ameamua kupambana nayo kwa kuruhusu risasi zitumike kuzuia utekelezaji wa katiba hiyo hiyo...! Hivi sasa ili kukihuisha CCM .... DOLA imejivika U-CCM na ndio inayopambana na CDM na siyo CCM, Hivyo DOLA hujiita CCM katika siasa na kubakia km DOLA ki IMLA....kazi kubwa ya CDM ni jinsi yakupambana na DOLA kisiasa ili hatimaye kuiendesha DOLA hiyo hiyo kurudia majukumu yake ya kutenda haki kwa kila raia bila ya kujali itikadi...Watanzania wengi haswa Wanawake hawajui tofauti ya DOLA na CCM na ndio maana hawachoki kukipigia kura wakidhani ndio Utiifu kwa DOLA yao... Na hata juhudi yaCCM kukichora CDM km kama chama cha magaidi ni ili wawapate wanawake kwani wanatabia ya kujitenga na fujo
 
Sumaye ameipiga kijembe serikali kwa kusema mlinzi na mtetezi wa katiba wa kwanza ni rais wa nchi akifuatiwa na viongozi wengine.

"Ndivyo wanavyoapa viapo vyao vya uaminifu kwa nchi. Kwa hiyo katiba nzuri lazima iambatane na serikali adilifu inayojali maslahi ya umma na rais anayeiongoza awe mchapakazi na anayejali maslahi ya umma mpana na siyo maslahi yake binafsi, ya watoto wake au ya marafiki zake.

"Yeye mwenyewe awe na uadilifu usiotiliwa mashaka ya aina yoyote na apigane vita vya wazi dhidi ya rushwa, ufisadi, madawa ya kulevya na maovu mengineyo katika jamii. Tukifanikiwa katika yote hayo, basi tutakuwa tumevuna na kuyala matunda mema ya katiba nzuri."

Kayasema akiwa Mzumbe Campus - Mbeya

Akimaliza hapo ataitwa ikulu akadadavue alikua anamaanisha nini.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
CCM ilikufa 2000 baada ya Azimio la Zanzibar lililoua Azimio la Arusha ikumbukwe azimio hili ndilo lililozaa uadilifu, maadili ya utawala, sera za kiuchumi na misingi ya uongozi ndani ya TANU na baadae CCM....! baadaya kulizamisha bahari ya Hindi, Ukazaliwa utawala wa kiimla unaosimamiwa na DOLA ... ! sasa hivi ipo ruksa ya DOLA kujiamulia mambo bila ridhaa ya wananchi ... Leo jeshi la wananchi limekua jeshi la kutoa matamko dhidi ya chama cha siasa? Jeshi la polisi linaamini wavaaji wa "safari suits" ni CHADEMA ....Leo hii waziri mkuu anaamini maandamano ni fujo ilhali yeye ni Mwanasheria! isitoshe ameapa kuitumikia katiba amabayo ameamua kupambana nayo kwa kuruhusu risasi zitumike kuzuia utekelezaji wa katiba hiyo hiyo...! Hivi sasa ili kukihuisha CCM .... DOLA imejivika U-CCM na ndio inayopambana na CDM na siyo CCM, Hivyo DOLA hujiita CCM katika siasa na kubakia km DOLA ki IMLA....kazi kubwa ya CDM ni jinsi yakupambana na DOLA kisiasa ili hatimaye kuiendesha DOLA hiyo hiyo kurudia majukumu yake ya kutenda haki kwa kila raia bila ya kujali itikadi...Watanzania wengi haswa Wanawake hawajui tofauti ya DOLA na CCM na ndio maana hawachoki kukipigia kura wakidhani ndio Utiifu kwa DOLA yao... Na hata juhudi yaCCM kukichora CDM km kama chama cha magaidi ni ili wawapate wanawake kwani wanatabia ya kujitenga na fujo

Kwa hiyo wana instill fear kwa wanawake ili wao wa provide security? Halafu ndo wapate kura nyingi?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Sumaye chunga sana!hata kama ni haki yako Kikatiba utashangaa ukikatiwa mrija wako wa posho na stahiki!sijui utapiga kelele au utakimbia nchi?usichezee walioshika mpini!nakushauri tu maneno mazuri sana hayo lakini watawala hawatayapenda!watakusambaratisha!unaweza kuwa mzalendo mzuri sana ila tunakuonea huruma!wakijibu hao na wapambe wao itakuwa tabu!
 
Aseme mara ngapi tena Mkuu!!!? Ndio kishasema wazi kwamba DHAIFU uongozi wa nchi umemshinda, hana hata moja analoliweza zaidi ya kuchekacheka na uVDG.


Ningemwona wa maana kama angesema wazi kuwa "kama Raisi ameshindwa kutekeleza kiapo alichokula cha uaminifu kwa Nchi ni bora akaachia ngazi kwa hiari yake"! Kwa hali ilivyo mbaya kutokana na biashara hii haramu hatuwezi kusubiria Raisi ajae, ni lazima hatua madhubuti zichukuliwe sasa! 2015 ni mbali sana na sifa ya Taifa itakuwa imepotea kabisa!
 
Huyu Sumaye kiakili bado hajakomaa kabisa.
Kila siku rais ajaye tu, wakati tuna rais sasa, kwanini asimshinikize Kikwete apambane na Ufisadi na Madawa ya kulevya?

Sumaye anazungumza kwa woga na unafiki mkubwa sana, halafu hapo hapo anataka watanzania waje wampe Urais!!
Sumaye akiulizwa kama ana mpango wa urais, anaogopa kusema na kubaki kuumauma maneno tu, mimi simkubali kabisa huyu jamaa, bora hata Fisadi Lowassa kuliko huyu Sumaye.

CCM tutaendelea kupelekeshwa ile mbaya na wanasiasa wa CHADEMA ambao wao hawamumunyi maneno, kila jambo ovu wanalisema hadharani kwa uhakika na ujasiri bila woga wala nini.
 
Ukishaona wakubwa wanasemana ujue mambo sio mambo. Sumaye usijali, atatoa tamko soon. List anayo anaiatamia kwanza, ataitotolesha soon.
 
Rais akitoka CHADEMA anaweza kabisa kumaliza tatizo hilo la Madawa ya kulevya siyo CCM.
Nasema kwa kujiamini maana wauzaji wanafahamika mpaka wanapoishi, vyombo vya ulinzi vinajua taarifa zao.
Ushiriki wa watawala kwenye scandal hii kumetufikisha hapa mahali tulipo maana utamkamata nani? Wahusika wapo madarakani, wanawatuma vijana wetu wakikamatwa huko nje wanakuja na vichekesho vya kusaini mikataba ya kubadilishana wafungwa, mara kutoa gesi ili mtoto asinyongwe.
 
Hii kauli ni mtego mkali sana kwa rais wa sasa, ina maana wazee wenzie wamemkatia tamaa. Au kwakuwa First Son anapiga hiyo biashara??
 
Back
Top Bottom