Sumaye haeleweki anachosimamia

Jamaa analia lia kweli sasa kama rais analia lia atawezaje kuongoza nchi

Miaka 20 bungeni hajasikika akikemea rushwa wala ufisadi halafu leo eti oooh naunda mahakama ya mijizi; jeuri hiyo ataitoa wapi kama sio porojo za akina mjomba megawati. Watu wameikataa katiba ya wananchi yenye maadili yanayokomesha ufisadi na kulinda rasilimali za taifa halafu leo wanaibuka na porojo hizi. Eti ooh mama ntilie wasisumbuliwe, ooh machinga ni muhimu nitawapa benki na mikopo; unajua hawa jamaa wanatuona sisi ni punguani tangu lini katetea wanyonge bungeni? waliotutetea miaka yote huku wanazomewa leo wanaonekana hawajui kazi anayejua kazi ni huyo wa kupiga domo; inawezekana akili zetu sio nzuri inafaa tupimwe kuwaendekeza watu kama hawa na kuwakenulia meno
 
huyu jamaa amejidhalilisha sana,amekuwa icon ya unafiki na uchu wa madaraka,atajuta sana baada ya october

Kati ya Sumaye na John Pombe Makufuli anayetaka kuingia Ikulu kwa kupiga push ups na kucheza rhumba kwenye jukwaa la kisiasa huku akikurupua ahadi za kila rangi na majigambo milioni kidogo ni nani mwenye uchu wa madaraka?..CCM mpaka wametamka kupitia Kampeni Meneja wao Abdallah Bulembo kuwa Nanukuu “Serikali imefanya makosa mengi na Chama Cha Mapinduzi kimefanya makosa mengi lakini hakitofanya kosa la kuruhusu chama pinzani kuingia Ikulu,” Ni nani mwenye uchu wa MADARAKA?
 

Ndio siasa hizo, unalialia nini sasa ye angekaa kimya watu wangemuheshimu sasa huu mpira unaitwa chandimu, pole.
 
Kenda kuungana na wezi wenzie. Hayo ndo yaliitwa magamba sasa yamevuka na ccm imebaki safiii. ccm oyeeeeeeeeeeeee!

Chenge,Ngeleja, Prof. Tibaijuka, Prof. Muhongo, Mwambalaswa Mwakyembe na Mabehewa ya kupeperushwa na upepo na wengine wengi je? Ufisadi umeisha ccm?
Nape na Mwigulu walikamatwa kwanini na Takukuru?
 
Miaka 53 gani niliodanganywa wakati ccm imeanza mwaka 1977 na mimi nimezaliwa 1980! sasa hata hesabu hujui unapelekwa tu kama ling'ombe! Lowasa out.....!

Akili ziro kabisa,
CCM inatokana na TANU na ASP tangia uhuru mfumo wa utawala ni mmoja tu tena nenda Lumumba utaona bango linakwambia hapa ndipo ilipozaliwa TANU 1954 Sasa ni zaidi ya miaka 61 bado hakizeeki?
 
Sumaye arudishe mahekari ya ardhi kule mvomero na nyumba zaidi ya 5 alizonunua kwa bei ya kutupa, na atuambie miaka 10 Ya u PM wake alishindwaje kutukomboa maskini badala yake akapora mali na ardhi za wanyonge!?

Wewe utakuwa Unamsema Mzee Mwinyi maana ndiye mwenye Shamba Kubwa sana pale Mvomero
 

Akili ndogo haiwezi kuifundisha akili kubwa hata siku Moja. Una Elimu gani mwenzangu?
Kazi ya Serikali ni kutengeneza Sera ambazo zitanufaisha Wananchi.
Kwa Mfano Kenya maBenk yanakuja na mbinu mpya kila siku ya kuwakopesha fendha wakenya wakati hapa ukitaka kukopa uweke bank pesa kwanza miezi sita hadi mwaka tutaendelea kweli?
hauwezi kuwa Tajiri katikati ya dimbwi la Masikini haiwezekani.
Sijui wewe unafurahia pesa za wavija jasho zinavyoliwa na wachache kama vile Tegeta Escrow?
sijui unafurahia kwenda kilomita 7kwa masaa manne?
Sijui unafurahia kwenda Hospital ya Umma usikute Dawa?
Sijui unafurahia Kukosa umeme unapouhitaji?
Sijui unafurahia watoto kukaa chini shuleni?
Sijui unafurahia Mkulima kunyonywa mazao yake na kukopwa?
Una nafasi gani katika wanaowadhurumu watanzania mpaka unatetea hivyo?
 
Haina uhusiano na hoja yangu kama vipi anzisha uzi wa kudai hizo pesa, mi namwambia huyu mwizi Sumaye arudishe ardhi za wanyonge.

Nilidhani unazungumzia Ufisadi in General kumbe unamzungumzia mtu,
Wewe ni hatari kuliko ukimwi virus vyako havina mbadala.
Kama ni kurudisha au kuondoa ufisadi nadhani tungeanza na wa Tegeta Escrow maana tuna mtaji wa Ushahidi wa watu waliokiri.
 

Hakuna aliyekuza Uchumi kwa mfumo wa ccm wewe.
Vipi maana hueleweki kabisa.
Benja alimwaga Ngano ya Bakhressa hii ni.kukuza uchumi?
 

Umeweka blah blah nyiiingi sana lakini ilichokusaidia ni kuanika mapungufu makubwa uliyonayo. Ndio maana mwanzoni Nilikueleza kuwa mtu mwenye ufinyu wa mawazo huwa anadhani kuwa kile anachokifahamu ndicho kila kitu. Hizo sentensi tano ulizoziandika ungezisummerise kwa neno moja tu, mfumo au mazingira.
Ndio maana basi, hata mwanzoni Nilihoji kuwa pamoja na yote unayodai kuhusu mfumo wa CCM, hao waliofanikiwa, waliweza vipi? Hilo ndilo swali la msingi hapa.
 
Hakuna aliyekuza Uchumi kwa mfumo wa ccm wewe.
Vipi maana hueleweki kabisa.
Benja alimwaga Ngano ya Bakhressa hii ni.kukuza uchumi?

Ina maana ndesamburo sio tajiri? Mbowe sio tajiri? Sijagusia swala la uchumi kama nchi, nimezungumzo ukombozi wa kiuchumi kwa watu na ndio maana tunazungumzia watu.
 

CCM haifai hata kwa nini.
Una Elimu ya Kudesa wewe ndiyo maana hata upeo wako wa kuelewa ni mdogo sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…