GE2025 Sumaye awaonya wanachama wa CCM Manyara wasibweteke Uchaguzi Mkuu

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,437
Reaction score
5,235
Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye, amewataka wanachama wa CCM Mkoa wa Manyara kutobweteka kuwa wagombea wao watashinda bila kufanya kampeni na kujitokeza kupiga kura Oktoba 29 mwaka huu.

Fredrick Sumaye, ambaye kwa sasa ndiye mratibu wa kampeni za uchaguzi za CCM mikoa ya Kanda ya Kaskazini ya Arusha, Tanga, Kilimanjaro na Manyara, ametoa wito huo katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi za CCM Mkoa wa Manyara zilizofanyika katika viwanja vya Motel Papa mjini Babati.

Amesisitiza kila balozi wa nyumba anayetokana na chama hicho kuhamasisha wapiga kura katika eneo lake ili kukipa ushindi chama hicho, kwa kuwa katika ushindani wa kisiasa mshindi wa uchaguzi hutangazwa baada ya kura kuhesabiwa. Hivyo akasema ni muhimu wanachama wa CCM wakajitokeza kupiga kura Oktoba 29 mwaka huu.

Your browser is not able to display this video.
 
Mzee huyu anazeeka vibaya. Hajui kuwa tume ya uchaguzi Iko chini ya Abdul? Sasa mama Abdul kwann asishinde?
 
Wasibweteke, kwani wanashindana na nani? Au mizengwe ya wenyewe kwa wenyewe 🤔
 

Halafu huyu naye slikuwa anausaka Urais. Mzee mzima anaendeleza Uchawa. Yaani Sumaye ni mtu wa kumnyenyekea Maza.... Sometimes ni kweli Watanzania hatunaga standards.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…