SUMATRA yawataka madereva wa mabasi kusitisha mgomo wao hapo kesho

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa nchi Kavu (SUMATRA) kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama barabarani pamoja na Chama cha Wamiliki wa mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani (lTABOA) imewataka madereva kusitisha mara moja mgomo wa mabasi ambao umetangazwa kufanyika siku ya kesho nchi nzima.

Kamanda wa Polisi kikosi cha Usalama barabarani Fortunatus Musilimu amesema waliopanga kufanya mgomo waache kwani suala lao lipo mahakamani tayari.

"Niwaombe wote wanaosambaza vipeperushi vya kutangaza mgomo huo waache hili suala tayari lipo mahakamani na kuhusu hizo kero zinazungumzika hakuna sababu ya madereva kufanya mgomo utakaoleta kero kwa wananchi wasiona hatia" amesema.

"Tayari hatua za awali za kuwafuatilia wanaochochea mgomo huo zimeanza kuchukuliwa tunaamini kesho huduma ya usafiri zitatolewa tena zitatolewa kwa kiwango cha juu zaidi" ameeleza Kamanda Fortunatus Musilimu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Madereva wa mabasi yaendayo Mikoani, Shabani Mdemu amesema kuwa, "Ni kweli vijana wametishia kugoma kesho lakini mimi kama kiongozi wao nimewaomba kusitisha mgomo huo naamini watanisikia,l. Ni kweli kuna tatizo Morogoro Sumatra tunaomba mfuatilie kama msipofuatilia hili tatizo vijana hawewezi kuvumilia hali hii"
 
"Tayari hatua za awali za kuwafuatilia wanaochochea mgomo huo zimeanza kuchukuliwa tunaamini kesho huduma ya usafiri zitatolewa tena zitatolewa kwa kiwango cha juu zaidi" ameeleza Kamanda Fortunatus Musilimu.
Hapa sasa ni vitisho,. Sheria za kazi duniani kote zinaruhusu migomo cha msingi ifuate taratibu, sasa kama wamefuata taratibu je!? Ina maana wao hawajui kuwa 'yanazungumzika' mpaka wakafikia hatua hii!?
 
Mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa nchi Kavu (SUMATRA) kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama barabarani pamoja na Chama cha Wamiliki wa mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani (lTABOA) imewataka madereva kusitisha mara moja mgomo wa mabasi ambao umetangazwa kufanyika siku ya kesho nchi nzima.

Kamanda wa Polisi kikosi cha Usalama barabarani Fortunatus Musilimu amesema waliopanga kufanya mgomo waache kwani suala lao lipo mahakamani tayari.

"Niwaombe wote wanaosambaza vipeperushi vya kutangaza mgomo huo waache hili suala tayari lipo mahakamani na kuhusu hizo kero zinazungumzika hakuna sababu ya madereva kufanya mgomo utakaoleta kero kwa wananchi wasiona hatia" amesema.

"Tayari hatua za awali za kuwafuatilia wanaochochea mgomo huo zimeanza kuchukuliwa tunaamini kesho huduma ya usafiri zitatolewa tena zitatolewa kwa kiwango cha juu zaidi" ameeleza Kamanda Fortunatus Musilimu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Madereva wa mabasi yaendayo Mikoani, Shabani Mdemu amesema kuwa, "Ni kweli vijana wametishia kugoma kesho lakini mimi kama kiongozi wao nimewaomba kusitisha mgomo huo naamini watanisikia,l. Ni kweli kuna tatizo Morogoro Sumatra tunaomba mfuatilie kama msipofuatilia hili tatizo vijana hawewezi kuvumilia hali hii"

Mimi siyo dereva ila nakiri kuwa Morogooro pale Msamvu kuna kero haswa wale vijana wa SUMATRA, hawana majibu mazuri hafu, hafu wamekaa kibabe sana. Vilevile Sumatra faini zenu ni za kuwakomoa madereva 250,000 kwa kosa moja kwa dereva anayepewa posho ya Tsh 30,000/ kwa siku ni uonevu,
 
Eti wanaosambaza ujumbe kukamatwa. Hilo litakua kosa la kiufundi.

1. Kugoma Ni Haki yao kimsingi
2. Viongozi wao kutoa taarifa ya mgomo kwa wanachama wao si kosa.

Nawahakikishia mkiwakamata Viongozi huo mgomo mtakuwa mmeuchochea maana wataanza kugoma kushinikiza waachiwe mkiwaachia watarudi kwenye madai yao.

Solution Ni kukaa nao na si vitisho.
 
Back
Top Bottom