Hata hviyo alisema ni dhahiri kuwa kukatishwa ghafla kwa mkataba huo, kutaiathiri kampuni ya Majembe hivyo ili kukabiliana na tatizo hilo, kampuni hiyo sasa inafanya tathmini ya hasara na kupata ushauri wa kisheria. "Agizo la waziri kutaka mkataba huo uvunjwe Desemba 31 mwaka huu, litafanya mkataba huo uvunjwe mwezi mmoja kabla ya kumalizika jambo ambalo kwa vyovyote, litailetea hasara kampuni," alisema Motto.