SUMATRA na ratiba mpya ya mabasi

SUMATRA na ratiba mpya ya mabasi

Nani analala kwenye kiti! unapanda bus la Dar Dom, unachukua hotel unalala kesho yake unapanda bunda bus Dom Mwanza.
Umetisha, mfano unasafiri na mzazi, dada, kaka, kwenye basi mnamizigo, mnafika dom mnashusha mizigo yenu, mnaanza kutafuta hotel, na mmefika kipindi bunge limeanza, hivyo inabidi mkodi tax kuifuata hotel, asubui tena hivyo, tengeza picha km hiyo, alafu asubui unakuta bunda limejaa, hivyo mlale tena!!!
 
Mkuu eddy mimi nasema madereva wazuri wapo wachache ndio maana nasisitiza tusafiri tuu mchana..izo semi treiler horse power zake nyingi ni kubwa unakuta lina mzigo linakimbia kama basi scania R 420 hp 420 na kuendekea kulipita ufanye kazi..mimi binafsi nasafiri sana usiku na mchana ikibidi umbali mrefu madereva wa usiku ni wachache sana naona wapo ok...dereva anaendesha anavyotaka utadhani kabeba mbao..
 
ukisikia vituko ndio hivi, akili zetu kama za fundi seremala kila sehemu gonga msumari, isitoshe sababu za kuzuia magari yasitembee usiku ni za ajabu tu, fikiria unatoka Dar unaambiwa ulale misigiri kisa sekenke kuna majambazi yaani ka mlima kama kichuguu askari wameshindwa kuwadhibiti hao majambazi miaka ishirini sasa? tukiwa na misitu kama rwelu triangle itakuwaje?
mbona hao ulowataja ndo majambazi wenyewe.
 
Mkuu eddy mimi nasema madereva wazuri wapo wachache ndio maana nasisitiza tusafiri tuu mchana..izo semi treiler horse power zake nyingi ni kubwa unakuta lina mzigo linakimbia kama basi scania R 420 hp 420 na kuendekea kulipita ufanye kazi..mimi binafsi nasafiri sana usiku na mchana ikibidi umbali mrefu madereva wa usiku ni wachache sana naona wapo ok...dereva anaendesha anavyotaka utadhani kabeba mbao..
jiulize, munafika singida saa 12 jioni, halafu linachochewa linaingia mwanza saa sita usiku, si bora tupelekane mdogo mdogo tusike asubuhi? tizama pale shelui mabasi ya dar yanavyotiririka.
 
Duuuuh hawa Sumatra watakua wanatupa na fedha za kujikimu njiani sisi abiria?
 
no think tank,, taifa halina watu wenye akili kabisa jamani...hivi mnafanya research kweli?? au mnalala tu na wake zenu na kudiscuss jioni na watoto wenu sebuleni halafu mnaleta mawazo mfu kama haya??
miaka inaenda tu kila kukisha mnaibua vitu vipya na ajali zipo palepale, chanzo cha ajali mpaka sasa hamkijui, mmewageuza polisi na traffic watoza ushuru.. wafanye research mje na solution ya kudumu jamani!!
 
mkuu Eddy huwezi nishawishi kwa lolote mabasi tunayo machache na hayasafiri umbali mrefu ajali za kutosha wewe basi linapata ajali ndani ya mji na abiria wanapoteza maisha hawapo makini hata wakiambia siku mbili sawa tuu mtafika salama...kuriko ivi sasa ajali ajali tuu
 
Ajali zinasababishwa na mambo mengi kama ubora wa barabara, matairi na madereva lakini sumatra ni kama wameng'ang'ania chanzo kimoja tu
 
WANATAKA KUTUMBUA MAJIPU NA HUKU TENA AU MAANA MM SIONA SABABU YA MAGARI KUTOKUTEMBEA ROUT ZA USIKU KWANI TATIZO NINI
 
Ni upuuzi tu, ushawahi sikia ajali za mabasi yanaouwa watu zinatokea usiku? Ni kuongezea garama abiria tu
Wewe umeelewa kweli!
hapo umeambiwa yanafika saa 8 kisha saa 11asubuhi safari ya kugeuka
Hii ina maanisha gari halipati kukaguliwa vyema dereva kachoka nk
 
Wewe umeelewa kweli!
hapo umeambiwa yanafika saa 8 kisha saa 11asubuhi safari ya kugeuka
Hii ina maanisha gari halipati kukaguliwa vyema dereva kachoka nk
basi kama zongtong jipya likitembea km 1200 unataka ulikague nini? wakati linapaswa kukaguliwa likifikisha km 5000.
 
WANATAKA KUTUMBUA MAJIPU NA HUKU TENA AU MAANA MM SIONA SABABU YA MAGARI KUTOKUTEMBEA ROUT ZA USIKU KWANI TATIZO NINI
eti hayatembei usiku wanaogopa majambazi, basi nchi nzima imeenea majambazi, hata somalia haiko hivyo.
 
Kama ni kweli basi nchi hii haitajikomboa ki uchumi. Muda unathamani sana na Muda ukisita umepita. Kila ikifika saa 12 jioni au 4 usiku uchumi unasimama. Kwa mwendo huo hiyo misaada ya wazungu tungali tunaihitaji. Tena sana tu. Huko USA Kuna kipindi watu walifanya kazi kwa saa 14, leo wamefika hapo walipo.
 
Uchumi unazidi kudorora yaani mtu atumie siku 2 barabarani kuja dsm tuu????jee anayeenda china.Yapaswa uchumi wetu uwe wa masaa24
 
Uchumi unazidi kudorora yaani mtu atumie siku 2 barabarani kuja dsm tuu????jee anayeenda china.Yapaswa uchumi wetu uwe wa masaa24
haiwezekani ikifika saa nne usiku nchi nzima inalala, nawasiwasi hata askari wa doria nao hulala, hakuna kiwanda kinachofanyakazi masaa 24, labda vijiwe vya bakurutu tu ndio vinapiga mziki hadi asubuhi.
 
hivi kwanini mabasi ya dar mwanza yasianze safari saa mbili usiku, yatembee usiku kucha yafike mwanza saa tano kesho yake. Na kutoka mwanza yaanze safari saa sita mchana yafike kesho yake asubuhi.
Ingekuwa ivyo ingekuwa powa sana watu tunatembea 24 hrs
 
Dah! jamaa wamezingua yaani mtu apoteze zaidu ya masaa ya 30/32 kwa kutozalisha kwa sababu za kihuni-huni kama hizi!

*Suluisho walete magari yanayoenda kasi kuliko haya tulionayo sasa hivi ili watu japo tupunguze kupoteza muda japo kwa japo isifikie 20/22!
 
Back
Top Bottom