SUMATRA na ratiba mpya ya mabasi

SUMATRA na ratiba mpya ya mabasi

SUMATRA imeanza kutoa ratiba mpya za mabasi ambapo ruti za mbali mf. Mwanza na Mbeya mabasi yatatakiwa kulala njiani na kuingia asubuhi kesho yake kama inavyonekana kwenye ratiba hapa chini.

Hatua hii inakuja ili kuthibiti mabasi kutembea usiku na kuingia mf, Mbeya saa nane usiku, kisha saa 12 asubuhi basi linageuza kurudi Mwanza.

Yapi maoni yako kuhusu hatua hii mpya?

View attachment 333495

A law minus any enforcement mechansm
is as good as a puppys poodle; wemejiandaaje kusimamia utekelezaji wa ratiba hiyoooo??!! Na human error je?! Na rushwa je?! Na vitisho vya vigogo je!?
 
Kwa usiku labda majambazi, ajali nyingi hutokea mchana kweupe kama viroba….
 
Hii imekaa vizuri kwa safari za kikazi, unapata night 4 za kusafiri na 7 za semina. Safi sana sumatra
 
@SUMATRA wekeni utaratibu ambao ni rafiki zaidi. Mfano trip ya Mwanza-Mbeya. Simamieni dereva anaetoka na gari mwanza anabaki Dodoma kusubiri gari ya kampuni hiyo itakayopita hapo Dodoma kesho yake. Hili mkiliwekea mkazo linawezekana. Hivyohivyo, gari linalosafiri trip hivyo lisiruhusiwe kugeuza kesho yake. Kama sikosei trip ya Arusha-Mbeya enzi hizo, mabasi ya Hood yalikuwa yakipumzishwa.
Hivi ishu huwa ni kuipumzisha gari au kuifanyia service, inaweza ikapumzishwa na isifanyiwe service.
 
hapa wanaongeza maabukizi ya ugonjwa wa ukimwi
 
BINADAMU NI WATU WA AJABU SANA,UKITAKA KUWARIDHISHA WOTE LAZIMA UWE KICHAA............................SIJUI WANATAKA NINI?IKITOKEA AJALI WAO NDIO WA KWANZA KUWALAUMU MADEREVA KWA MWENDO KASI,SUMATRA KWA KUTOKUSIMAMIA UTARATIBU..........HAYO YAKITATULIWA WENGINE TENA WANAKOSOA.........DU?
Sasa hapo sumatra wamesaidia nini kama sio kuchosha abiria tu!?......ndugu, kwa mfano kutoka mwanza adi dar sio mbali mpaka kufikia kutembea zaidi ya masaa 24 sasa,bora ata wangeruhusu mabasi yafanye kazi 24 hrs hapo ningeona wanafanya la maana,watembee kwa mwendo ambao upo chini ata ya speed limit, then wafike labda dodoma walale kesho waamshe nasafari wafike dar usiku wake ,huko sinikupoteza mda, kwanini mda ule wanaotakiwa walale hasiingie dereva wa shift nyingine, mbona wenzetu jirani kenya mabasi yana drive 24 hrs na hakuna ajali za ajabu ajabu......tatizo bongo kila mtu anataka aonekane kwenye TV mbele ya mh. Pombe kuwa anawajibika.
 
Miaka ya 1996 huko Tahfif bus lilikua linatoka Nairobi kwenda Mbeya na tulikuwa tunaambiwa linasafiri kwa siku 1 tu..na Mbeya lilikua linaingia saa 4 au 5 usiku na kesho yake linageuza..mpaka linaacha route hiyo sijawahi kusikia limepata ajali..kimsingi kusafiri usiku sio hatari mpaka ionekane njia ya kuzuia ni kulazimisha magari yasafiri mchana tu...maendeleo hayawezi kuja kwa mawazo ya kizamani kama haya, treni za mwendo kasi si ndo zitawachanganya kabisa SUMATRA
Tatizo la sasa hivi ni upatikanaji wa madereva wenye weledi, hakuna chuo kinachofundisha madereva wa mabasi makubwa, wengi wao ni mataniboi wanajifunzia gereji badae anaenda veta kujaribiwa tena kwa dakika kumi. Tajiri hawezi acha peleka bus kisa dereva hakuna, anachukua taniboy yeyote gereji anaingia barabarani, ndio hao kilasiku wanapiga mizinga.
 
Sasa hapo sumatra wamesaidia nini kama sio kuchosha abiria tu!?......ndugu, kwa mfano kutoka mwanza adi dar sio mbali mpaka kufikia kutembea zaidi ya masaa 24 sasa,bora ata wangeruhusu mabasi yafanye kazi 24 hrs hapo ningeona wanafanya la maana,watembee kwa mwendo ambao upo chini ata ya speed limit, then wafike labda dodoma walale kesho waamshe nasafari wafike dar usiku wake ,huko sinikupoteza mda, kwanini mda ule wanaotakiwa walale hasiingie dereva wa shift nyingine, mbona wenzetu jirani kenya mabasi yana drive 24 hrs na hakuna ajali za ajabu ajabu......tatizo bongo kila mtu anataka aonekane kwenye TV mbele ya mh. Pombe kuwa anawajibika.
hivi kwanini mabasi ya dar mwanza yasianze safari saa mbili usiku, yatembee usiku kucha yafike mwanza saa tano kesho yake. Na kutoka mwanza yaanze safari saa sita mchana yafike kesho yake asubuhi.
 
Huu ni upumbavu, ninbora tuanze kutembea na magari yetu binafsi sasa.safari ya 10-12 hrs unatembea siku mbili huu ni udwanzii.
Sie wa Mwanza, tutakuwa tunapanda mabasi ya dodoma tunalala kesho yake tunapanda mabasi ya Mwanza.
 
Wanataka madereva wapate mda wakupumzika. sawa, lakini ingekuwa vizuri zaidi kama madereva wa safare ndefu wangekuwa wanapokezana

Sawa kabisa mkuu, Zambia mabasi ya safari ndefu yana madereva wawili wawili. Yanasafiri usiku kucha na hamana ajali kama kwetu TZ.
 
iyo ya sumatra ipo sawa hao madereva mchana tuu hawazioni kona kali au gari mbele wanapita ivyo ivyo wenyewe wanasema mazima usiku itakuaje naunga mkono hoja madereva wa kuendesha usiku wapo wachache sana kwa iyo ni marufuku..
 
Arusha mpaka Dar ni kama 624km ajali kila leo hapo Tanga km chache tuu ajali nyingi sana..madereva haapo makini huwezi fananisha na walemadereva wa Lusaka mpaka Johannesburg 1500 km basi zinakwenda ukusikia ajali tela limekatika nyuma si si za kijinga kama hapa kwetu wanashindana kufika..
 
Ndio maana tz tunachelewa kwa kila kitu, inakera sana kuona unasafiri asubui unaenda arusha kwa mfano, uamke saa 10 asubui unawahi ubungo, ni ujinga mtupu, kwani nisitoke numbani saa 12 jioni nafika kituoni, by saa 3 safari inaanza, tunafika arusha saa, 12 asubui! Unafanya mambo yako kisha jioni unafanya safari kurudi dar, hii ingesaidia hata mafundi kufanya service mchana kwa uhakika kuliko hivi wanavyofanya kwa kutumia touch.
 
Mmmh itabidi wapunguze na nauli ili angalau mtu ubakiwe na hela ya kula usiku na mchana
 
Sie wa Mwanza, tutakuwa tunapanda mabasi ya dodoma tunalala kesho yake tunapanda mabasi ya Mwanza.
Kulala kupi kunakozungumziwa? Hivi unajipinda kwenye kiti cha basi hadi kunakucha alafu unasema mmelala? Au kwenye bench kisha unasema kabisa tumelala dodoma!!
 
Kulala kupi kunakozungumziwa? Hivi unajipinda kwenye kiti cha basi hadi kunakucha alafu unasema mmelala? Au kwenye bench kisha unasema kabisa tumelala dodoma!!
Nani analala kwenye kiti! unapanda bus la Dar Dom, unachukua hotel unalala kesho yake unapanda bunda bus Dom Mwanza.
 
Ndio maana tz tunachelewa kwa kila kitu, inakera sana kuona unasafiri asubui unaenda arusha kwa mfano, uamke saa 10 asubui unawahi ubungo, ni ujinga mtupu, kwani nisitoke numbani saa 12 jioni nafika kituoni, by saa 3 safari inaanza, tunafika arusha saa, 12 asubui! Unafanya mambo yako kisha jioni unafanya safari kurudi dar, hii ingesaidia hata mafundi kufanya service mchana kwa uhakika kuliko hivi wanavyofanya kwa kutumia touch.
Hivi kuna sababu gani ya kuzuia bus za Arusha Dar zisitembee usiku? kama ni majambazi basi jeshi letu la watu waoga sana, ukweli bus za Arusha zilipaswa zianze safari saa 3 usiku na kufika arusha saa 12 asubuhi.
 
iyo ya sumatra ipo sawa hao madereva mchana tuu hawazioni kona kali au gari mbele wanapita ivyo ivyo wenyewe wanasema mazima usiku itakuaje naunga mkono hoja madereva wa kuendesha usiku wapo wachache sana kwa iyo ni marufuku..
Tatizo la mchana unakuta mtu ana noah amekomaa barabarani unapiga honi hataki kupisha na bus ndio limechochea, kuna masemitrela yanakimbia kama boeng ukiliovertake nalenyewe linachochea zaidi bora bus zitembee usiku na mchana tuwaachie wenye noah na vitara.
 
Back
Top Bottom