tonicimmobility
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 493
- 1,038
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Nyasa, Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu ameeleza kuridhishwa na kile alichokiita mchango wa viongozi wa zamani na wa sasa katika kutetea haki na masilahi ya Watanzania.
Sugu ameyasema hayo siku ya Jumatano akizungumza na wanahabari moja kwa moja kupitia televisheni mtandao ambapo amesisitiza kuwa ni wakati muafaka kwa Watanzania wa makundi mbalimbali kama vile wastaafu, vijana, wanawake, na wafanyakazi kuungana na kutoa maoni yao kwa ajili ya amani na maendeleo ya taifa.
Soma pia: Polepole: Nilishajiapiza baba yangu mzee Polepole ndiye Mtu wa mwisho kuonewa katika nchi hii
“Nichukue fursa hii kutambua kwa kazi kubwa ya Bishop Josephat Gwajima na Balozi Humphrey Polepole... hata kama kuna rekodi za kauli au matendo yao ya huko nyuma ambavyo hatukubaliani navyo, lakini wametubu, wanazungumza kwa niaba ya nchi, basi tunawasamehe kwa sasa ili tuunganishe sauti hizi za Watanzania wote katika kuhakikisha nchi hii inakaa sawa”, amesema Sugu.
Sugu ameyasema hayo siku ya Jumatano akizungumza na wanahabari moja kwa moja kupitia televisheni mtandao ambapo amesisitiza kuwa ni wakati muafaka kwa Watanzania wa makundi mbalimbali kama vile wastaafu, vijana, wanawake, na wafanyakazi kuungana na kutoa maoni yao kwa ajili ya amani na maendeleo ya taifa.
Soma pia: Polepole: Nilishajiapiza baba yangu mzee Polepole ndiye Mtu wa mwisho kuonewa katika nchi hii
“Nichukue fursa hii kutambua kwa kazi kubwa ya Bishop Josephat Gwajima na Balozi Humphrey Polepole... hata kama kuna rekodi za kauli au matendo yao ya huko nyuma ambavyo hatukubaliani navyo, lakini wametubu, wanazungumza kwa niaba ya nchi, basi tunawasamehe kwa sasa ili tuunganishe sauti hizi za Watanzania wote katika kuhakikisha nchi hii inakaa sawa”, amesema Sugu.