Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 57,188
- 128,908
Mbunge wa Mbeya Mjini Mhe. Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu, leo amemwaga cheche bungeni kwa kuiwakia serikali kuhusu vurugu za wamachinga Mbeya hivyo kutaka tume huru iundwe ili kuchunguza kadhia hiyo.
Mhe. Mbilinyi ametoa cheche hizo bungeni mjini Dodoma wakati wa kujadili Tanzania kuridhia mkataba wa kimataifa wa haki za vijana wa Afrika.
kufuatia vurugu hizo, Sugu amesema mgambo walishindwa, polisi walishindwa, FFU walishindwa na jeshi pia lilishindwa, lakini wakazi wa Mbeya ndio wanaomjua ni nani alituliza vurugu zile!.
Sugu alisema kwa hasira kuwa kijana msukuma guta John Bosco aliuwawa kwa risasi huku diwani wa CCM akidai yeye ni nesi na siku hiyo alijuwa zamu, hakuna mtu yoyote aliyeumia wala kufariki!. Ametoa RIP kwa kijana huyo na kuomba matokeo ya tume tume yasisitize fidia kwa wahanga wa vurugu hizo!.
Sugu ameitaka serikali kutowanyanyasa tena machinga bali waachiwe kufanya shughuli zao kwa uhuru kama alivyofanya Satta wa Zambia mpaka hapo serikali itakapo wapatia utaratibu maalum.
Pongezi za dhati kwa Mhe. Sugu na pongezi kwa Chadema kutuingizia watu kama hawa Bungeni.
Pasco
Mhe. Mbilinyi ametoa cheche hizo bungeni mjini Dodoma wakati wa kujadili Tanzania kuridhia mkataba wa kimataifa wa haki za vijana wa Afrika.
kufuatia vurugu hizo, Sugu amesema mgambo walishindwa, polisi walishindwa, FFU walishindwa na jeshi pia lilishindwa, lakini wakazi wa Mbeya ndio wanaomjua ni nani alituliza vurugu zile!.
Sugu alisema kwa hasira kuwa kijana msukuma guta John Bosco aliuwawa kwa risasi huku diwani wa CCM akidai yeye ni nesi na siku hiyo alijuwa zamu, hakuna mtu yoyote aliyeumia wala kufariki!. Ametoa RIP kwa kijana huyo na kuomba matokeo ya tume tume yasisitize fidia kwa wahanga wa vurugu hizo!.
Sugu ameitaka serikali kutowanyanyasa tena machinga bali waachiwe kufanya shughuli zao kwa uhuru kama alivyofanya Satta wa Zambia mpaka hapo serikali itakapo wapatia utaratibu maalum.
Pongezi za dhati kwa Mhe. Sugu na pongezi kwa Chadema kutuingizia watu kama hawa Bungeni.
Pasco